Friday, August 9, 2013

HISTORIA YA MJI WA KILWA PAMOJA NA MAJENGO YA KALE



Mwanzo wa Kilwa umekadiriwa ulikuwa mnamo 800 BK. Kuna kumbukumbu ya kimdomo inayosema: Watu wa kwanza waliojenga Kilwa Kisiwani ndio Watakata, halafu watu wa Jasi wa kabila la Waranga. Badaaye akaja Mrimba na watu wake. Halafu akaja Sultan Ali bin Selimani Mshirazi yaani Mwajemi. Akaja na jahazi zake akaleta bidhaa na watoto wake. Mtoto mmoja aliitwa Fatima binti Sultan Ali. Hatujui majina ya watoto wengine. Walikuja na Musa bin Amrani Albedu. (kutoka BBC: The Story of Africa - The Swahili).





Kuanzia karne ya 11 Kilwa ilikuwa kituo muhimu ya biashara. Kuanzia karne ya 13 na 14 BK Kilwa ikawa muhimu zaidi kuliko Mombasa. Biashara yake ilikuwa dhahabu kutoka Dola la Mwene Mtapa (Zimbabwe), pembe za ndovu, chuma, nazi pamoja na kununua bidhaa kutoka Bara Hindi na Uchina. Sarafu ya dhahabu kutoka Kilwa imepatikana huko Zimbabwe Kuu.





Katika karne ya 14 -kati ya 1330 na 1340 BK- mji ulitembelewa na msafiri Mwarabu Ibn Battuta aliyeacha taarifa ya kwanza ya kimaandishi kuhusu mji. ajengo makubwa yalijengwa ikiwa magofu yao yamesimama hadi leo kama vile msikiti kuu, nyumba ya kifalme ya Husuni Kubwa na mengi mengine.

Kuja kwa Wareno katika Karne ya 16 ilivuruga biashara ya Waswahili. Kilwa ikarudi nyuma. Katika karne za 18. na 19. ikapata upya nguvu ya kiuchumi kutokana na biashara ya watumwa. Mwisho wa biashara hii ulimaliza utajiri wa Kilwa.
 

 Sehemu ya jengo ambalo lilikuwa na ukumbi mkubwa wa kunadi bidhaa zikiwemo watumwa,pembe za ndovu,simbi,mbao na vyombo vya kufinyangwa kutoka bara la Arabu na Ghuba ya uajemi,kisha kuingiza kwenye ngarawa tayari kwa kusafirisha (Maelezo haya ni kwa ajili ya picha ya hapo juu). 

Kilwa Kisiwani ni jina la kijiji kikubwa kwenye Kisiwa cha Kilwa karibu na mji wa Kilwa Masoko katika Mkoa wa Lindi, Tanzania. Ndipo mahali pa mji wa Kilwa ya kihistoria iliyokuwa mji mkubwa kabisa kati ya miji ya Waswahili katika pwani la Afrika ya Mashariki wakati wa karne za 12-15 BK. Kwa hivyo, Kilwa ilikuwa mji mkuu Afrika mashariki kabla ya wazungu hawajafika kwenye bahari kuu la Hindi.

Kwa mujibu wa tariki ya Kilwa ambayo ni miongoni mwa matini ya kizamani sana yanayotoa historia fupi kuhusu sehemu hii ya Tanzania, Kilwa ni mji ulioanzishwa na kusimamishwa na wahamiaji kutoka Shiraz, huko Uajemi kwa siku za leo. Ni dhahiri kwamba matini haya ambayo jina la mtunzi wake limepotea ni aina ya masimulizi ya kusisimua akili ya msomaji kwa kuwa na hadithi ya kibuni.

Kwa hivyo, ingawa yana maudhui ya kuvutia sana kutokana na ushuhudio wake muhimu sana, tariki hizi hazisomeki kama insha ya kisayansi ambayo itakuwa imeandikwa kufuatana na nadharia tete yenye uthabiti. Mintarafu asili ya wahamiaji wa kwanza ambao walifika Kilwa, hatuna uhakika kwamba walikuwa wanatoka Uajemi, kama inavyodaiwa na tariki hii. Hapo tuwe makini sana.

 Kwa mujibu ya tariki hizi, inasemekana kwamba Sultani mmoja aliyeitwa Hassan bin Ali kutoka Shirazi ndiye aliyehama kule kwao wakati wa kuibuka aina ya mgogoro kati ya watu wake. Sultani huyo akaamua kuondoka na watoto wake sita. Kuondoka kwao huko kwenye bandari ya Siraf, walisafiri kwa jahazi saba kuelekea Afrika mashariki. Hapo inaaminika kuwa kila wakipita kwenye bandari ya kanda ya pwani, mmojawapo alivunja safari yake huku akiaamua kuweka misingi ya mji wake.



Ndiyo asili ya miji saba ambayo tunayo mpaka leo kwenye kanda ya pwani ya afrika mashariki : Mandakha, Shaughu, Yanba, Mombasa, Pemba, Kilwa na Hanzuân. Sultani mwenyewe alikuwa wa mwisho katika kusalia katika msafara huu, naye akakaa kisiwa cha Hanzuani ambacho kipo Ungazija. Mikasa hii na tukio hilo limejitokeza katika miaka kuanzia 957 mpaka 985 baada ya K. Inaaminika kwamba Kilwa wakati ule kilikuwa kisiwa kilichomilikiwa na wenyeji waitwao wamuli.

Kwa kuwa walikuwa hawana nguvu nyingi, walikubali kukiuza kisiwa chao kwa kukubali kupewa vipande vya ntandio. Hapo ndipo Ali bin Hussein alipochukua kisiwa hiki kwa ajili ya kukaa ikiwa ni pamoja na kujenga majumba ya kujitetea dhidi ya watu wa bara na miji mingine ya pwani.

 Kati ya mwaka 957 hadi 1131, Kilwa uliwahi kupambana na mji jirani uliokuwa unaitwa, kwa enzi zile, Shagh. Ghasia zile zikakolea, zikawa zikageukia zikawa vita kwa ajili ya kutawala himaya kubwa. Kilwa ukawa na sifa za fahari katika pande zote za Afrika mashariki kutokana na nguvu zake na mali yake ambayo ilikuwa inatoka bara la Afrika, pahala panapoitwa Sofala. Dhahabu ya Sofala, ambayo ilikuwa ni baadhi ya madini iliyopatikana kwa wingi wakati ule, ilikwenda kuchukuliwa na kuletwa Kilwa kwa njia ya kutembea kwa miguu. Misafara hii ilikuwa changamoto kubwa sana katika kutajirisha himaya ya Kilwa.




Hapo si kiwanja ila ni ukumbi amabo mnada ulikuwa ukifanyika,au sherehe zao watawala hao wa kiarabu walikuwa wakifanyia humo,kwa mbele kuna maji ni bahari ambapo kuna ngazi za kuteremshia bidhaa kuingiza kwenye ngarawa zao.fika ukajionee ni utalii nafuu zana wa kuona kisiwa cha kihistoria Tanzania. (Maelezo haya ni picha ya juu).
Hapo yupo mwandishi mwingine katika lugha ya kiarabu, Al-Mutahar bin Tahir al Makdisi, ambaye vile vile anatoa ushahidi mzuri wa kwamba nchi ya zenj – ambayo ni sehemu hii ya kanda ya pwani kwa enzi hizo – ilichangia sana katika usafirishaji wa dhahabu kutoka Kilwa kwenda Uarabuni kuanzia karne hii ya 10.

Kwa kifupi, wataalamu wa historia wamekubali kusema kwamba kilele cha Kilwa katika kujifaharisha kilianza karne 12 ikadumu hadi karne 15. Kilwa ikawa muhimu zaidi kuliko Mombasa. Biashara yake ilikuwa dhahabu kutoka dola la Mwene Mtapa (Zimbabwe), pembe za ndovu, chuma, nazi pamoja na kununua bidhaa kutoka bara Hindi na Uchina. Sarafu ya dhahabu kutoka Kilwa imepatikana huko Zimbabwe Kuu.

Baharia maarufu ambaye pia alikuwa ni mwana historia hodari sana, Ibn Battuta, anathibitisha vilevile kwamba dhahabu ilikuwa inapatikana pia katika eneo lililoitwa Yufi, nchini mwa Limi (nchi ya kiajabu ambayo wataalamu wengine wanakisia ni pengine Nigeria). Zama zile zilikuwa za kudhabiti utawala wa Kilwa ambao ulipanua mpaka Mafia, Zanzibar na Pemba. Sultani Suleiman bin al-Hassan (1170-1189) aliwahi kukarabati majengo makubwa ya Kilwa kisiwani. Anajulikana sana kwa ujenzi aliouanzisha chini ya utawala wake ambao unaitwa Husuni mdogo. 

Enzi hii bado ilikuwepo chini ya nasaba (dynastie) ya Shirazi mpaka mwaka 1277, ambapo ni kipindi cha awamu nyingine iliyojitokezea katika nasaba ya Mahdaliya ambayo ilitoka Hadramau, Yemen. Karne 14 na mwanzoni mwa karne 15 zilikuwa nyenzi za fahari kubwa sana kwa sababu ya kufaidi na kujiimarisha kipindi kile cha nyuma ambacho Sultani Al Hassan bin Suleiman II (1331-1332) alipopata nafasi ya kuongeza nafasi ya kuswalisha swalat al ijumaa ikiwa ni pamoja na kujenga kasri inayojulikana kwa jina la Husuni Kubwa. 

                                                       Hii Ndiyo Ramani ya Kilwa
 Hicho ni kiberenge kilitumiwa na mmoja wa mwanaakolojia ambaye akikuwa akichimba ili aone masalia ya vyombo vilivyo kuwa zikitumika wakati huo na washirazi kisiwani hao wakati huo.aliyeshika kiberenge ni Bw.samweli mtembeza wattalii.

No comments: