Friday, March 21, 2014

TAARIFA KUHUSU SIKU YA HALI YA HEWA DUNIANI

Na Miza Kona Maelezo Zanzibar
Mamlaka ya Hali ya HewaTanzania imewataka vijana nchini kuchukua hatua za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa ili kizazi kijacho kiweze kufaidi dunia yenye mazingira bora.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani ,imewataka vijana kujihusisha na masuala ya hali ya hewa ili kupata maarifa na uelewa wa hatua za kuchukua katika kipindi hiki cha mabadiliko ya hali ya hewa duniani.

Taarifa hiyo mewataka vijana walioko mashuleni, vyuoni na wajasiriamali kushiriki katika kuokoa dunia kutoka kwenye majanga yaletwayo na mabadiliko ya hali ya hewa na chachu kubwa ni kuhakikisha vijana wanakuwa mstari wa mbele katika kufuatilia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na Mamlaka hiyo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Siku ya Hali ya Hewa Duniani ni siku ya kutafakari juhudi zinazochukuliwa na Wanasayansi Duniani katika kufahamisha Dunia kuchukua tahadhari juu ya mabadiliko ya hali ya hewa na athari zake.

Mamlaka ya Hali ya Hewa inawakaribisha wananchi kutembelea vituo vya hali ya hewa nchini ili kuona shughuli zinazotolewa na Mamlaka hiyo kuanzia kesho
Siku ya hali ya hewa duniani huadhimishwa kila ifikapo tarehe 23 Machi ya kila mwaka na ujumbe wa mwaka huu ni Ushirikishwaji wa vijana katika masuala ya hali ya hewa. mwisho

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO.

No comments: