Sunday, March 30, 2014

Wanane wauawa Jamhuri ya Afrika ya Kati

Vikosi vya Umoja wa Afrika nchini Jamhuri ya afrika ya kati vinasema kuwa watu wanane wameuawa na vikosi vya Chad katika mji mkuu wa Bangi.
Vyombo vya habari hatahivyo vimeiweka idadi hiyo kuwa juu zaidi.
Vikosi hivyo ambavyo vilikuwa vimewasili mjini humo ili kuwatorosha raia wa Chad wanaoishi nchini humo vinadaiwa kuwafyatulia risasi wakaazi wanaoishi katika maeneo ya wakristo ya mji wa Bangi.

Chad imeshtumiwa kwa kuwaunga mkono waasi wa kiislamu wa seleka ambao mwaka uliopita waliipindua serikali.
Taifa hilo la Jamhuri ya afrika ya kati limekumbwa na ghasia za kidini tangu kupinduliwa kwa rais Franswa Bozize.

Chanzo: BBC Swahili

No comments: