Friday, March 21, 2014

Waziri Nyalandu atoa mpya

Asema mwanamke atakayevaa hereni za meno ya tembo kukamatwa
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, amesema kuanzia sasa mwanamke yeyote atakayekutwaa amevalia urembo uliotengenezwa kwa nakshi na malighafi ya meno ya tembo atakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Nyalandu aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, mara baada ya  kusaini makubaliano na Taasisi ya Kimataifa ya Uhifadhi kutoka Marekani (ICCF), kwa ajili ya kuimarisha ulinzi pamoja na kuweka ushirikiano katika sekta ya wanyama hasa kuzuia ujangili unaoendelea kwa sasa  nchini.

Waziri Nyalandu alisisitiza kuwa mtu yeyote atakayekutwa na mapambo yanayotokana na nyara hizo hata akiwa kigogo amevalia hereni au shanga, atakamatwa na hatua za kisheria dhidi yake zitachukuliwa ikiwa ni sehemu ya harakati za kutokomeza ujangili nchini.

Chanzo: Tanzania Daima

No comments: