Tuesday, November 12, 2013

NITAMNG’OA SPIKA MAKINDA-MBUNGE




Mbunge wa Nzegamkoani Tabora ,Dkt.Hamisi Kig wangalla ,amesema bado ana dhamira ya kuwasi lisha hoja ya kumng’ oa madarakani Spika wa B unge, Bi.Anne Makinda.
Alisema uvumi ulioenea kuwa hoja yake imeondolewa kwa agizo la Chama Cha Mapinduzi (CCM), hauna ukweli.

Dkt. Kigwangalla aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika mkutano wa hadhara u lioshirikisha wakazi wa jimbo hilo na vitongoji vya ke uliofanyika katika Uwanja wa Parking.

Katika mkutano huo, Dkt. Kigwangalla aliulizwa swali na mkazi wa jimbo hilo kama kweli ana ubavu wa kumng’oa Bi.Makinda, anayetoka na na chama chake.
“Mheshimiwa mbunge,naomba utu thibitishie kama una uwezo wa kumng’oa Spika wa Bunge (Makinda), kama ulivyotangaza dhamira ya kuw asilisha hoja binafsi bungeni ili bunge liweze kumng’oa.

“Kwa jinsi tunavyofahamu utaratibu ndan i ya CCM, huna ubavu wa kufanya hivyo , ina onesha ulikuwa ukijifurahisha tu,”alihoji mwananchi huyo.
Mwananchi huyo aliongeza kuwa, kwa kawaida CCM ina utaratibu wa kuzuia hatua mbalimbali zinazotaka kuchukuliwa na wanachama wake hivyo alimshauri Dkt.Kigwangalla, aacha ne na hoja hiyo kwani hana ubavu wa kumng’oa Bi.Makinda.

Akijibu swali hilo,Dkt. Kigwangalla alisema,si kw eli kwamba CCM ina utaratibu wa kuondoa kin yemela hoja ambazo haikubaliani nazo ambapo suala la kutaka kumng’oa Bi. Makinda lipo ndani ya uwezo wake na kufafanua kuwa, ho ja hiyo haijaondolewa na hivi sasa ipo katika hatua za mwisho ili iweze kufikishwa bungeni.

“Kwa hili la kumng’oa Spika wa Bunge,niwaele ze wazi kuwa si kweli linaweza kunishinda... hoja imewasilishwa na Bi. Makin da atang’oka kama nikiamua kuendelea nayo kwa sababu tayari hoja nimeiwasilisha na nimekidhi masharti yote.
“Hivi tunavyoongea, hoja yangu tayari imeto ka hatua ya kwanza na kukidhi vigezo vyote sasa inaenda hatua ya pili ambayo Kamati ya Bunge y a Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge,itaamua hoja yangu iingizwe bungeni au isiingizwe,”alisema .

Aliongeza kuwa,baada ya hapo utafuata mcha kato wa mwisho ambao ni hoja hiyo kufikishwa bungeni na yeye kuiwasilisha rasmi mbele y a Bunge ili kufanyiwa uamuzi na wabunge wote kwa kupiga kura na kama atashinda au kushind wa,hilo ni jambo lingine.
Dkt.Kigwangalla alisema uamuzi wa kuo ndoka au kutoondoka kwa Spika, kutategeme au amuzi wa wabunge wenzake na kusisitiza kuwa , CCM haiwezi kuzuia hoja hiyo bila ya kupatiwa uamuzi na wabunge wote.

Akijibu swali ambalo lilihusiana na fedha za ushuru wa huduma zilizotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Resolute, ulioko wilayani humo, Dkt. Kigwangalla alisema fedha hizo sh.bilioni2.340,zililipwa na mgodi huo na s asa zimehifadhiwa katika akaunti maalumu ili baadaye zitumike kama mtaji wa kuanzishia Benki ya Maendeleo ya Wananchi wa Nzega.

“Fedha hizi tulizipigania kwa kiasi kikubwa hadi kuandamana lakini tulifanikiwa kuzipata, niwathibitishie zipo salama katika akaunti maalumu tuliyoianzisha ili baadaye ziweze kuanzisha Benki yetu ya Maendeleo ambayo itaweza kutupa mikopo ya kuendesha shughuli zetu,”alisema .

Alisema lengo lake ni kuhakikisha fedha hizo zinatumika vizuri ili kuwasaidia wananchi w a Nzega kubadilisha maisha yao ambapo watu watahamasishwa kujiunga katika ushirika au SACCOS ili waweze kupewa mikopo p ia zitatumika kununulia mitambo ya kutengeneza barabara na uchimbaji visima vya maji.

Gazeti moja linalotoka kila siku (si Majira), liliandika habari inayosema Dkt. Kigwangalla anadai Bi. Makinda amekiuka kanuni kwa kuidhinisha malipo ya sh. 430,000 kama posho kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, tofauti na wajumbe wa kamati nyingine ambao malipo yao ni sh. 180,000 kwa siku.

Hoja hiyo ilipingwa vikali na baadhi ya wabunge akiwemo Mbunge wa Tabora Mjini, Bw. Ismail Aden Rage (CCM) na Mbunge wa Kigoma Kusini, Bw. David Kafulila (NCCR-Mageuzi) ambao walidai hawaoni sababu ya kumuondoa Bi. Makinda madarakani.

Bw. Kafulila alisema hilo ni suala la wana-CCM, kwani Bi. Makinda aking’olewa madarakani, mtu ambaye ataziba pengo lake hawezi kutoka upinzani. Hoja hiyo ya Dkt. Kigwangalla iliibua mjadala kwa baadhi ya wabunge na wengine kukataa kusaini karatasi ambayo walipelekewa ili kuunga mkono.

Mbunge wa Ludewa, mkoani Njombe, Bw. Deo Filikunjombe, alisema hoja ya Dkt. Kigwangalla imejengwa katika msingi hafifu isiyozingatia masilahi mapana ya nchi na mtazamo finyu.
Chanzo: Majira

No comments: