Saturday, August 3, 2013

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI AZIMIO HUKO TUNDURU WASOMEA CHINI YA MITI NA OFISI YA KIJIJI

 Hili ni Moja ya Darasa linalotumiwa na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Azimio kufundishwa na kujisomea. Jengo la Mbele katika kuta zake ni majengo ya shule yaliyojengwa Miaka ya 1970. Majengo hayo hayatumiki kwa sababu hayana paa na yalikuwa na nyufa kubwa kuweza kuhatarisha maisha ya wanafunzi wa shule hiyo iliyopo Kata ya Mtina Tarafa ya Lukumbule.
 Huu ni mwonekano Mwingine wa jengo hilo na darasa moja la wanafunzi wa darasa la Tatu wanaosomea nje ya majengo ya darasa kwa kuwa shule hiyo ina madarasa manne tu huku idadi ya wanafunzi ni kubwa na kukiwa na madarasa 7





Mbeya ya picha ni Jengo la madarasa mawili yaliyojengwa kwa nguvu za Wananchi kijiji hapo na hadi leo halijakamilika ujenzi wake.
Upande wa kulia ni Vyumba vya madarasa mawili yaliyojengwa na TASAF na nyuma kabisa ya picha ni Tanuli la Matofali yanayogeuka kuwa kichuguu ile hali wananchi waliandaa tofali hizo miaka mitatu iliyopita

Haya ni majengo yaliyohalibika kutokana na kuchakaa kwa kuta zake ambapo shule hiyo ilianzia na majengo haya miaka ya 1970




NA CHIWAMBO AUSI
Hayo ndiyo majengo ya shule ya msingi Azimio yakionyesha madarasa manne tu ya kusomea wanafunzi na vyumba vya nje yaani chini ya miti. Wananchi walijitolea kufyatua tofali ila hadi sasa zinaota kichuguu kwani hada sasa zina miaka Mitatu huku zikiwa zinaharibika. Tofali nyingi zimehariika na kutokana na asili ya udongo wa sehemu hiyo, matofali hudumu kwa muda wa miaka miwili tu kabla halijajengewa.

Ni hatari sana kuona wanafunzi kusomea chini ya miti ambako wanafunzi huzagaa kila mahali na kuleta picha mbaya katika suala zima la Elimu. Ni miaka zaidi ya 50 ya uhuru. Jengo linaloonekana kuwa zuri ni la Tasaf lenye madarasa mawili na ofisi moja tu na jengo lingine ni nguvu za wananchi ambalo lina vyumba viwili tu na ofisi moja.

Serikali ya Wilaya ya tunduru ichunguze suala hili la Elimu shuleni hapo na ichukue hatua haraka iwezekanavyo. Kutokana na muda wa kuwepo Wilayani hapo kuwa mchache nilishindwa kufanya mahojiano na Afisa Elimu wa wilaya hiyo. Taarifa ya mahojiano yangu na viongozi wahusika nitaiweka mwezi September baada ya kufanya mahojiano na viongozi wahusika. 

achiwambo@yahoo.com

No comments: