Wednesday, January 23, 2013

MCHAKATO WA UCHAGUZI 2015 USIWE MBEBWE KIASI CHA KUSHINDWA KUFANYA KAZI ZENYE MASLAHI KWA UMMA.



 MAKALA YA CHIWAMBO
Katika Makala ya Chiwambo leo inazungumzia zaidi juu ya utendaji kazi wa watumishi wa umma, wanasiasa, na namna vyombo vya habari vinavyotumika visivyo ili kutetea maslahi ya wachache. Hili linajitokeza kila uchaguzi hasa kuanzia Mwaka 2005, 2010, na inavyoonekana 2015 nayo ipo vivyo hivyo. Wananchi hugawanywa vipande vipande katika makundi mbalimbali huku makundi hayo yote husimamia maslahi ya kundi husika.

Katika nchi yetu kwa bahati mzuri hatuna Ukabila kama kule Nchini Kenya ambapo nchi hiyo katika kila chaguzi utawala suala la ukabila. Lakini huku kwetu Tanzania makundi ndiyo tatizo kubwa ambayo lengo kuu ni kushika hatamu ya kuongoza nchi. Wakati huu karibu kila chama kinazunguzia zaidi kuhusu uchaguzi 2015. Nani atakuwa Rais ajaye sio kwa chama tawala tu bali hata chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Viongozi wetu inavyoelekea hasa wale wanaohitaji Urais 2015 wameanza kujisahau. Wamesahau wapiga kura wao na kuzungumzia zaidi suala la uchaguzi mwaka 2015. Swali la kujiuliza ni kwamba je wananchi munawatumikia kweli? Panafikia mahali mtu unapata mashaka juu ya utendaji wao wa kazi. Magazeti wameyatawala kwa kuandika zaidi habari zao za uchaguzi 2015 na nani atakuwa mbabe katika uchaguzi huo.

Ukweli ni kwamba wananchi hatupendi kuona nchi inalumbana juu ya nani atakuwa Rais ajaye Mwaka 2015 badala yake muwatendee haki hawa Wananchi waliowafanya muingie hapo Mjengoni. Katika tafsiri ya mwandishi wa habari inasema kwamba ni “The voice of the voiceless” au Watch dog of the Government”. Hii inamaana kwamba mwandishi wa habari ni mtu anayewasemea wananchi ambao hawana pa kusemea.

Wananchi walio wengi Tanzania hasa wale wa vijijini hawana wasemaji licha ya kuwa na wabunge ambao huwakilisha wilaya hizo na wanaonekana kwao uchaguzi hadi uchaguzi. Sasa huyu mwandishi anatakiwa kuwa msemaji na mfichuaji wa maovu na mazuri yote yanayofanywa na Wananchi, kikundi cha watu, pamoja na kuikosoa serikali iliyopo madarakani kwa kuonesha kwamba hapa bwana mkuu hujafanya vizuri na hapa umefanya vizuri.

Lakini kwa sasa waandishi wa habari wetu wamewageuka wananchi. Na wamebadilisha maana halisi ya Mwandishi wa habari ambapo wameifanya kuwa “Journalist is a person who deal with the viceveser of the voice of the voiceless”. Inamaanisha wanajadili zaidi suala la kwamba mwandishi wa habari na kazi yake ni kuweka kinyume cha tafsili halisi ya kuwasemea wale wasio na sauti na badala yake kusimama upande Fulani wa kundi analoliamini yeye ili kutetea maslahi ya mtu binafsi kunyakua kiti cha uraisi 2015.

Hili ni balaa nan i janga kwa taifa la leo na kesho. Matokeo ya vyombo vya habari kuwa wapiga debe kwa viongozi wa aina Fulani ni bomu ambalo litakuja kuwalipukia wenyewe hapo baadaye. Waandishi wenzangu mulio wengi mumekuwa ndumila kuwili na watawaliwa wa fikra zenu. Inaonesha namna gani elimu muliyonaye haisaidii Taifa letu badala yake unafuata matakwa ya wachahce wenye fedha na wanasiasa.

Wewe mtaaluma wa masuala ya uandishi wa Habari, iweje ufundishwe nini cha kuandika na mtu ambaye hata taaluma yenyewe ya uandishi wa habari hana na hajawai kuisoma. Na wengine hata tafsiri ya neon lenyewe Journalism halijui. Sasa inakuwaje kikundi hiki cha watu kitawale sanaa ya uandishi wa habari. Kwa msingi huu mutaendelea kununuliwa siku hadi siku, maisha hadi kiama. 

Kwa mabo kama haya munakaa vikao na kusema hatuna uhuru wa Habari nchi. Kama unakubali kununuliwa na ukanunulika unadhani uhuru utakuwepo kweli? Tumezichoka habari za kusikia hatuna uhuru wa vyombo vya habari nchini huku ninyi wenyewe mkiwa mstari wa mbele kuwasaliti wananchi. Munategemea nini? Fedha za leo zitawatawala ninyi wenyewe hapo kesho. Mara nyingi ninyi munakuwa mstari wa mbele baadaye kusema kiongozi huyu ni mbaya, hafai na kumwangika vichwa vya habari vya kumkejeli baada ya kupata madaraka.

Kama mimi ningekuwa ndiye Rais wan chi hii ningemshinikiza waziri anayehusika na masuala ya vyombo vya habari andaye mswada mpya zaidi wa kuvinyonga vyombo vya habari ili wakose uhuru zaidi. Kwani kiasi cha uhuru uliopo wameshindwa kukitumia. Mambo ya kuzungumzia yapo mengi ten asana kila kona. Hivi swali lenu ni hili, je umewai kutembelea vijijini kule na kuona nyakati za mvua wanaishije? Wanakula nini? Adha gani wanayokutana nayo?

Hivi ni kweli vitu vya kuzungumzia kwenye vyombo vyenu vya habari (Media) vimekwisha kabaisa? Au munataka wananchi waandamane pamoja na kuwalamba mboko ili muandike habari zao na muwatumikie vyema? Hivi munadhani hiyo elimu yenu bila wananchi mungeza kuipa? Utitili wa magazeti sasa unathibitisha usemi wangu kuwa wanaripoti habari mbalimbali ili kulinda maslahi ya watu wachache badala ya umma.

Mutazame maeneo ya Ngorongoro watu wanavyoteseka na Njaa, Tunduru hadi leo korosho hazinunuliwi na wananchi hawajui lini zitanunuliwa huku watu binafsi wakinunua kangomba za korosho kwa bei ya shilingi 500 kwa kilo. Ninyi waandishi muko wapi? Kwanini musiripoti habari kama hizi zinazooneka ni za ulanguzi. Maisha ya wanatunduru msimu huu wa mvua yanakuwa hali tete? Chakula chao kikuu ni ugali wa muhogo wa wa kuloweka kwenye maji na kukausha ambao hauna virutubisho mwilini. Na mvua zinapochanganya watu hushindwa kula na wengine hushindia miogo ya kupika au uji.

Nakumbuka mwalimu wangu Mama Mushi wa somo la NEWS REPORTING Chuo kikuu MT. Augustine Mwanza alinifundisha kwamba Greater The Name Greater The News, And Greater the Event Greater the New”. Ila hili neon lisitumike visivyo ili kuweza kuwanyima na kuwafunga midomo wananchi. Pamefikia mahari mtu unahamua kuaghahilisha kununua Gazeti Fulani kisa linapendelea sana upande Fulani wa chama au kundi la watu wataka Madaraka badala ya kuwazungumzia wananchi na shida zao zinazozidi kuongezeka siku hadi siku na zitazidi kuongezeka siku hadi siku.

Inawezeka waandishi wetu wanafanya haya kwa sababu vyombo vya habari vilivyo vingi nchini vinamilikiwa na wenye fedha na wanasiasa hivyo wanalazimika kuandika au kuripoti kile basi wao anachohitaji. kwa mfano kama mimi ningekuwa namiliki vyombo vya habari basi nikilala nikiamka natoa amri kesho magazeti au media zangu zote munilipoti kwamba nimetoa msaada huu ili nionekana nafanya mema kwa wananchi kumbe moyoni ni danganya toto.

 HivyoViongozi wetu tunawaomba muwatumikie wananchi vilivyo ili kuweza kuleta ufanisi zaidi na kupunguza lindi la umaskini linaloikabili nchi yetu. Masuala ya uchaguzi 2015 yasiwe ndio kikwazo kwa maendeleo ya nchi yetu Tanzania. CCM na CDM na vyama vingine muwatumikie wananchi kwanza na sio kulumbana juu ya uchaguzi 2015 na badala yake mufanye kama mulivoagizwa na wananchi. Je ukifika mwaka 2015 utawaeleza nini hao wananchi waliokuchagua kuwa kiongozi wao? 

Makala hii Imeandikwa na Chiwambo Ausi
TEOFILO KISANJI UNIVERSITY (TEKU)
E-Mail: Ausichiwambor@hotmail.com

No comments: