Friday, April 6, 2012


MWANAHARAKATI NA HADITHI YA LEO
Hapo mwanzo katika kijiji kimoja kulikuwa na vijana wenye nguvu na waliopigania nchi yao kuwa huru. Nchi hiyo ilijulikana kwa jina la Kuabudika, na ilikuwa na miji mikubwa kama sita. hali ya jiji la kwanza ilikuwa sawa na yale mengine. kila kukicha nchi hii maarufu kwa utajili wa kila aina ilibadilika. maisha yalikuwa bora ya jana kuliko leo kikicha. nimesahau kuanza na neno hili "hadithi hadithi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!" hadithi hadithi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!".
yale majoho waliyozoea kuvaa kila siku wale wenye nazo ilifikia mahali bei ilipanda kiasi kwamba kama ni mfanyabiashara ndogondogo ununuapo joo moja fedha za mtajiulikuwa kwaheli. watu walilalamikia juu ya nchi yao. Nchi hii ilikuwa na sifa kubwa yenye viongozi wanaotabili nini hapo baadaye kitatokea na nani aondolewe wapi hapelekwe wapi. kiongozi aliyeamishwa akikataa kufanya hivyo hatima yake ilikuwa ni kifo tu.
Hali ilikuwa vile hadi walipozaliwa watoto mapacha watatu waliofanana kwa kila sifa. walikuwa wakakamavu, wazuri, wenye nia ya kukomboa nchi yao na walitembea wakati wote pamoja. walitumia muda wao wote kusoma kuanzia darasa la kwanza hadi la nane wakiwa na wazazi wao wateule. watoto hawa walipendana sana, walivaa sare vizuri ijapokuwa uwezo wao ulikuwa mmmmmmmmmmm.
Mungu aliwabaliki wale watoto watatu na kufahuru darasa la nane shule ya msingi Majaribu iliyoko wilaya ya Chinyauleje kata ya Kweko. walichaguliwa kuingia kidato cha kwanza na kumaliza kidato cha nne shule ya sekondari Achimwene. mungu aliwabaliki kusomea masomo ya uasikari katika kikosi maalumu. majina ya wale wote yalikuwa "HUZUNI, AMANI NA UTULIVU". baadaye walifanikiwa kwenda kikosi kingine cha masomo ya juu ya uasikari na kuwa makomando wa jeshi.
Hawakulidhika na mishahara waliyopewa kwani walikuwa na ndoto ya kuikomboa nchi yako. Vijana hawa waliamua kuacha kazi na kuendelea na masomo ya chuo kikuu. walisoma chuo kikuu cha Mwanaharakati kilichopo nchi nyingine ya Ahadi. walisoma masomo ya "BA-political science and International Relatioship".
baada ya kutunukiwa Shahada zao walirudi Nyumbani Nchi ya "Kuabudika". siku ile ilikuwa siku ya ajabu kubwa sana. vijana walifuatwa na ndege ya Wanamapinduzi. safari ilianza saa sita mchana. safari ile ilikuwa ni ya siku mbili. waliingia nchini mwao mnamo saa 8.00 mchana. nchi ilianza kutikisika ghafla kabla ndege kutua uwanja maarufu wa St. Ambuje. Mchana kukawa giza nene kama manane ya usiku. nchi ilikuwa nyeusi ikiashiria kuingia kwa wakombozi watatu kutoka Mwanaharakati university.
Ndege ilitua chini, ghafla mchana ulilejea. Kiongozi wa nchi lle maarufu kwa jina la NJETE JA KWEKULA", ALIAGIZA VIJANA WALE WATATU WAUWAWE HARAKA IWEZEKANAVYO KWANI MTABRI WAKE MAARUFU ALITABIRI KUWA VIJANA WALE WA WATATU MMOJA KATI YAO ATAKUWA MTAWALA WA NCHI LE.
ikumbukwe kuwa yule raisi alijiweka madarakani ni kiongozi wa maisha. hakukuwa na uchaguzi wa rais katika nchi ile, yeye aliteua wabunge na viongozi wote wa serikali. yeye ndiye Hakimu na jaji mkuu wa nchi ile. na wazizi wa wae watoto waliuawa na rais wakati watoto hawa wakiwa wachanga sana baada ya rais wa nchi hiyo kuwatuhumu kwa kutaka kufanya mapinduzi.
Wakiwa uwanja wa ndege wale vijana watatu waliwekwa chini ya ulinzi na kikosi maalumu cha makomandoo. ilikuwa patashika vijana wale kukamatwa. vurugu kali ilitokea. na wakati huo huo watu walikuwa wamejaa barabara zote kuzunguka kiwanja maarufu cha ndege. barabara zote zilijaa watu kwa kuwa waliona wanamapinduzi walikuwa wanaingia siku ile. vijana wale walitakiwa kuzungumza na wananchi ili kuzungumzia nini hatima ya nchi yao ambayo uchumi ulishuka kiasi kwamba thamani ya fedha ilishuka hata mkate ulikuwa haushikiki kwa bei mbaya.
wote watatu walikamatwa palepale uwanja wa ndege na kupandishwa ndege maalumu ya jeshi na ndege kupaa tena kuelekea uwanja wa dhambi tayari kwa kunyongwa kama hukumu inavyonesha. 
wakati ule vyombo vya habari vilikata matangazo ghafla. wananchi walishangaa sana kuona mgeni wao anapandishwa ndege ya kijheshi na kupaa juu. ghafla mabomu ya machozi yalianza kuvuma huku na kule. watu waliuwa sana. yale yalikuwa mauaji makubwa kuliko yote Tangu nchi ile Iumbwe na Mwenyezi Mungu.
watu waliuwawa makanisani, misikitini, mitaani na maeneo yenye mkusanyiko. hali ilikuwa mbaya tena mbaya sana. watu milioni moja waliuwawa. hapo ndipo sheria mbaya zaidi zilivyoongezeka. katiba ya nchi ilibadilishwa na kunyima uhuru wa vyombo vya habari, maandamano pamoja na mikusanyiko. 
siku ile ya mauaji umji ulijaa maiti kiasi kwamba watu walisema leo ndio mwisho wa dunia. Miezi ishirini na nne ilipita, hatima ya nchi haijulikani. wannchi hawajui wale wakombozi wao wamepelekwa wapi. na mtu hana haki ya kuongea juu ya mstakabali wa nchi yao. watu waliamini mungu ndiye aliyesababisha hali hiyo ya nchi. nchi ilikuwa maskini ya mwisho katika dunia ile. watu waliishi bora jana kuliko leo na walikuwa wanasubiri kufa tu maana hakukuwa na namna ya kuwezakuendesha nchi yao.
vijana wale baada ya ya safari ya siku mbili wafikishwa msitu mnene wa "CHIKANJE". msitu ule watu huwa ni chakula cha wanyama. wale askari waliopewa kazi ya kuwanyonga wale vijana watatu, walianza kuwaambia kuwa "nyinyi mlikuwa ni makomandoo wa jeshi, mliacha kazi ya uasikali kwenda masomoni ili kuikomboa nchi yetu. na rais wa nchi hii ametoa amri ya kuuawa kwenu. mnatakiwa muuawe mara moja................................................................................................................. ni amri.
mungu si athumani. mungu amtupi mja wake. wale asikari wanyongaji walikaa kikao cha ghafla. loo!!!!!!!!!!!!. askari mmoja alisema "haiwezekani watu hawa wauawe". mmmmmmmmmm! la hasha!!!!! penye nia pana njia. askari walitafakari na kufikia hatima ya wale vijana watatu. askari wale waliamua kuwaachia huru wale vijana watatu kwa masharti maalumu.
Walikaa kikao cha ghafla na wale watuumiwa watatu. waliwafungua pingu na kuanza kupanga mikakati ya kuipindua nchi. waliweka kila njia na mipangoyote ilikaa vizuri. walipanga wale watakuwa na ulinzi wa jeshi la nchi hiyo. katika mikakati yao ilikuwa ni kumteka kiongozi wa jeshi wa nchi ile na kisha kumalizia kwa rahisi. haraka haraka haina baraka, mmoja wa askari kwa cheo cha Copro Antinion Mwangatu-mbujiko. kazi ilianza mara moja.
kama mungu alipanga hivi. wananchi wa nchi ile waliamka asubuhi bila ya kuamshwa na kuanza kuandamana bila ya kiongozi. kila kijiji, katani, wilaya ,miji na majiji yaliandamana. watu walikuwa wachungu kama pilipili kichaa. Habari ndiyo hiyo kila kona ya jiji. Wananchi walibeba mabango yaliyoandikwa "MAPINDUZI NI LAZIMA, RAIS HATUKUTAKI, LAZIMA UONDOKE, PIGA UA GALAGAZA NCHI HII SI YAKO, RAIS ONDOKA TUPATE AJIRA NA  mengine mengi". kumbe hali ile ilitengenezwa na jeshi la nchi ile na wale vijana watatu wa chuo kikuu.
Askari wote wa nchi waliwatetea wananchi, hakuna aliyeuawa na askari kama ilivyokuwa mwanzo, katiba haikufuatwa kwa askari kuruhusu wananchi waandamane, na kuwapa mabango. kipindi wananchi wakiandamana jeshi la nchi hiyo ilimteka kamanda wa jeshi la nchi hiyo Meja General MWE ULI.
Rais alishangaa ghafla kuona wananchi wanakaribia kasili wakiwa na mabango ya ya maandamano pamoja na silaha kali wakisindikizwa na jeshi la nchi hiyo huku ndege za jeshi za kiita zisizo na rubani na zenye rubani zikiwa na siraha nzito nzito ikiwemo mabomu mazito mazito.
wananchi wa nchi ile walifanikiwa kuiteka ikuru na kumchoma moto Rais wa nchi ile. habari yake iliishia pale. mara ya mwisho yule rais kabla ya kifo chake alisema "KWELI NGUVU YA UMMA..................................................................................................................................................................."
LEO HII NAUKUMIWA BILA KUTAKA KISA UONGOZI WANGU ULIKUWA MBAYA" MUNGU NISAIDIE NIFIKA PAHALA PEMA PEPONI" Wananchi walisema "ameeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee" wengine walisema Amina".

No comments: