Friday, April 6, 2012

HOTUBA MBAYA YA BWANA P. W. BOTHA


VITUKO VYA WAKUBWA
HII NDIYO MOJA YA HOTUBA MBAYA ZA P. w. BOTHA
Ø Akiri kuwaua kwa weusi kwa sumu
Ø Mweusi ni malighafi ya mweupe

HABARI KAMILI
Hii ni hotuba ya aliyekuwa rais wa Afrika Kusini, p. w. Botha alipohutubia baraza lake la mawaziri wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi nchini humo. Katika hotuba hiyo iliyochapishwa na gazeti la “SUNDAY TIMES” la nchini humo toleo la Agosti 18, 1985, Botha anapojigamba eti ardhi hiyo ni mali yao na haipaswi kuingiliwa.

Ikumbukwe kuwa katika utawala huo, mtu mweusi aliteswa na kunyimwa haki zake za msingi na alifanywa kuwa kiumbe dhaifu kisichostahili kuishi kwa raha katika nchi hiyo.

P. W. BOTHA KUSHOTO NA NELSON MANDERA KULIA

“Kaka zangu na dada zangu, Pretoria imetengenezwa na watu weupe kwa ajili ya watu weupe na hatuna haja ya kuuthibitisha umma au mtu mweusi kuwa sisi ni watu bora, tumekuwa tukiwaambia  watu weusi jambo hili kwa njia elfu.

Africa kusini ya leo haikutengenezwa katika mawazo ya kawaida, tumeitengeneza kwa kutumia akili nyingi, jasho na damu. Mnaposema kuwa tunawabagua weusi sielewi.

Hivi ni Afrikaners ndio waliojaribu kusitisha kizazi cha Aborigines wa Australia? Je ni Africaners waliotenga na kuwanyanyasa watu weusi Marekani kasikazini kwa kuwaita niggaz?

Je, ni Africaners waliowatenga na kuwanyanyasa watu weusi huko England kwa kuwatungia sheria ya kuwakandamiza? Canada, Ufarasa , Russia, na Japan nao wana njia zao za kibaguzi. Hivi kwanini hasa kuna kelele nyingi dhidi yetu? Huu ni uendawazimu! Kwanini wanatukaba koo kiasi hiki? Hawatundendei haki hata kidogo.

Nataka kuwaeleza kuwa hakuna kibaya tunachokitenda hapa ambacho hao wanaojihita wako katika dunia ya ustaarabu wameacha kufanya. Sisi ni watu wema tusio na hatia na ambao tumeweka wazi mfumo wa maisha ya tunayotaka tuishi kama watu weupe.

Sisi sio wanafiki kama wazungu wenzetu wafanyavyo kwamba wanapenda watu weusi.

Ukweli kuwa weusi wanaofanana na binadamu na kutenda mambo kama binadamu hayawahalalishi kuwa wao ni watu wenye akili timamu au binadamu aliyetimia. Kanunguyeye si nungunungu na mijusi hawawezi kuwa mamba kwa sababu eti wanafanana.

Kama mungu alitaka tufannane na weusi angetufanya wote tuwe na rangi moja na fikra sawa. Lakini alituumba tofauti, weupe, weusi, wanjano, watawala na watawaliwa. Katika upeo sisi ni bora kuliko weusi na hilo halina ubishi kwani limejidhihilisha kwa miaka mingi iliyopita.

Naamini kuwa Africaner ni mtu safi, mwenye hofu na mungu. Ni mtu mbaye ameonyesha kwa vitendo njia sahihi ya utu. Hata hivyo inafurahisha kuona Ulaya, America, Canada, Australia na wengine wengi wako nyuma yetu achilia mbali maeneo yao.

Kuhusu uhusiano wa kidemokrasia, sote tunafahamu lugha inayotakiwa kutumika. Na kwa ushaidi ulio wazi hivi kuna mtu hapa asiyejua kuwa nchi nyingi za Ulaya zina tamani kuwekeza Afika kusini.

Nani anayenunua dhahabu yetu, nani anayenunua almasi yetu? Nani anafanya bihashara nasi? Nani anatusaidia katika kuendesha siraha za nyukilia? Ukweli ni kwamba sisi ni watu wao na wao ni watu wetu. Hii ni siri kubwa. Nguvu ya uchumi wetu inajengwa kwa kiasi kikubwa na America, Uingereza, na Ujerumani. Ni jambo kubwa sana hili na kwa maana hiyo, mweusi ni malighafi kwa mweupe.

Hivyo basi, kaka na dada zangu hebu tuungane kumpiga vita huyu mweusi. Napiga mbiu kwa Africaners wote kujitokeza kwa hali na mali kupigana vita hii. Kwa hakika mungu hawezi kuwatupa watu wake ambao ni sisi. Hadi sasa imeonekana kwa vitendo kuwa weusi hawawezi kujitawala. Wape bunduki kama hawataanza kuuana.

Hawana lolote jema isipokuwa mashujaa wa kupiga kelele, kucheza ngoma, kuoa wanawake wengi na kupenda sana ngono. Hebu sasa tukubali kuwa mtu mweusi ni alama ya umskini, udumavu wa akili, uvivu na aliyekosa ushindani. Hivi hapo je, si kweli kwamba mtu mweupe aliumbwa ili kumtawala mtu mweusi? Hivi utajisikiaje unaamka asubuhi unakuta Kaff*ir amekaria kiti cha utawala? Hivi unajua kitakachotokea kwa wanawake wetu? Hivi kuna mtu anaweza kwamba mweusi ataitawala nchi hii.
                            NELSON MANDELA
Kwa hiyo tuna sababu nzuri ya kuwapeleka akina Mandela jela waozee huko na katika hili nadhani upo umuhimu wa kupewa pongezi kwani tungekuwa na uwezo wa kuwaangamiza lakini sasa wanaishi.

Napenda kuwatangazia mikakati mipya ya kuwaangamiza hawa weusi. Tutumie sumu kuwamaliza.

Kamwe tusirushusi idadi ya watu weusi iendeleekukua vinginevyo tutakwisha. Tayari nimeshawaleta wanasayansi ambao wamekuja na sehemu kubwa ya mzigo wa sumu na ninawasaka watafiti wengine zaidi waangalie sehemu murua za kuitumia sumu hiyo kwa lengo la kuwaangamiza weusi.

Sehemu nzuri za kuwaangamiza kwa sumu ni hospitali na pia katika usambazaji wa chakula inaweza kutumika. Tumetengeneza sumu inayoua taratibu na kupunguza uwezo wa uzazi. Lakini hofu yetu ni kwamba itakuwaje kama sumu hiyo itaangukia mikono yao.

Hata hivi tunafanya kila yuwezalo kuhakikisha kuwa sumu hiyo inabaki katika himaya yetu. Pili, watu weusi wanapenda sana pesa kwa hiyo tunaweza kuwatenga kwa njia hiyo. Wataalamu wetu wanalifanyia kazi suala hilo ili mtu mweusi amchukie mweusi mwenzake.

Hawana upeo wa kufikiri na huyo ndiye kiumbe dhaifu kisicho na akili ya kuona mbali.

Kuna umuhimu mkubwa wa kupanga mambo hayo yaendelee kwa muda mrefu ili wasibaini kuwaua. Kwa kawaida mtu mweusi hapangi mikakati inayozidi mwaka mmoja. Na hapa napenda niwaombe kina mama wa ki Afrikaner wazae kwa fujo kuongeza idadi.
STEVE BIKO: ALIYEUAWA WAKATI WA SIASA ZA UBAGUZI AFRIKA KUSINI
Litakuwa jambo la maana pia kama kutatengwa vituo maalumu ambako vijana wa kike na kiume watakaa na serikali kuwawezesha ili wazae kwa idadi kubwa iwezekanavyo ili kuongeza idadi yetu. Wakati hilo likiendelea, lazima tuwabane watu weusi waachane na wake zao.

Ninayo kamati inayoratibu na inayoangalia njia nzuri ya kuwafanya watu hawa wachukiane na wauane wenyewe kwa wenyewe. Adhabu kwa mweusi aliyemuua mweusi iwe ndogo ili kuwapa hamasa ya kuendelea na mauaji.

Wanasayansi wangu wameshauri pia kuna ulazima wa kuwawekea sumu kwenye pombe, sumu ambayo itakuwa inawaua taratibu na kumaliza uwezo wa kuzaa pia. Njia kama hii na nyingine zifananazo na hii itawarahisisha kuwapunguza idadi.

Rekodi zinaonyesha pia kuwa mtu mweusi anapenda sana mwanamke mweupe. Hii ni nafasi nzuri kwetu. Wanawake wetu warembo wanaotumika katika mbinu za kuwaangamiza wapinzani wetu watatumika kuwaua hao wanaopinga ubaguzi wa rangi.

Hili jeshi letu la mwituni la mapenzi huku tukiwa na jeshi kama hilo kwa upande wa wanaume ambao watatafuta wanawake weusi. Pia serikali imeagiza Malaya kutoka Marekani na ulaya kwa ajili ya kukidhi haja yao.

Ombi langu la mwisho ni kwamba wajawazito wanapozaa hospitalini, watoto lazima wauwawe pindi tu wanapotoka tumboni. Hatuwalipi wale wauguzi kwa ajili ya kutuletea watoto weusi katika dunia hii bali kuwaangamiza.

Serikali yangu imetenga fungu maalumu la pesa kwa ajili ya kufanikisha mpango huo. Pesa inafanya lolote na kwa vile tunazo tuzitumie ipasavyo.

Kwa muda huu ndugu zangu weupe, msiyaweke moyoni wala msione aibu kuitwa wabaguzi na wala sijali mhandisi wa Mfalme wa ubaguzi.

Siwezi kugeuka nyani eti kwa sababu mtu kaniita nyani. Nitabaki kuwa nyota inayong’aa ….mtukufu Botha.

Leo naondoa mawingu; kesho nitajalibu mlima”.

HABARI HII ILIWAI KUTOLEWA NA GAZETI LA RAI, OKTOBA 19-25, 2006. UK. 17.

IMELETWA KWENU NA CHIWAMBO AUSI R (TEOFILO KISANJI UNIVERSITY-TEKU, BA SOCIOLOGY AND SOCIAL WORK) 18, March, 2012.

MAWASILIANO:-



1 comment:

Unknown said...

Nimekupata mkuu, endelea kutufahamisha