Sunday, March 30, 2014

Wamisri wanaomtusi El-Sisi waonywa

Wizara ya mambo ya ndani ya nchi ya Misri imesema kuwa inachunguza maneno yanayoandikwa kwenye mitandao ya kijamii yakiwa na kitambulisho, yaani "hashtag", yanayomtusi waziri wa ulinzi aliyestaafu ili kugombea urais, Field Marshall Abd-el-Fattah el-Sisi.

Heshtegi hiyo ambayo tafsiri yake ni "mpigie kura kuwadi", imesambazwa kwenye Twitter zaidi ya mara 100-milioni na imependwa na watu zaidi ya 40,000 kwenye Facebook.
Inaarifiwa kuwa wizara ya mambo ya ndani ya Misri imesema itawakamata watu wanaoitumia sana heshtegi hiyo.

Maneno hayo piya yamekuwa yakichorwa kwenye kuta za mjini Cairo chini ya mabiramu ya picha za Bwana Sisi.
Field Marshall E-Sisi aliipindua serikali iliyochaguliwa kwa njia za kidemokrasi ya Mohamed Morsi wa Muslim Brotherhood mwezi Julai mwaka jana.

Chanzo: BBC Swahili

No comments: