Tuesday, November 5, 2013

Mwanafunzi ajitia kitanzi kuepa kufeli



Dar es Salaam na Mikoani.Mtihani wa kidato cha nne ulioanza jana nchini, umeingia dosari baada Omary Mkumbo (25) Mkazi wa Mwangata C, Manispaa ya Iringa, kufariki dunia kwa kujinyonga akihofia kufeli mtihani.
Mkumbo alitarajia kuanza mtihani jana kwenye Kituo cha The dream Centre kilichopo Kata ya Gangilonga, mkoani Iringa.

Hata hivyo, alikutwa amejinyonga huku akiacha ujumbe chumbani kwake usiku wa kuamkia jana unaosomeka: “Buriani, nimechoka kufeli mtihani”.
Shangazi wa marehemu, Betha Nzogu (60) alisema Mkumbo alitarajia kuanza mtihani jana ikiwa mara ya tatu tangu alipohitimu kidato cha nne mwaka juzi na kufeli, kisha tukio kama hilo kujirudia mwaka jana.

Alisema kabla ya kuchukua hatua hiyo, Mkumbo alimsaidia kuchinja kuku ambazo huziuza na kwamba, baada ya kumaliza kazi hiyo alirudi nyumbani kwake na kuanza kazi ya kufua nguo.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mwangata C, Saleh Mgimwa alisema alipata taarifa za kujinyonga kwa kijana huyo saa 3:30 usiku.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhan Mungi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na chanzo ni hofu ya kufeli mtihani.
Wakati hayo yakitokea, Dar es Salaam mwanafunzi Asmah Furahisha wa Sekondari ya Kenton iliyoko Sinza, alishindwa kuungana na wenzake baada ya kuzimia dakika chache baada ya kuitwa kuanza mtihani wa jiografia.

No comments: