Saturday, May 25, 2013

HISTORIA YA UMOJA WA AFRIKA



Umoja wa Afrika (UA) (kiingereza: African Union (AU); kifaransa: Union africaine (UA); Kihispania: Unión Africana (UA) ; Kireno: União Africana (UA) ) ni muungano wa nchi 54 za Afrika ulioanzishwa Julai 2002. Umoja huu unaendeleza kazi za Umoja wa Muungano wa Afrika (kwa kiingereza: Organisation of African Union - OAU). 

Nia ya umoja huu ni kujenga muundo na mfumo wa kisiasa, kiuchumi, na kijamii ili kufikia wakati ambapo bara la Afrika litakuwa na bunge moja, benki moja, jeshi moja, rais mmoja, sarafu moja, n.k. Dhumuni kubwa la umoja huu ni kuungannisha nguvu za mataifa ya Afrika ili kuweza kutatua matatizo yanayokabili bara hili kama vile vita, njaa, ukimwi, n.k. Nchi zote za Afrika ndizo wanachama isipokuwa Moroko. AU ilianzishwa 1963 ikijulikana kama OAU hadi sasa ni miaka 50 tangu kuundwa na hivi leo viongozi mbalimbali wa Africa wamesherehekea sikukuu ya miaka 50 tangu kuzaliwa. Swali ni kwamba je wamefanikiwa kufikia malengo ya AU?

Nchi wanachama
Umoja wa Afrika ina nchi wanachama 53. Ndizo nchi karibu zote za bara la Afrika isipokuwa Moroko iliyoondoka mwaka 1985 kwa sababu ya UA ilitambua Sahara ya Magharibi kuwa nchi ya kujitegema wakati Moroko inadai ya kwamba ni eneo la majimbo yake ya kusini.

Mkutano wa kwanza wa Bunge la Umoja wa Afrika ulifanyika mwaka 2004 huko Afrika Kusini.
Mikutano mikuu ya UA

    Durban (Afrika Kusini): 9-11 Jul. 2002.
    Maputo (Msumbiji): 10-11 Jul. 2003.
    Sirte (Libya), mkutano wa dharura: Feb. 2004.
    Addis Ababa (Ethiopia): 6-8 Jul. 2004.
    Abuja (Nigeria): 24-31 Jan. 2005.
    Sirte (Libya): 28 Jun. - 5 Jul. 2005.
    Khartoum (Sudan): 16-24 Jan. 2006.

Viongozi

Mwenyekiti wa UA hivi sasa Denis Sassou-Nguesso na Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya UA ni Alpha Oumar Konaré. Spika wa Bunge la Umoja wa Afrika ni Getrude Mongella.

CHIWAMBO AUSI R,
BA SOCIOLOGY AND SOCIAL WORK,
TEOFILO KISANJI UNIVERSITY.
http://chiwambo.blogspot.com
ausichiwambor@hotmail.com

No comments: