Sunday, February 10, 2013

BUNGE LA TANZANIA LIMEPOTEZA MWELEKEO KIASI CHA KUFANANISHA NA KIJIWE CHA WAHUNI.


MAKALA YA CHIWAMBO

Kwa wale waliofuatilia Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wiki iliyopita na mwanzoni mwa wiki hii anaweza kuthibitisha kuwa Bunge letu limepoteza mwelekeo na kugeuzwa kuwa kijiwe cha wahuni. Pia unaweza kufananisha na shule za kata ambazo hufanya kazi ya kukuza watoto wanaomaliza darasa la saba.

Wabunge kutoka nje ya kikao cha Bunge ilikuwa kama fasheni ya vyama vya upinzani hasa Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo (CHADEMA) pale walipoona hoja zao hazisikilizwi. Kwa safari hii waliamua kutumia njia zote mbili yaani kutoka nje ya Bunge siku ya Jumatatu na siku ya Jumanne kutumia njia mbadala ambayo wanadhani kuwa ni njia mzuri kuliko zote ni kuzomea zomea bila utaratibu ambapo Muheshimiwa Tundu Lisu, John Mnyika, Na Nasari ndio wanaosemekana kuwa ni chokochoko la zomea zomea kule mjengoni.

Kwa wale niliosoma nao Chuo Kikuu kimoja hasa wale wanaosoma Shahada ya Sosholojia na Maendeleo ya jamii nimewai kuwaeleza kwamba “Hata motto mdogo ukimnyanyasa na kumonea kila ukutanapo, basi ujue kuwa siku moja atakugeukia na kukurudishia matusi au kukurusha mawe kama silaha yake dhidi ya uonevu, 2012”.

Hili ndilo linalotokea ndani ya Bunge letu. Hoja za wapinzani kwa miaka mingi hasa Bunge la Kumi limekuwa hodari kwa kuweka kapuni Hoja z wabunge wa upinzani na matokeo ya haya ni vurugu kubwa zilizotokea wiki hii. Ni hatari sana kuona Bunge linafanywa kama sehemu ya kuendeleza ubabe wa kisiasa na si kujadili hoja zenye maslahi kwa Watanzania.

Katika historia ya Mabunge Duniani ni kwamba vurugu Bungeni ni sehemu ya kawaida kwa baadhi ya nchi na linaonekana ni jambo la kawaida ila kwa upande wan chi yetu ni jambo geni licha ya wabunge wa Tanzania kutaka kuzichapa Mwaka 2011. Wiki hii waliona bora kumzomea Naibu Spika, Job Ndugai.

Kutokana na mahojiano yaliyofanywa na mwandishi wa Gazeti la Raia Mwema na Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji P. Msigwa alisema kwamba “ipo siku watavunja viti vya Bunge……” na mwishowe alimalizia kwa kusema hatua zichukuliwe ili wasifike huko.

Kuna jambo linanishangaza sana hasa kwa Wabunge wetu na jambo hilo ndilo linalofanya Bunge letu lipoteze mwelekeo. Jambo kuu ni lile la Mbunge kupinga uozo wa wizara husika kwa kuongelea zaidi madudu yaliyomo katika Wizara husika na wakati wa kuhitimisha hoja yake anamalizia kwa kuunga mkono hoja iliyopo.

Huu ni undumila kuwili ambao unalifanya Bunge letu kupoteza Mwelekeo. Kuna Rafiki yangu mmoja siku moja aliniambia kwa sasa kuangalia Bunge ni sawa na kusoma gazeti la udaku. Nilimuuliza kwanini? Hakuweza kunipa jibu. Kwa hakika kauli yake ina uhalisia katika Bunge letu.

Watanzania wenzangu, wasomaji wa makala ya Chiwambo, ni maoni yangu kwamba Bunge hili linaloongozwa kivyama zaidi ifike siku liongozwe na mtu asiye mwanachama wa chama chochote hapa nchini ili lilete ufanisi zaidi kuliko tunayoyashuhudia huko Dodoma kila unapofanyika Mkutano wa Bunge.    

No comments: