Monday, October 28, 2013

RUSHWA CCM : SUMAYE AZIDI KUTEMA CHECHE



Waziri Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye, ameunga mkono kauli ya Rais Jakaya Kikwete, kuhusu kukithiri kwa rushwa ndani Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwa ndiyo moja ya sababu ya wananchi kukasirika na kukichukia chama.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Sumaye, alisema yeye alianza muda mrefu kuzungumzia rushwa, hivyo anashukuru Rais kuzungumzia vitendo hivyo.
"Namuunga mkono Rais, tupambane na rushwa kwenye uchaguzi na mahali popote pale... Rais amefanya vizuri sana," alisema Sumaye na kuongeza;

"Wapo wanaosema Rais anazungumza tu, kiongozi lazima azungumze kwanza na baadaye matendo yafuate... waliopo chini yake wataanza kuchukua hatua (kuwajibika) na watakaobaki yeye (Rais) atawachukulia hatua wenye matatizo."
Alisema mkuu wa nchi na Chama akizungumzia jambo baya ni lazima aungwe mkono. "Haiwezekani ni mshangae , namuunga mkono kwani ni dhahiri kabisa tusipomuunga mkono wananchi watatukataa," alisisitiza Sumaye.

Alipoulizwa kama kuna uwezekano wa CCM kupoteza majimbo mengi katika uchaguzi ujao, Sumaye alisema hilo lipo dhahiri.
"Wananchi wengi hawapendi rushwa hata kidogo, kwani hawanufaiki nayo, tukiendekeza rushwa wananchi watakiadhibu chama chetu." alifafanua. Alisema yeye anapiga rushwa ndani ya CCM, ndani ya chama chochote kile ndani ya Serikali.

Alipoulizwa sababu za vyama vya upinzani kuzidi kukua kwa kasi, Sumaye alisema; "Tukiweka viongozi ambao hawamudu nafasi na hasa kama wamezipata kwa rushwa watu wanakasirika, wakikuchukia wanakunyima kura."
Alitaja sababu nyingine kuwa ni viongozi wa CCM wa mikoa na kwingineko hawaendi kwa wananchi matokeo yake wanapoteza
mvuto wa chama. Alitaja sababu nyingine kuwa watu wamezidi kuelimika tofauti na ilivyokuwa zamani.

"Zamani mpinzani alionekana kama mhalifu, lakini sasa anaonekana kama yupo ndani ya chama tawala, jambo ambalo ni zuri," alisema.
Alisema kama alivyobainisha Rais Kikwete, hivi sasa vinara wa rushwa ndio wanaonekana watu wa maana na kupokewa kwa nderemo kila wanapopita ndani ya jamii.

Alisema kama wana CCM watapuuza kauli hiyo ya Rais Kikwete na kuwaruhusu watoa rushwa kushika dola, chama hicho kitakuwa kimejichimbia kaburi refu lililomiminwa zege.
Sumaye alisema kauli ya Rais Kikwete ina mantiki kubwa kwa chama hicho na taifa kwa ujumla na kama itafanyiwa mzaha CCM itaangamia.

Sumaye alisema hivi karibuni amepanga kuitisha mkutano wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine, atatoa tamko rasmi la kuunga mkono kauli ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete kupambana na vitendo viovu vya rushwa vinavyofanywa na baadhi ya watu wenye malengo ya kugombea urais, ubunge na udiwani katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015.

Hivi karibuni Rais Kikwete, alielezea kusikitishwa na kukithiri kwa vitendo vya rushwa ndani ya chama hicho na kuonya kuwa hali hiyo ikiendelea itaathiri Cham

No comments: