Thursday, June 21, 2012

BUSARA ITUMIKE KUZUNGUMZIA MGOGORO WA ZANZIBAR


BUSARA ITUMIKE KUZUNGUMZIA MGOGORO WA ZANZIBAR
Chiwambo Asi R.
Zanzibar mwishoni mwa wiki iliyopita tulishuhudia machafuko makubwa sana. Ikihusisha vitendo vya uchomaji wa makanisa, uhalibifu wa mali za umma, na wengine kuwekwa ndani. Hili si jambo tu la kukurupuka na kuanza kubeza sana upande mmoja kwani kila jambo ni matokeo ya mfumo Fulani.

Taasisi iliyoingia kashfa hiyo ni Taasisi ya UAMSHO ikiwa chini ya baadhi ya waislamu Zanzibar. Zanzibar wanataka nchi yao iwe huru, wakati watanganyika tunataka Zanzibar iendelee kuwa hru. Na cha kusikitisha zaidi lile baraza la usuruhisho masuala ya muungano ni raia wa Zanzibar. Hakuna Mtanganyika pale.

Ofisi inayohusika na masuala ya muungano ni ofisi ya Makamu wa rais. Na hata walio kwenye kamati hiyo wote ni  Wazanzibar. Hivi unadhani kama ikitokea wao hawautaki muungano unadhani kwamba wataleta majibu yaliyo sahihi? Hawa ni viongozi wetu, tuendelee kuwaamini kwani tushike ule usemi usemao kiongozi ni kioo cha jamii.

Makundi yeyote yanavyoanzishwa huanza na  Hatua (stage) zake. Kila hatua inajitegemea kama ifuatavyo:-
  1. Hatua ya kwanza ya kuunda Kikundi. (Preliminary or incipiency stage). Hapa ndipo vichwa vya watu vinapogongana kimawazo juu ya kit Fulani kwenda tofauti. Viongozi hutokea ambao si rasimi na kuanza kuonesha hisia zao.
  2. hatua ya pili ambayo inahsisha kuanza kutengeneza kundi na kuongeza uelewa kwa watu (Coalescence stage). Hapa panahitaji viongozi ambao wataongeza ukaribu na watu wengine. Kipindi kingine wanazungumzia mawazo yao yote hata kupitia vyombo vya habari.
  3. hatua ya nne ambapo kikundi kimekomaa na kufikia kilele cha kundi (Institutionalization or Bureaucratization stage). Hapa viongozi wanakuwa ni wakuchaguliwa na ufata mfumo wa taasisi Fulani (chain of command). Na viongozi hao hulipwa kiasi cha fedha.
  4. Anguko. (Decline stage).hapa ni sehemu ya mwisho kabisa ambapo ni anguko ku la kundi lililoundwa katika hatua ya kwanza. Hapa kundi hili usambaratika kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kufanikiwa kwa lengo lao, au kusambaratishwa.

Hizo ndizo hatua za makundi yanavyotokea. Hivi viongozi wetu hawakuziona hatua kama hizi? Kama kweli tunautaka muungano kwanini serikali iliwaachia uhamsho kuendesha mijadala yake huku wakijua kuwa wanazidi kulikuza zaidi kundi hili? Huu ni uasi au ni nini? Kwa upande wangu naona kwamba ni uzembe wa watu wachache ndio uliopelekea visiwa vya Zanzibar kuingia kwenye machafuko.

Kwa kiongozi yeyote aliyesomea masuala ya uongozi au jamiii lazima amezisoma hatua kama hizi na namna ya kuyasambaratisha haya makundi. Kwanini zisitumike ikiwemo njia za amani. Makundi haya yalipata uchungu zaidi pale viongozi wa taasisi zisizo za kiserikali walipokamatwa na jeshi la polisi katika eneo la bunge kwa madai kuwa ni kinyume na sheria za nchi kwa kifupi nilivyoelewa mimi ni kwamba walikuwa waasi. Ni kweli kabisa.

Lakini ilipaswa itumike busara kutatua mgogoro huu badala ya vitisho. Hawa Wazanzibar walianza kudai Zanzibar ijitenge kwa muda wa miaka mingi sana. Kwa wale wenye kumbukumbu munaweza kumkumbuka yle aliyekuwa rais wa Zanzibar Ndugu Aboud Jumbe Mwinyi alivyotangaza nia ya kutaka kuvunja muungano akiwa Dodoma kwenye vikao Fulani. Kilichompata ni kuondolewa klatika nafasi hiyo.

Nyadhifa zake zote za kichama na serikali alivuliwa kufumba na kufumbua macho. Hii ni kweli kuwa uasi ulianzia muda mrefu sana. Hapo ndipo Mwalimu Nyerere aliposema kuwa tusikubali kuvunja muungano. Hata Nyerere wetu kumbe aliyajua haya mapema hasa pale kundi la G51 lilivyoanza kukua nchini Tanzania.

Kwa hiyo suala la hawa jamaa wa UAMSHO chanzo chake kimetoka mbali. Kwa hiyo kwa wakati huu ambao nchi mbalimbali zinaonyesha namna waasi wanavyoongezeka siku hadi siku, hasa nchi zile za kiarabu na baadhi ya nchi za Kiafrika, napendekeza serikali bora itumie busara zaidi katika kutatua tatizo hili badala ya vitisho na nguvu nyingi. Kweli hawa watu wapo kinyume cha sheria za nchi.

Lakini busara muhimu zaidi kuliko nguvu zaidi. Kwanini serikali isikae nao pamoja na kanza kusikiliza madai yao? Kama yana msingi kwa hatima ya nchi yetu yafanyiwe kazi. Mbona madaktari ilitumika njia kama hii. Kwanini isitumike kule Zanzibar. Inasikitisha kuona kila kukicha vituko Zanzibar mara tunataka nchi yetu.

Haya yamefugwa sana na sisi wenyewe kwani viguvugu lilipoanza hasa katika ule muswada wa maoni ya katiba mpya hawa walichana hadharani na kupinga kujadiliwa. Wakati ule likuwa muhimu kuweza kutafta njia mbadala za kutatua ili kuonyesha namna tunavyoujali muungano wetu.

Nalipenda sana Tanzania hasa hili jina zuri la Tanzania. Kwa hiyo nadhani viongozi wa serikali mutatumia wawazo haya ili kuhakikisha tunabaki na Tanzania moja, Imara na yenye amani na utulivu kama aliotuachia mwalimu Nyerere.

Powered by Chiwambo Ausi R.       

MWANAHARAKATI NA TANZANIA YA LEO


MWANAHARAKATI NA TANZANIA YA LEO

Hapo mwanzo katika kijiji kimoja kulikuwa na vijana wenye nguvu na waliopigania nchi yao kuwa huru. Nchi hiyo ilijulikana kwa jina la Kuabudika, na ilikuwa na miji mikubwa kama sita. hali ya jiji la kwanza ilikuwa sawa na yale mengine. kila kukicha nchi hii maarufu kwa utajili wa kila aina ilibadilika. maisha yalikuwa bora ya jana kuliko leo kikicha. nimesahau kuanza na neno hili "hadithi hadithi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!" hadithi hadithi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!".

yale majoho waliyozoea kuvaa kila siku wale wenye nazo ilifikia mahali bei ilipanda kiasi kwamba kama ni mfanyabiashara ndogondogo ununuapo joo moja fedha za mtajiulikuwa kwaheli. watu walilalamikia juu ya nchi yao. Nchi hii ilikuwa na sifa kubwa yenye viongozi wanaotabili nini hapo baadaye kitatokea na nani aondolewe wapi hapelekwe wapi. kiongozi aliyeamishwa akikataa kufanya hivyo hatima yake ilikuwa ni kifo tu.

Hali ilikuwa vile hadi walipozaliwa watoto mapacha watatu waliofanana kwa kila sifa. walikuwa wakakamavu, wazuri, wenye nia ya kukomboa nchi yao na walitembea wakati wote pamoja. walitumia muda wao wote kusoma kuanzia darasa la kwanza hadi la nane wakiwa na wazazi wao wateule. watoto hawa walipendana sana, walivaa sare vizuri ijapokuwa uwezo wao ulikuwa mmmmmmmmmmm.

Mungu aliwabaliki wale watoto watatu na kufahuru darasa la nane shule ya msingi Majaribu iliyoko wilaya ya Chinyauleje kata ya Kweko. walichaguliwa kuingia kidato cha kwanza na kumaliza kidato cha nne shule ya sekondari Achimwene. mungu aliwabaliki kusomea masomo ya uasikari katika kikosi maalumu. majina ya wale wote yalikuwa "HUZUNI, AMANI NA UTULIVU". baadaye walifanikiwa kwenda kikosi kingine cha masomo ya juu ya uasikari na kuwa makomando wa jeshi.

Hawakulidhika na mishahara waliyopewa kwani walikuwa na ndoto ya kuikomboa nchi yako. Vijana hawa waliamua kuacha kazi na kuendelea na masomo ya chuo kikuu. walisoma chuo kikuu cha Mwanaharakati kilichopo nchi nyingine ya Ahadi. walisoma masomo ya "BA-political science and International Relatioship".

baada ya kutunukiwa Shahada zao walirudi Nyumbani Nchi ya "Kuabudika". siku ile ilikuwa siku ya ajabu kubwa sana. vijana walifuatwa na ndege ya Wanamapinduzi. safari ilianza saa sita mchana. safari ile ilikuwa ni ya siku mbili. waliingia nchini mwao mnamo saa 8.00 mchana. nchi ilianza kutikisika ghafla kabla ndege kutua uwanja maarufu wa St. Ambuje. Mchana kukawa giza nene kama manane ya usiku. nchi ilikuwa nyeusi ikiashiria kuingia kwa wakombozi watatu kutoka Mwanaharakati university.

Ndege ilitua chini, ghafla mchana ulilejea. Kiongozi wa nchi lle maarufu kwa jina la NJETE JA KWEKULA", ALIAGIZA VIJANA WALE WATATU WAUWAWE HARAKA IWEZEKANAVYO KWANI MTABRI WAKE MAARUFU ALITABIRI KUWA VIJANA WALE WA WATATU MMOJA KATI YAO ATAKUWA MTAWALA WA NCHI LE.

ikumbukwe kuwa yule raisi alijiweka madarakani ni kiongozi wa maisha. hakukuwa na uchaguzi wa rais katika nchi ile, yeye aliteua wabunge na viongozi wote wa serikali. yeye ndiye Hakimu na jaji mkuu wa nchi ile. na wazizi wa wae watoto waliuawa na rais wakati watoto hawa wakiwa wachanga sana baada ya rais wa nchi hiyo kuwatuhumu kwa kutaka kufanya mapinduzi.

Wakiwa uwanja wa ndege wale vijana watatu waliwekwa chini ya ulinzi na kikosi maalumu cha makomandoo. ilikuwa patashika vijana wale kukamatwa. vurugu kali ilitokea. na wakati huo huo watu walikuwa wamejaa barabara zote kuzunguka kiwanja maarufu cha ndege. barabara zote zilijaa watu kwa kuwa waliona wanamapinduzi walikuwa wanaingia siku ile. vijana wale walitakiwa kuzungumza na wananchi ili kuzungumzia nini hatima ya nchi yao ambayo uchumi ulishuka kiasi kwamba thamani ya fedha ilishuka hata mkate ulikuwa haushikiki kwa bei mbaya.

wote watatu walikamatwa palepale uwanja wa ndege na kupandishwa ndege maalumu ya jeshi na ndege kupaa tena kuelekea uwanja wa dhambi tayari kwa kunyongwa kama hukumu inavyonesha.

wakati ule vyombo vya habari vilikata matangazo ghafla. wananchi walishangaa sana kuona mgeni wao anapandishwa ndege ya kijheshi na kupaa juu. ghafla mabomu ya machozi yalianza kuvuma huku na kule. watu waliuwa sana. yale yalikuwa mauaji makubwa kuliko yote Tangu nchi ile Iumbwe na Mwenyezi Mungu.

watu waliuwawa makanisani, misikitini, mitaani na maeneo yenye mkusanyiko. hali ilikuwa mbaya tena mbaya sana. watu milioni moja waliuwawa. hapo ndipo sheria mbaya zaidi zilivyoongezeka. katiba ya nchi ilibadilishwa na kunyima uhuru wa vyombo vya habari, maandamano pamoja na mikusanyiko.

siku ile ya mauaji umji ulijaa maiti kiasi kwamba watu walisema leo ndio mwisho wa dunia. Miezi ishirini na nne ilipita, hatima ya nchi haijulikani. wannchi hawajui wale wakombozi wao wamepelekwa wapi. na mtu hana haki ya kuongea juu ya mstakabali wa nchi yao. watu waliamini mungu ndiye aliyesababisha hali hiyo ya nchi. nchi ilikuwa maskini ya mwisho katika dunia ile. watu waliishi bora jana kuliko leo na walikuwa wanasubiri kufa tu maana hakukuwa na namna ya kuwezakuendesha nchi yao.

vijana wale baada ya ya safari ya siku mbili wafikishwa msitu mnene wa "CHIKANJE". msitu ule watu huwa ni chakula cha wanyama. wale askari waliopewa kazi ya kuwanyonga wale vijana watatu, walianza kuwaambia kuwa "nyinyi mlikuwa ni makomandoo wa jeshi, mliacha kazi ya uasikali kwenda masomoni ili kuikomboa nchi yetu. na rais wa nchi hii ametoa amri ya kuuawa kwenu. mnatakiwa muuawe mara moja................................................................................................................. ni amri.

mungu si athumani. mungu amtupi mja wake. wale asikari wanyongaji walikaa kikao cha ghafla. loo!!!!!!!!!!!!. askari mmoja alisema "haiwezekani watu hawa wauawe". mmmmmmmmmm! la hasha!!!!! penye nia pana njia. askari walitafakari na kufikia hatima ya wale vijana watatu. askari wale waliamua kuwaachia huru wale vijana watatu kwa masharti maalumu.

Walikaa kikao cha ghafla na wale watuumiwa watatu. waliwafungua pingu na kuanza kupanga mikakati ya kuipindua nchi. waliweka kila njia na mipangoyote ilikaa vizuri. walipanga wale watakuwa na ulinzi wa jeshi la nchi hiyo. katika mikakati yao ilikuwa ni kumteka kiongozi wa jeshi wa nchi ile na kisha kumalizia kwa rahisi. haraka haraka haina baraka, mmoja wa askari kwa cheo cha Copro Antinion Mwangatu-mbujiko. kazi ilianza mara moja.

kama mungu alipanga hivi. wananchi wa nchi ile waliamka asubuhi bila ya kuamshwa na kuanza kuandamana bila ya kiongozi. kila kijiji, katani, wilaya ,miji na majiji yaliandamana. watu walikuwa wachungu kama pilipili kichaa. Habari ndiyo hiyo kila kona ya jiji. Wananchi walibeba mabango yaliyoandikwa "MAPINDUZI NI LAZIMA, RAIS HATUKUTAKI, LAZIMA UONDOKE, PIGA UA GALAGAZA NCHI HII SI YAKO, RAIS ONDOKA TUPATE AJIRA NA  mengine mengi". kumbe hali ile ilitengenezwa na jeshi la nchi ile na wale vijana watatu wa chuo kikuu.

Askari wote wa nchi waliwatetea wananchi, hakuna aliyeuawa na askari kama ilivyokuwa mwanzo, katiba haikufuatwa kwa askari kuruhusu wananchi waandamane, na kuwapa mabango. kipindi wananchi wakiandamana jeshi la nchi hiyo ilimteka kamanda wa jeshi la nchi hiyo Meja General MWE ULI.

Rais alishangaa ghafla kuona wananchi wanakaribia kasili wakiwa na mabango ya ya maandamano pamoja na silaha kali wakisindikizwa na jeshi la nchi hiyo huku ndege za jeshi za kiita zisizo na rubani na zenye rubani zikiwa na siraha nzito nzito ikiwemo mabomu mazito mazito.

wananchi wa nchi ile walifanikiwa kuiteka ikuru na kumchoma moto Rais wa nchi ile. habari yake iliishia pale. mara ya mwisho yule rais kabla ya kifo chake alisema "KWELI NGUVU YA UMMA..................................................................................................................................................................."

LEO HII NAUKUMIWA BILA KUTAKA KISA UONGOZI WANGU ULIKUWA MBAYA" MUNGU NISAIDIE NIFIKA PAHALA PEMA PEPONI" Wananchi walisema "ameeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee" wengine walisema Amina". 

POWERED BY CHIWAMBO AUSI R, TEKU UNIVERSITY, 2012