Friday, March 21, 2014

MKENYA ATOA ONYO KWA WATANZANIA


Dodoma. Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wameaswa wasinakili tu michakato ya Kikatiba toka nchi nyingine, kwani yale yafanywayo huko hayataakisi wala kukidhi matakwa ya Watanzania.

Hayo yalibainishwa na Mwanasheria Mkuu wa zamani wa Kenya, Amos Wako mjini Dodoma leo, wakati akielezea yale Kenya iliyokumbana nayo wakati ikiandika Katiba yake mpya.

“Mnaposikiliza uzoefu wa nchi nyingine, tafadhali msiwanakili, msije mkarudia makosa yao,” alisema Wako ambaye hivi sasa ni Seneta wa Kaunti ya Busia, akiongeza: “Hata kama mmependa waliyoyafanya, yawezekana yasiwafae [Watanzania].”

Vilevile, Bw. Wako aliipongeza Tanzania kwa kuwa tayari kupeleka mapendekezo ya Bunge Maalum la Katiba moja kwa moja kwa wananchi, akisisitiza kuwa uamuzi huo utazuia rasimu isije ikachakachuliwa na wanasiasa.

“Kama [rasimu] ingepitiwa na chombo kingine [kabla ya kwenda kwa wananchi], yawezekana ikafanyiwa mabadiliko yasiyo na maslahi [kwa umma],” alisema nguli huyo wa sheria.

Ungepende kufahamu kilichojiri baada ya hotuba ya Wako? Je, Mchungaji Christopher Mtikila aliibua suala gani leo?


Tazama VIDEO ufahamu mengine yalotokea leo Dodoma.
Chanzo: Mwananchi

No comments: