Saturday, October 12, 2013

KIBAYA WILAYANI KITETO HULALA CHINI



Wanafunzi 32 walala chini kwa miaka mitano shuleni
Na. Mohamed Hamad KITETO

JUMLA ya wanafunzi wa kiume 32 wa shule ya msingi na ufundi Kibaya iliyoanzishwa mwaka 1950 Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, wanalazimika kulala chini kwa zaidi ya miaka mitano kwa kukosa vitanda.

Akisoma risala kwa mgeni rasmi leo (jana) kwenye mahafali ya 58 toka kuanzishwa shule hiyo mmoja wa wahitimu hao alitaja changamoto zinazo wakabili kuwa ni kukosemaka kwa vitanda vya wavulana bweni

Zingine ni upungufu wa viti 39 vilivyopo 11, na meza 37 za waalimu zilizopo 13, vyumba vya madarasa 5 vilivyopo 8, nyumba za walimu 13 zilizopo 6 pamoja na matundu 23 ya vyoo kati ya 6 yaliyopo.

Kwa mujibu wa risala iliyosomwa na mmoja wa wahitimu hao imeeleza kuwa shule hiyo ni ya kutwa na bweni, ina jumla ya wanafunzi 561 kati ya hao 304 ni wavulana na wasichana 257

"Mheshimiwa mgeni rasmi kwa heshima kubwa na taadhima mbali na matatizo haya tatizo lingine ni kukosekana kwa uzio hapa shuleni hivyo watu wanaingia shule kwa muda watakao"

Kwa mujibu wa mwalimu mkuu wa shule hiyo Bi.Msangi alieleza MTANZANIA kuwa shule hiyo kwa sasa inakusudiwa kufungwa kwa kukosa choo chenye hadhi hivyo kuhofiwa wanafunzi kudumbukia

Kwa upande wake Simon Parseko (mwanafunzi) aliwaomba wadau wa elimu wilayani na nje ya Wilaya kuwasaidia vitanda, magodoro na shuka kwani wamechoka kulala chini kwa zaidi ya miaka mitano

"Mwalimu alituambia tuwaleze wazazi watununulie vitanda ili tuje navyo hapa shuleni lakini ilishindikana kutokana na kutojua aina ya kitanda kinachohitajika hivyo kutulazimu kuendelea kulala chini"

Naye mgeni rasmi Bakari Mahanyu ambaye pia ni mmoja wa maafisa wa Elimu Wilayani hapo alitupia mpira Serkali ya Kijiji kuwa ndio wenye jukumu la kufanya ukarabati shuleni unapohitajika

Alisema Serikali imekwisha sogeza huduma karibu na wananchi hivyo wenye jukumu la kuendeleza shule ni pamoja na wadau wa Elimu, wazazi pamoja na Serikali ya Kijiji.

Chanzo: Mjengwablog

No comments: