Tuesday, November 12, 2013

CHADEMA: HATUHUSIKI MADAI YA ZITTO



Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema Ofisi ya Katibu Mkuu wa chama hicho imepokea barua iliyoandikwa na Naibu Katibu Mkuu, Bw. Zitto Kabwe.

Barua hiyo, inamtaka Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt. Wilbrod Slaa athibitishe madai ya ripoti inayosema“Taarifa ya Siri ya CHADEMA”iliyosambazwa katika mitandao mba limbali ya kijamii.

Taarifa hiyo inadai kuchunguza mwenendo wa Bw.Kabwe tangu mwaka 2008-2010 na kubaini amepokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuivuruga CHADEMA.
Akizungumza na Majira jana, Ofisa Habari wa CHADEMA,Tumaini Makene,alise ma barua aliyoiandika Bw. Kabwe itafanyiwa kazi kwa mu jibu wa taratibu, kanuni za katiba ya chama.

“Chama chetu kinaongozwa na vikao hivyo barua yake itafanyiwa kazi...CHADEMA h aiendeshwi na taarifa za magazetin i au mitandaoni,”alisema Bw. Makene.
Aliongeza kuwa,si mara ya kwanza makundi yasiyojulikana kusambaza taar ifa za kutaka kumchafua Bw. Kabwe k upitia mitandao hiyo ambapo Ofisi ya Habari,ilishughulikia suala hil o na kuhakikisha taarifa hizo zinaondolewa.
“Hivi sasa ni mara ya pili, Bw. Kabwe anali fahamu hilo hivyo CHADEMA hakihusiki, lakini kitashughulikia suala hili kupitia vikao ili kupata majibu sahihi,” alisisitiza Bw.Makene.

Katika taarifa yake aliyoitoa juzi kwa vyombo vya habari, Bw.Kabwe alisema taar ifa hizo zimesambazwa katika mitandao ya kijamii hiv yo alimtaka Dkt.Slaa, athibitishe kinachoitwa“Ta arifa ya Siri ya CHADEMA”,kama ni taa rifa ya chama au kiikanushe ili kumpa fursa ya kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa taarifa hiyo.
Hata hivyo, Bw. Kabwe ambaye pia ni Mbunge w a Kigoma Kaskazini,aliziita taarifa hizo za kutunga zilizojaa uongo wa kiwango cha kutisha hali ambayo imemfedhehesha, kumsikitisha na kumkasirisha.

Alisema taarifa hizo ziliibuliwa katika kipindi am bacho alikuwa safarini kutetea haki za Watanza nia na Afrika ambao utajiri wao wa rasilimal i unafaidiwa na watu wachache waliohifadhi fedha katika akaunti nje ya nchi.
Chanzo: Majira

No comments: