Thursday, March 20, 2014

BREAKING NEWS: Vifusi vya ndege vyaonekana Australia?

John Young meneja mkuu wa halmasshauri ya usalama wa ndege nchini Australia

Waziri mkuu wa Australia amesema kuwa mitambo ya satelite ya nchi hiyo imenasa picha za vitu vinavyoonekana kama vifusi ambavyo huenda ni vya ndege ya Malaysia iliyopotea siku 13 zilizopita.

Waziri mkuu huyo, Tony Abbott, ameambia bunge mjini Canberra kwamba picha za Satelite zimeonyesha vitu viwili vinavyofanana na vifusi vya ndege hiyo.
Taarifa hii imejitokeza karibu wiki mbili baada ya ndege hiyo kutoweka na abiria zaidi ya miambili kutoka mjini Kuala Lumpur Malaysia kuelekea Beijing.

Msemaji wa halmashauri ya usalama wa safari za ndege, John Young, baadaye alisema kuwa vifaa hivyo ambavyo kimoja kina ukubwa wa mita 24, vimeonekana umbali wa kilomita 2500 kusini Magharibi mwa pwani ya Australia.
Aliongeza kwamba,vifusi itakuwa vigumu kuviona vifusi hivyo na pia huenda sio vya ndege hiyo.

Wakati taarifa hii ilipotolewa, kulikuwa na ndege ya Australia katika neo hilo , ndege zaidi zinatarajiwa kuwasili katika eneo lenyewe na pia manowari ya jeshi inaelekea huko.
Chanzo: BBC Swahili

Sunday, March 16, 2014

YANAYOJIRI HUKO KALENGA



Inasikitisha, kuwa chaguzi ndogo kama hii ya Kalenga ni kielelezo cha udhaifu wetu kama taifa. Kwamba wapiga kura wasiozidi 70 elfu ' wanavamiwa' jimboni na watu kwa maelfu kutoka pande mbali mbali za nchi katika kushiriki kupigania kititi cha Ubunge.

 Na imefika mahala hata wapiga kura wale wa Kalenga wapatao 70 elfu hawapati nafasi ya kuwasikliliza wagombea ubunge bali wanawasikiliza waliokuja kupiga kampeni na kisha kuondoka ifikapo kesho Jumapili. Wagombea wao wamefunikwa. Ni laiti nusu tu ya fedha inayotumiwa na vyama kule Kalenga kwa kugharamia kampeni ingetumika kwa maendeleo, basi, ingetosha kuzisaidia kata kadhaa za Kalenga katika kuboresha huduma ya afya na elimu.... Inasikitisha.
Maggid,
Kunduchi Mtongani

Kura ya maoni jimbo la Crimea

                                                         bango la kampeni ya kura ya maoni Crimea
Wapigakura katika jimbo la Crimea leo wanapiga kura ya maoni kuhusiana na iwapo jimbo hilo lijitenge na Ukraine na kujiunga na Urusi, na kuzusha mzozo ambao ni sawa na uliokuwa wakati wa vita baridi.
Mzozo huo katika eneo hilo la pembe ya mashariki mwa bara la Ulaya umeiweka hali ya diplomasia katika mtafaruku.

Kiasi ya watu milioni 1.5 wanapiga kura katika eneo hilo, ambalo lina idadi kubwa ya watu wenye asili ya Urusi.
Uchaguzi ni kati ya kuwa sehemu ya Urusi ama kuchukua madaraka zaidi lakini kubakia Ukraine, lakini hakutakuwa na nafasi ya kuchakua kubakia kama ilivyo hivi sasa.

Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa saa 12 asubuhi na vitafungwa saa kumi na mbili jioni kwa saa za Ulaya ya mashariki, ambapo matokeo yatapatikana mara baada ya kufungwa vituo vya kupigia kura, licha ya kuwa kumekuwa na kauli mbiu inayosema "tuko Urusi" , mabango hayo yakiwa katika majengo ya serikali, hali ambayo inatoa ishara juu ya matokeo.

Mataifa ya magharibi
Mataifa ya magharibi yamesema hayataitambua kura hiyo ya maoni, wakati Urusi ikisisitiza kuwa ni mfano wa kuamua kujitawala kama ilivyofanya Kosovo.
Majeshi ya Urusi na wanamgambo wanaounga mkono Urusi wamedhibiti eneo hilo la rasi muda mfupi baada ya rais anayeungwa mkono na serikali ya Urusi Viktor Yanukovich kuondolewa madarakani mwezi uliopita baada ya miezi mitatu ya maandamano dhidi ya serikali yake ambayo yamesababisha umwagikaji wa damu.

Ulinzi mkali kabla ya kura hiyo ya maoni
Vituo vya kijeshi vya Ukraine katika eneo hilo, ambalo ni mahali Urusi ilipoweka meli zake za kivita tangu katika karne ya 18, vimezingirwa lakini hakuna mapambano ya silaha na haijafahamika ni nini kitatokea kwa vituo baada ya kura hiyo ya maoni.

Waandishi washambuliwa
Kumekuwa na mashambulizi kadha dhidi ya waandishi habari pamoja na wanaharakati wanaopendelea umoja , mashambulizi ambayo yameshutumiwa na shirika linalotetea haki za binadamu la Amnesty International kuwa yanatia wasi wasi mno.
Marekani imepuuzia kura hiyo ikiita "kura kwa mtutu wa bunduki" na serikali mpya ya Ukraine imeiita kura hiyo ya maoni kuwa ni batili na ina wasi wasi kuwa Urusi inajaribu kuchochea uasi mkubwa zaidi katika eneo lenye wakaazi wengi kutoka Urusi upande wa mashariki ya Ukraine.

Wanaharakati watatu wameuwawa katika miji wa mashariki ya Donetsk na Kharkiv muda kuelekea kura hii ya maoni kwa jimbo la Crimea na waungaji mkono wa Urusi wametoa wito wa kuwa na aina hiyo ya kura katika majimbo mengine ya Ukraine.

Wabunge wa Urusi wameidhinisha rais Vladimir Putin kuivamia Ukraine wakati akipenda , wakidokeza haja ya kuwalinda watu wenye asili ya Urusi dhidi ya watu wenye msimamo mkali wa kizalendo.

Ukraine iko katika hali kamili ya tahadhari kijeshi na katika mkesha wa kura hii ya maoni imeyashutumu majeshi ya Urusi kwa kukamata kijiji nje kidogo ya Crimea , ikisema, " Ukraine ina haki ya kutumia hatua zozote zinazowezekana kuzuwia uvamizi wa kijeshi wa Urusi.
Mwandishi: Sekione Kitojo / afpe
Mhariri: Amina Abubakar

Chanzo: DW Swahili

Urusi yakwamisha azmio la kulaani kura ya maoni ya Crimea

Kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, jijini New York.
Urusi imelipigia kura ya turufu azimio linaloungwa mkono na mataifa ya magharibi lenye kulaani kura ya maoni ya Crimea katika kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumamosi(15.03.2014).

Rasimu ya azimio hilo lenye kusema kura hiyo ya maoni ya Jumapili haitokuwa na maana imeungwa mkono na kura 13 katika Baraza la Usalama la nchi wanachama 15 lakini limekataliwa wakati Urusi mwanachama wa kudumu wa baraza hilo ilipotumia kura yake ya turufu kulizuwiya. China mwanachama mwengine wa kudumu wa baraza hilo haikushiriki katika kupiga kura hiyo na kuifanya Urusi izidi kutengwa katika suala la mzozo wa Ukraine.

China ambayo mara nyingi imekuwa ikiiunga mkono Urusi katika baraza hilo hususan katika kura kuhusiana na masuala ya Syria,wanadiplomasia wameiona hatua yake ya kujitowa kupiga kura ni matokeo mazuri ambayo yangeliweza kupatikana katika kura hiyo ya leo.

Balozi wa China katika Umoja wa Mataifa Liu Jieyi amesema kupitisha azimio kuhusu Ukraine wakati huu kutakuja tu kusababisha malumbano na kuifanya hali hiyo kuzidi kuwa ngumu.

Balozi wa Marekani Samantha Power ameliambia baraza hilo katika kikao chake cha saba cha dharura kuhusu Ukraine tokea kuanza kwa mzozo wa nchi hiyo kwamba Urusi iliotengwa, ilioko peke yake na inayofanya makosa imekwamisha kupitishwa kwa azimio hilo.

Ameongeza kusema katika hotuba yake fupi "Hivi tunavyozungumza vikosi vya ulinzi vya Urusi vinakusanyika kwenye mpaka wa mashariki na Ukraine."
Kerry, Lavrov washindwa kupata muafaka
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov (kushoto) na mwenzake wa Marekani, John Kerry.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov (kushoto) na mwenzake wa Marekani, John Kerry.
Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov, na mwenzake wa Marekani, John Kerry, wameshindwa kutatua tofauti zao juu ya mkoa huo wa Crimea, hata baada ya mazungumzo yao ya masaa nyumbani kwa balozi wa Urusi nchini Uingereza hapo jana (tarehe 14 Machi 2014).

Wakizungumza kwa pamoja na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao, mawaziri hao walionesha wazi kutokufikia makubaliano yoyote katika suala hilo tete linalozidi kuzigawa serikali zao, licha ya wote kusema kuwa yalikuwa mazungumzo ya kuridhisha.

Hata hivyo, Lavrov alirejelea msimamo wa nchi yake kwamba haina nia ya kuingilia kijeshi nchini Ukraine, ingawa hakuonesha uwezekano wowote wa pande hizo mbili kuwa na msimamo wa pamoja juu ya hali ya mambo kwenye mkoa wa Crimea.
Kwa upande wake, Kerry alisema baada ya mazungumzo hayo marefu, mwenzake Lavrov aliweka wazi kwamba "Rais Putin hayuko tayari kuamua chochote juu ya Crimea hadi kura ya maoni itakapofanyika", akiongeza kwamba msimamo wa Marekani juu ya kura hiyo ya maoni unabakia kuwa ule ule kuwa "inakiuka katiba ya Ukraine, na sheria za kimataifa na tunaamini si halali."

Kwa mara nyengine, Lavrov alizionya nchi za Magharibi dhidi ya kuiwekea nchi yake vikwazo vya kidiplomasia au vya kiuchumi kutokana na msimamo wake juu ya Ukraine. Wakaazi wa Crimea watapiga kura ya maoni ya ama kujiunga na Urusi au kuwa taifa huru hapo kesho, baada ya bunge la mkoa huo kuamua wiki iliyopita kujiunga na Urusi. Kesho hiyo hiyo pia, wanadiplomasia wa Umoja wa Ulaya wataamua hapo kesho juu ya orodha ya Warusi watakaolengwa na vikwazo hivyo.

Marekani yawaonya raia wake
Waungaji mkono wa Ukraine katika mji wa Simferopol, Crimea, wakipinga kura ya maoni ya kuamua ikiwa mkoa huo ujiunge na Urusi ama la.
Waungaji mkono wa Ukraine katika mji wa Simferopol, Crimea, wakipinga kura ya maoni ya kuamua ikiwa mkoa huo ujiunge na Urusi ama la.

Wakati hayo yakiendelea, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imewaonya raia wake juu ya uwezekano wa mapambano ya kijeshi kwenye mpaka wa Ukraine na Urusi na pia vuguvugu la kuipinga Marekani nchini Urusi, huku Crimea ikijiandaa na kura hiyo ya kujiunga na Urusi.

Licha ya kusema kwamba haina taarifa yoyote ya mgogoro wa kijeshi ndani ya Urusi kutokana na wasiwasi uliopo kwenye eneo hilo au kitisho chochote kwa raia wake, Marekani imesema kupitia "onyo la safari" kwamba raia wake walio kwenye eneo hilo na wale wanaopanga kwenye huko wanapaswa kuwa na tahadhari.

Katika kile kinachoonekana kama makabiliano mabaya kabisa tangu kuanza wakati wa Vita Baridi, Urusi ilituma wanajeshi zaidi mkoani Crimea siku ya Ijumaa na kutishia kupeleka wanajeshi kwenye maeneo mengine ya Ukraine kufuatia ghasia zilizotokea usiku wa Alhamis kwenye mkoa wa Donetsk.
Mwandishi: Mohammed Khelef/Reuters/AFP/dpa
Mhariri: Amina Abubakar

Chanzo: DW Swahili

Ndege ya Malaysia ilibadili mkondo 'Maksudi'

                                     Marubani wawili waliokuwa wanaendesha ndege ya Malaysia
Mtambo wa mawasiliano wa ndege ya Malaysia iliyotoweka wiki moja iliopita, ulizimwa kwa maksudi.
Hii ni kwa mujibu wa taarifa ya waziri mkuu wa Malaysia Najib Razak.
Taarifa zinazohusiana
Asia

Alisema kuwa ndege hiyo ilibadili mkondo na kuendelea kuruka kwa saa saba zaidi ya muda uliotakiwa kulingana na mawasiliano yaliyorushwa kwa Satelite na mtambo wa Radar.

Bwana Razak aliongeza kwamba hatua za ndege hiyo zinaambatana na matakwa ya mtu binafsi ambaye alikuwa akiielekeza.
Ngege hiyo ilitoweka wiki jana ikiwa imewabeba abiria 239.
Nusura bwana Razak aseme kuwa ndege hiyo ilitekwa nyara ingawa alisisitiza kwamba uchunguzi ungali unaendelea kubaini ilikokwenda ndege hiyo.
Dhana kwamba ndege hiyo ilitekwa nyara ilipingwa vikali awali lakini sasa inaonekana imerejea kuwa mojawapo ya sababu za kutoweka kwake.

Mtambo wa mawasiliano wa ndege hiyo ulizimwa kwa maksudi na huenda marubani walifanya hivyo kwa hiari au kwa kulazimishwa.
Darubini sasa inawalenga watu waliokuwa wameabiri ndege hiyo na wafanyakazi wa ndege.

Wapelelezi watataka kujua ikiwa kumekuwa na tukio lolote la matatizo ya kiakili, changamoto za kifamilia na shinikizo la mawazo kwa yeyote aliyekuwa katika ndege hiyo, hasa marubani.

Ni wiki nne tu zimepita tangu rubani wa ndege ya Ethiopia kuiteka nyara ndege akitaka kupata hifadhi nchini Switzerland.
Marubani wa ndege hiyo ya Malaysia walikuwa na rekodi nzuri tu ya kikazi ingawa polisi bado wamefanya msako nyumbani kwao.

Chanzo: BBC Swahili

Ufaransa yazongwa na hewa chafu

Serikali ya Ufaransa imezindua mfumo wa kuendesha magari kwa siku maalum mjini Paris, kama njia ya kujaribu kupunguza uchafuzi mkubwa wa hewa.
Kuanzia Jumatatu, madereva watatumia magari yao mara moja moja huku siku zingine wakitembea kwa miguu katika mji mkuu Paris.

Hii ni mara ya pili tangu mwaka 1997 kwa hatua hiyo kuongezwa nguvu.
Serikali iliafikia hilo katika tangazo lake la siku ya Jumamosi baada ya kiwango cha uchafuzi wa hewa kuzidi kwa siku tano za wiki mfululizo hasa katika mji wa Paris na viunga vyake.

Hali ya ukungu unaotanda kote Paris ni kutokana na hali ya baridi kali usiku na mchana jambo linalozuia hewa kuchanganyika vyema.
Mnamo siku ya Ijumaa serikali ilitoa usafiri bila malipo kwa wananchi ili kuwashashwishi kuacha kutumia magari yao. Hali hiyo itaendelea siku ya Jumatatu.

Wanasayansi wanasema kuwa uchafuzi wa mazingira mjini Paris umekuwa mbaya sana hata kuliko mji wa Beijing wenye mazingira chafu zaidi ya hewa duniani.
Mnamo siku ya Ijumaa, kiwango cha uchafuzi wa mazingira kilikuwa kikubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa.

Serikali itatathmini viwango vya uchafuzi siku ya Jumatatu na kuona ikiwa itaongeza muda wa agizo hilo au la.

Chanzo: BBC Swahili

Mkanyagano waleta maafa Nigeria


Watu kadhaa wameuwawa na wengine wengi kujeruhiwa baada ya vurumai kutokea pale walipokuwa wakihudhuria zoezi la serikali la kuwaajiri watu kazi katika miji kadhaa Nchini Nigeria.

Maelfu ya watu waliokuwa na hamu kubwa ya kupata ajira, walijitokeza kwa wingi katika zoezi hilo kote Nchini humo. Walikuwa wamejitokeza katika ofisi za wizara ya uhamiaji.
Walioshuhudia wamesema kuwa karibu watu saba wamekufa pale umati uliposukumana katika lango kuu la uwanja wa kitaifa wa michezo mjini Abuja.
Wengine walipoteza maisha yao katika uwanja wa michezo wa Port Harcourt na uwanja wa shule katika mji wa Minna.

Tatizo la ajira kwa vijana ni kubwa mno Nchini Nigeria huku zaidi ya robo tatu ya vijana walio na chini ya umri wa miaka 25 wakiwa bila kazi.
Maelfu ya watu walijitokeza kufanya mtihani wa ajira - inaarifiwa mkanyagano ulitokea walipojaribu kufika katikati ya uwanja.

Chanzo: BBC Swahili

Majeshi ya Somalia, AU wakomboa miji kadhaa kutoka kundi la Alshabab


Majeshi ya Somalia na yale ya Umoja wa Afrika  (AU) wamekomboa miji kadhaa kutoka kwa wanamgambo wa  Al-shabab katika kile walichokiita juhudi mpya za kuliondoa kundi  hilo kutoka kwenye ngome zake nchini humo.

Moja ya maeneo ni  katika mji wa Burdhubo ambao ulikuwa ni ngome kuu ya Alshabab kusini mwa Somalia. Majeshi kutoka Umoja wa Afrika  nchini  Somalia yajulikanayo kama AMISOM na jeshi la taifa la Somalia yalichukua  tena udhibiti wa eneo hilo Jumapili baada ya siku moja ya mapigano.

Kanali Ali Hamud msemaji wa AMISOM aliimbia VOA kwamba wapiganaji wa Alshabab wanarudi nyuma mara tu wanapoona majeshi ya AMISOM,  lakini hilo bado linaangaliwa ikiwa badala yake wanajipanga kwa vita vya  msituni.

Miji mingine ambayo jeshi la Somalia na AMISOM wamekomboa tangu Ijumaa ni pamoja na Weel Dehyn,Wajid,Rabdhure Ted na Hudur. Wako katika mikoa ya Gedo na Bakool karibu na mpaka wa Ethiopia na kilometa chache kutoka mji mkuu wa Somalia Mogadishu.

Chanzo: BBC Swahili

KATUNI YA LEO NA Chiwambo's Blog


Saturday, March 15, 2014

KIJIJI CHA NANDEMBO HUKO WILAYANI TUNDURU


KATUNI YA LEO


Baraza la Usalama kupiga kura juu ya Ukraine

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linakutana kwa dharura kulipigia kura azimio dhidi ya kura ya maoni mkoani Crimea linaloungwa mkono na Magharibi, huku Marekani na Urusi zikishindwa kukubaliana juu ya Ukraine.

Kikao hicho cha dharura ambacho kinapangwa kuanza saa 5:00 asubuhi kwa saa za New York hivi leo (tarehe 15 Machi 2014), kimeitishwa kwa ombi la serikali ya Marekani. Wanadiplomasia wanasema wanatarajia Urusi kulipigia kura ya veto azimio hilo, lakini bado haijafahamika ikiwa China nayo itafanya hivyo hivyo au la.

Kawaida Urusi na China huwa na msimamo mmoja kwenye Baraza hilo la Usalama, hasa kuhusiana na suala la Syria. Chanzo chengine cha kidiplomasia kimesema kuwa lengo pekee la azimio hilo ni kuifanya China ijizuwie kupiga kura na hivyo kuitenga zaidi Urusi.
Inasemekana kuwa azimio hilo limeandikwa kwa lugha ambayo itaishawishi China, kwani haliitaji moja kwa moja Urusi, halitishii vikwazo na wala kuitaka Urusi kuondoa wanajeshi wake mkoani Crimea, ambako kawaida imekuwa na kituo cha kijeshi. Msimamo wa China umekuwa ni kuheshimu uhuru na mamlaka ya taifa na kujizuia kuingilia mambo ya ndani ya nchi husika.

Kerry, Lavrov washindwa kupata muafaka
Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov, na mwenzake wa Marekani, John Kerry, wameshindwa kutatua tofauti zao juu ya mkoa huo wa Crimea, hata baada ya mazungumzo yao ya masaa nyumbani kwa balozi wa Urusi nchini Uingereza hapo jana (tarehe 14 Machi 2014).

Wakizungumza kwa pamoja na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao, mawaziri hao walionesha wazi kutokufikia makubaliano yoyote katika suala hilo tete linalozidi kuzigawa serikali zao, licha ya wote kusema kuwa yalikuwa mazungumzo ya kuridhisha.

Hata hivyo, Lavrov alirejelea msimamo wa nchi yake kwamba haina nia ya kuingilia kijeshi nchini Ukraine, ingawa hakuonesha uwezekano wowote wa pande hizo mbili kuwa na msimamo wa pamoja juu ya hali ya mambo kwenye mkoa wa Crimea.

Kwa upande wake, Kerry alisema baada ya mazungumzo hayo marefu, mwenzake Lavrov aliweka wazi kwamba "Rais Putin hayuko tayari kuamua chochote juu ya Crimea hadi kura ya maoni itakapofanyika", akiongeza kwamba msimamo wa Marekani juu ya kura hiyo ya maoni unabakia kuwa ule ule kuwa "inakiuka katiba ya Ukraine, na sheria za kimataifa na tunaamini si halali."

Kwa mara nyengine, Lavrov alizionya nchi za Magharibi dhidi ya kuiwekea nchi yake vikwazo vya kidiplomasia au vya kiuchumi kutokana na msimamo wake juu ya Ukraine. Wakaazi wa Crimea watapiga kura ya maoni ya ama kujiunga na Urusi au kuwa taifa huru hapo kesho, baada ya bunge la mkoa huo kuamua wiki iliyopita kujiunga na Urusi. Kesho hiyo hiyo pia, wanadiplomasia wa Umoja wa Ulaya wataamua hapo kesho juu ya orodha ya Warusi watakaolengwa na vikwazo hivyo.

Marekani yawaonya raia wake
Wakati hayo yakiendelea, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imewaonya raia wake juu ya uwezekano wa mapambano ya kijeshi kwenye mpaka wa Ukraine na Urusi na pia vuguvugu la kuipinga Marekani nchini Urusi, huku Crimea ikijiandaa na kura hiyo ya kujiunga na Urusi.

Licha ya kusema kwamba haina taarifa yoyote ya mgogoro wa kijeshi ndani ya Urusi kutokana na wasiwasi uliopo kwenye eneo hilo au kitisho chochote kwa raia wake, Marekani imesema kupitia "onyo la safari" kwamba raia wake walio kwenye eneo hilo na wale wanaopanga kwenye huko wanapaswa kuwa na tahadhari.

Katika kile kinachoonekana kama makabiliano mabaya kabisa tangu kuanza wakati wa Vita Baridi, Urusi ilituma wanajeshi zaidi mkoani Crimea siku ya Ijumaa na kutishia kupeleka wanajeshi kwenye maeneo mengine ya Ukraine kufuatia ghasia zilizotokea usiku wa Alhamis kwenye mkoa wa Donetsk.
Mwandishi: Mohammed Khelef/Reuters/AFP/dpa
Mhariri: Amina Abubakar

Chanzo: DW Swahil

Yanga, Azam kikaangoni

Dar es Salaam. Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, inaendelea leo kwa mechi mbili zitakazopigwa kwenye viwanja viwili tofauti, Jamhuri Morogoro na Azam Complex Jijini Dar es Salaam.

Kwenye Uwanja wa Jamhuri, Yanga iliyotolewa kwenye Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Al-Ahly, inaanzia kwenye uwanja huo kuumana na Mtibwa Sugar ya Morogoro huku Azam FC ikiwa kwenye uwanja wake wa nyumbani kupambana na Coastal Union ya Tanga.

Yanga iliyoaga mashindano ya Afrika kwa penalti 5-4, ina fursa ya kupora madaraka ya uongozi wa ligi lakini endapo tu itaifunga Mtibwa Sugar.

Mabingwa hao watetezi wa Ligi wapo nafasi ya tatu kwenye msimamo, wakiwa na pointi 38 nyuma kinara Azam FC yenye pointi 40 kileleni. Mbeya City inakamata nafasi ya pili ikiwa na pointi 39.

Endapo itaibuka na ushindi katika mchezo wa leo, Yanga itafikisha pointi 41 na kuishusha Azam hadi katika nafasi ya pili sanjari na kuisukuma Mbeya City katika nafasi ya tatu.

Hata hivyo, Yanga inajivunia  faida ya kuwa na  mechi nyingi mkononi tofauti na Azam na Mbeya City , kwani imeshuka uwanjani mara  17 na ushinda mechi 11, sare tano na kufungwa mchezo mmoja.

Azam tayari  imecheza mechi 18, kati ya hizo imeshinda 11, sare saba na haijapoteza mchezo, wakati Mbeya City imeshuka uwanjani mara 21, imeshinda mechi 10, sare tisa na imenyukwa mara mbili.

Kocha wa  Yanga, Hans Van Der Pluijm ambaye atamkosa winga wake, Mrisho Ngasa aliyeumia wakati wa mechi dhidi ya Al-Ahy ametamka kwamba anataka kutwaa ubingwa ili iwe zawadi ya kuwafuta machozi mashabiki wa timu hiyo wenye majonzi ya kuondolewa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Naye kocha msaidizi wa Yanga, Boniface Mkwasa alisema kuwa wanaelekeza nguvu hizo katika mchezo na Mtibwa Sugar ili kuhakikisha wanaondoka na ushindi.

“Mtibwa Sugar wamekuwa wakiisumbua Yanga katika Uwanja wa Jamhuri, lakini hiyo ni hali ya mchezo. Ninachoweza kusema baada ya kutolewa Ligi ya Mabingwa tumeelekeza nguvu katika michezo ya Ligi Kuu,”alisema Mkwasa.

Kwa upande wake, Kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Maxime amekiri kwamba mechi hiyo itakuwa ngumu kwa upande wake, lakini amejiandaa kwa mapambano.

Naye, nahodha wa Coastal Union, Juma Nyoso amesema wanaiheshimu Azam kama timu nje ya uwanja lakini si ndani ya uwanja, hivyo dakika 90 ndizo zitatoa jibu nani mbabe kati ya timu hizo.
Chanzo: Mwananchi


Kinana: Wasaliti CCM wako kumi

Dodoma. Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana amesema hana mpango wa kuwahoji Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wanaotokana na chama hicho kwa sababu ya misimamo yao inayokinzana na miongozo ya chama, kwa kuwa anawafahamu wote kwa majina na idadi yao haizidi kumi.

Kauli hiyo ya Kinana inafuatia taarifa zilizoripotiwa na gazeti hili hivi karibuni kuwa, CCM kimeanza kuwahoji baadhi ya wabunge wake, ambao ni Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kwa sababu ya kupingana na maelekezo ya chama hicho kuhusu Muundo wa Serikali mbili.

“Sisi (CCM) hatuhoji mtu kwa sababu ya kuwa na msimamo tofauti, kwani hawa wenye msimamo tofauti na chama hawazidi kumi ama siyo zaidi ya 15,” alisema Kinana na kuongeza;

“Hawa watu mimi nawajua kwa majina, mmoja (jina tunalo) ni hatari zaidi kwa sababu anaweza kuwakusanya wengine na kuwashawishi wafuate msimamo wake, lakini waliobaki wote, hawatishi kwa kuwa wanabaki na misimamo yao wenyewe.”

Kwa mujibu wa habari hiyo, wajumbe waliohojiwa ni wale wanaotokana na Ubunge wa Jamhuri ya Muungano na ambao wanataka Muundo wa Serikali tatu. “Ni kweli hata mimi niliitwa na akaniambia (mwakilishi wa chama) ametumwa aniletee ujumbe kuwa niko kwenye orodha ya watu 90 na nikiendelea na msimamo wangu nitachukuliwa hatua,” alieleza mmoja wa wajumbe waliodai kuwa wamehojiwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM.

Maelezo ya Kinana

Kinana aliliambia gazeti hili kuwa, kulingana na muundo wa chama hicho tawala, viongozi wanaoweza kuwahoji watu ni yeye Katibu Mkuu, Makamu Mwenyekiti, Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu na Mwenyekiti wa chama Taifa. “Tena tunafanya hivyo kwenye vikao maalumu na kwa sababu ambazo haziwezi kuwa siri.”

Kinana alieleza kuwa taarifa kwamba CCM imewahoji watu 90 kutokana na kuwa na misimamo tofauti na chama hicho kuhusu Serikali mbili na kura ya wazi, siyo za kweli na anaamini imesambazwa na watu kwa malengo yao binafsi. Kinana anafafanua kuwa CCM kama chama kikubwa nchini chenye wafuasi karibu nchi nzima, hakiwezi kudhibiti mitizamo ya watu na kimsingi tofauti za mitazamo ndiyo msingi wa demokrasia.

Novemba 20 mwaka 2012 akizungumza katika kipindi cha Jenerali on Monday kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Kinana alitoa onyo kwa makada wasaliti kuwa atasimamia utekelezaji wa uamuzi wa Halmashuari Kuu ya CCM (Nec) ya kuwabaini na kuwaondoa viongozi wanaokwenda kinyume na matakwa ya chama na kukipaka matope.

Kura ya wazi na Serikali mbili

Katika hatua nyingine, Kinana alizungumzia msimamo wa chama hicho wa kura ya siri na muundo wa Serikali mbili, akieleza kuwa siyo jambo la ajabu, kwani katika mchakato wa kutunga katiba, kila kundi lina maoni na mtazamo wake na kuutetea kwenye mijadala.

“Wanaosema kuna vyama havina msimamo pale bungeni ni waongo. Siyo vyama tu, kila kikundi kina msimamo unaotokana na uchambuzi wao wa hali ya siasa nchini na wanachofikiri kina masilahi kwa nchi na watu wanaofuata mtazamo wao. Hawawezi kuniambia kama Lipumba (Profesa Ibrahim) na Mbowe (Freeman), hawana wanachosimamia kwenye mjadala huo wa Bunge Maalumu,” alisema na kusisitiza:
“Watanzania wasitarajie miujiza, lazima mivutano ya aina hiyo iwepo, kwani kila kundi linajitahidi kupenyeza mawazo yake na wanaoitetea misimamo hiyo ni watu. Kikubwa hapa sasa ni uvumilivu, watu wavumiliane na wazungumze kwa hoja na mwisho wa yote wafikie mwafaka.”

Alipoulizwa kama ni kweli CCM imekuwa ikiwashinikiza wajumbe wake kusimamia matakwa ya chama hicho, alijibu “Siyo CCM tu, CUF wanakutana na Chadema wanakutana, tena kila siku. Hili ni jambo la kawaida.”

Anasema tatizo siyo chama kuwa na msimamo, bali chama kutokukubali kubadili misimamo yake hata kama haikuwa sawa. Unaweza kuwa na msimamo wako, lakini ukaja mbele ya wenzako, ukagundua kuwa hauko sahihi, ikifikia hapo unapaswa kulegeza kamba ili uingize mawazo ya wenzako pia kwenye hoja zako, alisema.

Wito kwa Wajumbe wa Bunge la Katiba

Kinana ametoa wito kwa Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba akiwataka watambue kuwa Tanzania siyo nchi ya kwanza kutengeneza katiba.

Alisema zipo nchi nyingi duniani, ikiwamo India, Indonesia, Columbia, Kenya na Pakistan ambazo zilitumia muda mrefu zaidi kutunga katiba zao.

“Sisi kutumia majuma matatu kutengeneza kanuni za kuongoza Bunge Maalumu la Katiba, ni hatua nzuri tunayopaswa kujivunia,” alisema.

Kinana aliendelea kueleza kuwa pamoja na tofauti zinazojitokeza katika mijadala ya Bunge hilo Maalumu, makundi yanayounda Bunge hilo yanapaswa kutambua utaifa na uzalendo na ikilazimika waache tofauti zao ili wawe na mwelekeo wa pamoja katika kufikia mwafaka unaokusudiwa.

“Kwa hali hiyo pamoja na tofauti zetu, tusiondoke kwenye lengo. Mimi naamini katiba tunayoitaka itapatikana ila safari ya kuipata ni ndefu na ngumu.”

Chanzo: Mwananchi

West Brom yamtimua Nicolas Anelka

Mchezaji wa klabu ya soka ya West Brom, Nicolas Anelka amefutwa kazi kwa kosa la utovu wa nidhamu.
Klabu hiyo iliamua kuchukua hatua hiyo baada ya Anelka kutangaza kupitia mtandao wa kijamii kuwa anaacha kazi.

Anelka alisema kuwa anaondoka katika klabu hiyo baada ya kukosa kutatua tofauti zilizopo kati yake na Albion kuhusu ishara yake yenye utata ambayo inasemekana kuwa ya kibaguzi dhidi ya wayahudi.

Mshambuluaji huyo mwenye umri wa miaka 35, alipigwa marufuku kutocheza mechi tano na kutozwa faini ya pauni 80,000 na shirikisho la soka Uingereza ,kwa kufanya ishara hiyo, baada ya kuingiza bao dhidi ya klabu ya West Ham mwezi Disemba.
West Brom imechukua hatua ya kumfuta kazi Anelka kutokana na ishara hiyo na pia kwa sababu ya matamshi yake kwenye mtandao wa kijamii.


Ishara hii inapigiwa debe na msanii wa Ufaransa Diedonne M'bala M'bala
Awali aliachishwa kazi mwa muda na Albion, wakati klabu hiyo ilipokuwa inafanya uchunguzi wake binafsi.
Mapema siku ya Ijumaa, Anelka alitangaza kwenye mitandao ya kijamii kuwa anaondoka katika klabu hiyo.

Aliandika: "kufuatia mazungumzo kati yangu na maafisa wa klabu, kuna masharti kadhaa ambayo wamenipa kabla ya kujiunga tena na klabu hiyo, Masharti ambayo siwezi kuyakubali.''


Hata hivyo klabu ilisema kuwa masharti yaliyotolewa kwa Anelka ni pamoja na kumtaka awaombe msahama mashabiki , wadhamini na jamii kwa ujumla kwa athari iliyotokana na ishara yake aliyoifanya Disemba tarehe 28 na pili akubali kutozwa faini.
Chanzo: BBC