Monday, January 28, 2013

“MAGAZETI YA UDAKU NI JANGA LA TANZANIA”



JOHN F. KENNEDY (1917-1963)
“There is a traffic disadvantage in not having the abrasive quality of the press applied to you daily. Even though we never like it, and even though we wish they didn’t it, and even though we disapprove, there isn’t any doubt that we could not do the job at all in a free society without a very, very active press”.
                                  John F. Kennedy (1917-1963).
MAKALA YA CHIWAMBO
“MAGAZETI YA UDAKU NI JANGA LA TANZANIA”
                 
Nakubaliana sana na maneno ya President J. F. Kennedy aliposema “kuna hasara kubwa sana kwa kutokuwa na vyombo vya habari vye ubora. Do you know why? Vyombo vingi vya habari nchini vinapotoa zaidi habari za udaku inachangia mawazo ya watu kudumaa na kushindwa kufikiri nini tufanye ili kujiletea maendeleo ya mtu binafsi. Hizi gazeti au tv zenye ubora kwa kawaida hazipedwi. Kwa mfano Nchiya Tanzania kuna gazeti la Raia Mwema, Mwananchi, The citizen, The Gudian, Nipashe na hata lile lililofungiwa na serikali Gazeti la Mwanahalisi, ni         watu wachache ndio wanaosoma gazeti hizi. 
 
              Pia hata Wasomi wetu vyuoni wahasomi. Walio wengi wanasoma magazeti ya udaku na yale ya sport. Pamefikia mwanafunzi unamuuliza hivi leo kuja jambo gani limefunika sana vyombo vya habari mbalimbali. Atakujibu do you know what? Muda sina.
 
      Huyu mwanafunzi wa chuo kikuu anasema muda wa kusoma gazeti ambazoni quality News anasema hana time ila kwenye michezo hata akiliona la juzi au mwakajana anatamani liwe lake asome. Ninyi kama tegemeo letu la taifa mnadhani tutafika kweli.
 
      Mara nyingi utasikia “RAIS AFANYA MAUAJI YA KUFURU”, CHIWAMBO ZE DOCTOR KAFUMANIWA LIVE, WAZIRI AUSI KAKUTWA NA PEMBE ZA TEMBO”. Mmmmmmmmh!!!! Ingia humo ndani usomo uone utumbo uliopo. Hauendani na kitu wanachozungumzia. Eti Rais wanayemzungumzia ni Yule wa wajinga Chikaje street.
 
     Kwanini waandishi kama hawa wasifungiwe tu. Je elimu yake ina faida gani. Kama ana “LAW DEFORMATION” kwanini anashindwa kuandika kitu kinachoendana na hali halisi. Ama kweli “KILIO CHA SAMAKI MACHOZI HUISHIA MAJINI”. Huwezi kuona watanzania wanatesekaje huko chini. Wewe mwandishi wetu taifa linakutegemea sana.
 
      Kulaumu wanafunzi nao sio zuri bali tuangalie zaidi kwa hawa waandishi uchwara wa magazeti yetu. Pamefikia mahali mtu uachoka hata kusoma gazeti husika kwa sababu mwandishi anaonekana anapendelea sana chama Fulani, au sehemu Fulani.
 
       Kwa mfano Tv zilizonyingi Tanzania kama vile Cloud Tv pia wanaangalia zaidi taarifa za majijini na mikoani. Hivi jiulize mara ngapi wanaripoti habari za vijijini. Hikinacho kinachangia kupoteza ubora wa tv zetu. Hata hizi tv media nyingine nazo ni vile vile wanaangalia zaidi Dar es salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya. Hivi kule Kigoma, Rukwa na Mikoa ya kusini mbona hawalipoti matukio kama kule mijini.
 
Ukweli ni kwamba vijijini watu walio wengi wanateseka; hawana huduma za jamii. Umeme kwao ni ndoto. Wanauona wakiwa mjini tu. Kwa msingi huo serikali inataka kufungia matumizi ya analogia bila kuangalia hawa wanakijiji ambao ni asilimia 80% ya Watanzania kweli wataweza kutumia digitari. Kama chakula tu ni shida je mtu alipie king’amuzi ataweza.
 
  Watanzania vijijini wamekata tamaa. Hawana wa kumweleza shida zao,sauti yao imefunikwa na waandishi uchwara ambao wamenunuliwa. Nakumbuka kwamba kipindi nasoma St. Augustine university of Tanzania 2011 katika kozi ya NEWS REPORTING chini ya Mwalimu wangu Madam Mushi,  alinifundisha namna ya kwenda kupata taarifa vijijini. Hapo ndipo aliponikalilisha kuwa maana ya Jonalist “Is the voice of the voiceless”. Hatu Lecture wangu Denis Mpagaze pia alikuwa analizungumzia sana neon hili.
 
Mimi naweza kujiita ni mwanafunzi wa Danis Mpagaze kwa kuwa amenifundisha. Huyu ni Msomi nan i Mwandishi ya jarida la “Physiognomy” pia ni Lecture st. Augistine University-Mwanza. Nilifurahia sana na Documentary zake ambapo alituonyesha mwanga juu ya Uandishi wa habari kwa kutuonyesha documentary ya “Mto tigite” namna watu walivyopalika ngozi na kugeuka kuwa rangi tofauti na walizonazo. 
 
Ukiangalia documentary hiyo utaona namna watanzania vijijini walivyokata tama. Hawana imani na hata viongozi wao kwa kukosa kuwatetea. Haya nimeyathibitisha baada ya kutembelea kijiji kimoja cha wilaya ya Newala kijiji cha Kitangali A, pia hata maeneo mengine ya kusini kama vile kijiji cha Mtama (Masasi), Namakambale B, Azimio,(Tunduru).
 
Hivyo somo langu la bure kwa waandishi wa habari ni kwamba mutembelee vijijini kuliko mijini.
 
   AUSI CHIWAMBO
TEKU UNIVERSITY
MBEYA
ausichiwambor@gmail.com
  

PICHA HALISI ZINAZOONESHA KUANZA KWA MAANDAMANO MTWARA SIKU YA KWANZA MWISHONI MWA MWAKA 2012 HADI SASA


 Mwanzoni mwa maandamano yaliyotokea Mtwara yalipambwa na Mabango ya aina hii. Hii ni siku ya kwanza ya maandamano.
Haya ni mabango mengine
 Hizi ni nyaraka za serikali zikiungua moto mjini Masasi Juzi



 Wauguzi wa Hospitali ya Ndanda wakisubili majeruhi

 Nyumba ya Mbunge wa Jimbo la Masasi,Mariam Masembe ambayo ilichomwa moto juzi na watu wenye hasira. Vitu mbalimbali viliharibiwa.Picha na Mpiga Picha Maalum-Mwananchi


HILI NI GARI LILILOCHOMWA MOTO IKISEMEKANA GARI HILO LILIKWENDA KUMFUATA BIBI (Upande wa kulia) ALIYESEMA KUWA WAKIAMISHA GESI KWENDA DAR ES SALAAM ITAGEUKA KUWA MAJI




 Hili ni gali la kubebea wagonjwa


Huu  ni siku ya kwanza maandamano yalianza kama inavyoonekana wakiwa na mabango yao yaliyoonesha madai yao




 Hii picha imechukuliwa kutoka Masasi








 Nyumba ya Mbunge wa Jimbo la Masasi,Mariam Masembe ambayo ilichomwa moto juzi na watu wenye hasira. Vitu mbalimbali viliharibiwa.Picha na Mpiga Picha Maalum-Mwananchi

 
 MJI WA MASASI KWA MBALI INAONEKANA NAMNA HII

MAGAZETINI LEO 28-01-2013






Sunday, January 27, 2013

GESI YA MTWARA SASA YAONEKANA KAMA YALE YA LUDISM YALIYOTOKEA WIINGEREREZA


MAKALA NA CHIWAMBO
Kwa wale waliosoma kidato cha Tano na cha sita Katika History 2 wanaweza kuthibitisha hicho kichwa cha habari. Kipindi kile Nedy Ludy ilifanikiwa kuhalibu viwanda,Majumba na vingine vingi kwa sababu eti ya ugunduzi wa viwanda ambapo nchi hiyo ilipitia kipindi cha mageuzi kutoka kutegemea kilimo na kuingia mapinduzi ya viwanda.  Wananchi wengi waliona hali hile ni tete kwani hawakuweza kunufahika badala yake ni mwendo wa mateso tupu. Waliamua kuchoma moto viwanda kimya kimya.

Kwa wale waliotembelea mikoa ya kusini na wilaya zake ikiwemo Tunduru unaweza kusema kule sio Tanzania. Ni kama nchi nyingine hivi. je tUnaweza kusema viongozi waliotokea kusini wana lahana? Nakumbuka kama dishi langu halijakaa sawa basi hata Rais wa awamu ya Tatu ni wa Masasi pale Lupaso. ameifanyia nini kusini kwa miaka yote aliyokuwepo kule?

 je amechangia kuua bandari ya Mtwara? waangalie viongozi wa sasa wanavyovutia gesi iende mtwara. sasa unaweza kujiuliza kwamba hivi hawa viongozi ni wazalendo kweli? wanafanya nini huko waliko? Kusini sasa hali imekuwa kama vita. vita vinavyojulikana vita vya gesi. kila kona Tanzania wanazungumzia. sasa wavamia ofisi za umma, mahakama zinachomwa moto, nyumba za wabunge zinateketezwa. hali ni tete. ni balaa. wanakusini sasa wamechoka na mfumo uliopo?

 Nasikia eti yule kiongozi mkuu wetu bwana Mkubwa yupo nchi za wenzetu kujadili masula ya nchi za wengine na kusahau vita baridi na ya moto iliyopo Tanzania. Hadi sasa hatujasikia mataifa makubwa duniani wakisema chochote. naamini wanasubiri iongezeka nao walete mandege kama yale ya mali ili kuwauwa wanakusini? Hapo ndipo watapoamini kwamba hali imekuwa tete? kw nini tusubili waingereza au Ufaransa wakileta yale madege? mungu ibaliki Tanzania.

Tusifike huko kwani mimi ni ni Mwanakusini ambao sipo tayari kuona Tanzania ivamiwe na wakoloni wale waliotutawala kama mali. Tujiulize nani wamesababisha haya. viongozi wetu wanahusikaje juu ya hili? je kauli zao zinaleta tija kwa wanakusini? kwa upande wangu naamini kauli za viongozi zinaweza kuleta vita au la kule kusini. hata Nchini Mali ilianza wa Mvutano kati ya serikali na wananchi hasa waasi. munakumbuka Misri ilikuwaje? ni jukumu lenu viongozi kuakikisha mapatano ya maridhiano ni muhimu zaidi kuliko tunakoelekea.

 Damu inayomwagika Kusini itadumu vizazi na vizazi kama mgogoro hautatatuliwa. Kwa wale waliofuatilia uasi wa Nigeria, na Sudani zote mbili wataona au waliona namna mafuta yalivyosababisha mtafaruku wa nchi. Vita visivyo na mwisho. Sipendi kuona kusini yangu inagawanywa na kuwa nchi nyingine? je itaitwaje? hili sio jambo jema. Hili jambo ni hatari. Serikali jamani kwanini musichukue hatua ya amani kuliko vita iliyoko sasa. Kwa kawaida umma unanguvu zaidi kuliko majeshi. Kwani ukiua wote kule kusini wataishi nani? maana pakifikia mahali watu wapo tayari kufa kwa ajili ya kutetea maslahi yao ona hapo pana jambo. njia pekee ni kukaa meza moja tu.
Hakuna jipya zaidi ya hilo. serikali ikubali imeshindwa vinginevyo inaweza kutokea yale ya Ludism kule wingereza miaka ya nyuma sana. Sasa serikali itumie Wanasaikolojia na wanasosholojia ambao ni wataalamu wa jamii yao ili kutatua mgogoro huu. naamini viongozi wetu watazuia ili ofisi na majumba yasichomwe moto kama Ludism.
HALI YA USAFIRI KUSINI
Hali ya usafiri kusini ni aibu. Unaweza kusema haijawai kuwa na Rais kutoka kusini. Pia utajiuliza hawa viongozi wa kule kusini wanafanya nini? Tuna wabunge wengi kweli kweli. Tunduru peke yake inawabunge wawili akiwamo Injinia Makani na Mtutura. Je hawa watu wa kusini Hasa Tunduru, Lindi na Mwata watafaidikaje na gesi iliyopo kusini? Baraara tangia uhuru haijajengwa. Ni wimbo wa Taifa wakati wa kampeni. Kuna kupindi walikuwa wanasafiri kwa kutumia meli lakini sasa bandari ilikufa tunaendelea kupata tabu ya usafiri.
Ukiwauliza viongozi wetu wameifanyia nini kusini watakujibu Tumejenga lile daraja kubwa nchini Tanzania ya Mkapa na ile ya Msumbiji. Inawezekana hawa viongozi wanapita kwa anga tu. Uangalie chini kuna nini unafili wataweza? Hali ni mbaya. Nawaomba mujalibu kutembelea kusini ukizunguka kuanzia Namtumbo, shuka chini hadi Tunduru, kasha usikae pale Tunduru teremuka hadi Masasi kasha pandisha hadi Hotel ya Nangurukuru Mkoani Lindi.
Sasa ukianzia hapo Nangurukuru kuelekea Daraja la Mkapa utaomba kama lingekuja wingi lizoe tope zote ziwekwe pembeni ili mupite kwa amani na utulivu. Kulala nchiani ni kawaida kule kwetu. Unapaswa uwe na Biskuti, ikiwezekana pika kabisa ugali au chukua unga na dagaa wakati wa kusafiri ili usife njaa maana gari likiingia kwenye tope mbona mutakesha.
Kwa kifupi hizo barabara nilizozitaja ni mbaya mno. Tangu uhuru hazijajengwa. Na madai ya hawa wanakusini wanasema iweje bomba la gesi lijengwe miezi 18 tu wakati barabara tangu uhuru bado?

PICHA ZINAZOONESHA MATUKIO YA MKOANI MTWARA

Kulia ni Rais Kikwete, na Kushoro ni Prof. Ibrahim Lipumba 

 
HILI NI GARI LILILOCHOMWA MOTO IKISEMEKANA GARI HILO LILIKWENDA KUMFUATA BIBI (Upande wa kulia) ALIYESEMA KUWA WAKIAMISHA GESI KWENDA DAR ES SALAAM ITAGEUKA KUWA MAJI


Hizi ni nyaraka za serikali zikiungua moto mjini Masasi Juzi
Picha hii imewekwa inaonesha hali ya usafiri Mikoa ya Kusini. Walio wengi wanadai kuwa iweje bomba la gesi lijengwe miaka miwili wakati Barabara hii tangia uhuru wa Tanzania hadi leo haijawekwa lami?
Nyumba ya Mbunge wa Jimbo la Masasi,Mariam Masembe ambayo ilichomwa moto juzi na watu wenye hasira. Vitu mbalimbali viliharibiwa.Picha na Mpiga Picha Maalum-Mwananchi
Hii ni katuni ya Masudi Kipanya ikionesha kuwa ukitembelea na kuamia mtwara unaweza kuwa tajiri eti kwa kuwa gesi inapatikana hapo.
Rais wa Awamu ya Tatu Mh. Benjamin W. Mkapa aliyetoa kauli kwamba wananchi wasitishe maandamano badala yake wakae meza moja ya mazungumzo ili kufikia muhafaka.