Tuesday, April 1, 2014

BREAKING NEWZ: Magaidi yafanya Shambulizi, yauwa watu sita Nairobi.

Polisi wa Kenya wakikagua eneo lililoshambuliwa la kanisa huko Mombasa. March 23, 2014.
                                   

VOA NAIROBI
Milipuko mitatu katika mji mkuu wa Kenya wa Nairobi imesababisha vifo vya watu 6 na karibu darzeni mbili kujeruhiwa jumatatu usiku katika mtaa mkubwa wenye wakazi wengi wa asili ya Kisomali wa Eastleigh.

Mkuu wa polisi wa County ya Nairobi Benson Kibue anasema milipuko hiyo ilitokea takriban saa moja na nusu usiku  na kwa karibu wakati mmoja katika migahawa ya Sheraton Café na The New Kwa muzairua Grill.

Kufuatana na mmiliki wa Sheraton Café Bw. Patrick Gakuyu watu walikuwa wanatizama taarifa ya habari ya saa moja kwenye televisheni wakati aliposikia milipuko miwili na umeme kuzimika na kuwa katika kiza. Anasema anadhani ni grunetti mbili zilizorushwa ndani ya mgahawa wake.

Jumapili usiku karibu na mtaa huo mtu anayedhaniwa ni gaidi aliuwawa alipokuwa anatengeneza milipuko yake pamoja na wenzake watatu. Na gruneti moja ilipatikana siku hiyo hiyo ya jumapili katika mji wa pwani wa Lamu ndani ya kanisa moja.

Usalama umeimarishwa katika miji mikuu ya Kenya na hadi hivi sasa haijulikani aliyehusika na mashambulio ya jumatatu.

BBC NAIROBI
Watu sita wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika shambulizi la kigaidi katika eneo la California mtaa wa Eastleigh, mjini Nairobi.
Polisi wamesema kuwa milipuko miwili ilitokea wakati magaidi waliporusha mabomu katika mkahawa mdogo ulio karibu na kituo cha mabasi mtaani humo.
Polisi mtaani Eastleigh 
Walioshuhudia shambulizi walisema kuwa walisikia mlipuko wa tatu katika eneo hilo ingawa polisi hawajathibitisha hilo.
Miongoni mwa waliojeruhiwa walikuwa wanawake ambao walipata majeraha mabaya na kukimbizwa hospitalini kwa matibabu.
Kwa mujibu wa polisi wale waliouawa walikuwa wamekwama ndani ya mkahawa huo baada ya mlango kufungwa na washambulizi waliorusha mabomu hayo ndani ya mkahawa wenyewe.
Waathiriwa walikuwa wameenda kununua chakula cha jioni. Idadi kubwa ya wakimbizi wa Somali wanaishi katika mtaa wa Eastleigh.

Inaarifiwa washambuliaji walitumia maguruneti au mabomu ya kutengezwa nyumbani kufanya mashambulizi hayo.





















No comments: