Sunday, April 6, 2014

MCT yataja jopo la wajuzi wa habari

BARAZA la Habari Tanzania (MCT) limetangaza majina saba ya wajumbe wapya wa jopo la wajuzi wa uhuru wa habari wa kujiendeleza.

Majina hayo yalitangazwa mjini Dodoma jana na Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga.

Katibu huyo aliwataja walioingia kwenye jopo hilo kuwa ni Profesa Penina Mlama, Jenerali wa Ulimwengu, Profesa Ruth Meena, Alli Ahmed Uki, Bonaventura Rutimwa, Ndimara Tegambwage na Wangethi Mwangi.

“Jopo hili limechaguliwa kutokana na vigezo vya kuleta tija, ujuzi na kuibua masuala mapya ya kuipeleka mbele tasnia  habari,” alisema huku akiongeza kwamba  huteuliwa kila baada ya miaka mitatu.

Mukajanga aliwataja wajumbe waliopita kuwa ni Profesa Issa Shivji, Profesa Robert White, Profesa Palamagamba Kabudi, Profesa Penina, Saida Yahya, Wangethi, Ulimwengu na Dk. Peter Mwesige.

Wakati huohuo, alizungumzia kuhusu  mchakato wa Katiba mpya na kuwataka Watanzania kuondoa hofu kutokana na kelele zinatokea ndani ya Bunge Maalumu la Katiba, kwa kuwa ndiko kutakakosaidia kupatikana kwa katiba bora.


Aliwataka baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo kuacha kuleta masuala ya kisiasa katika Bunge hilo, kwa sababu ni la maridhiano.

No comments: