Tuesday, March 25, 2014

64,000 huugua TB nchini

ZAIDI ya watu 64,000 nchini huugua Kifua Kikuu (TB) kila mwaka sawa na wastani wa wagonjwa 176 kwa siku.

Hayo yalibainishwa jijini Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Taasisi ya Mapambano dhidi ya Kifua Kikuu na Ukimwi Temeke, Joseph Mapunda, katika maadhimisho ya Siku ya Kifua Kikuu Duniani
Alisema takwimu hizo zimepatikana kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia mpango wa taifa wa kudhibiti kifua kikuu na ukoma.

Alisema idadi kubwa ya watu wanaoambukizwa ugonjwa huo ni watu wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi (VVU), walio katika msongamano na wazee wenye zaidi ya miaka 60.

Alitaja makundi mengine ambayo wapo katika hatari ya kuambukizwa ugonjwa huo ni watoto chini ya miaka mitano, watu wenye lishe duni na wenye magonjwa ya muda mrefu kama kisukari na saratani.

“Kuna idadi kubwa ya wagonjwa wanaopatikana vijijini lakini kutokana na ukosefu wa fedha na serikali kutotoa kipaumbele katika hili, ugonjwa huu umekuwa chanzo cha kupoteza nguvu kazi ya taifa kila kukicha” alisema.

Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Hewa katika Hospitali ya Aga Khan, Dk. Naeem Sultan, alisema kama watu wakiwa na utaratibu wa kupima afya zao mara kwa mara kutokomea magonjwa ya hewa ni suala linalowezekana.


No comments: