Thursday, February 14, 2013

NAFASI ZA UALIMU 26,537 ZATANGAZWA


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa.(Picha na Maktaba).


Jumla ya waalimu 26,537 wameajiriwa na serikali kwa mwaka wa fedha 2012/13. Walimu wa ngazi ya cheti walioajiriwa ni 13,568. Kati yao walimu 13,527 wamepangiwa kufanya kazi katika shule za msingi zilizopo kwenye halmashauri na walimu 41 wamepangwa katika shule za msingi za mazoezi zilizopo chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Jumla ya walimu wa sekondari na vyuo vyuo vya ualimu walioajiriwa ni 12,973 wakiwemo walimu walimu wa shahada 8,887 na wa stashahada ni 4,086.

MAGAZETINI LEO ALHAMISI 14, FEBRUARY, 2013








Wednesday, February 13, 2013

Mkuu wa tume ya uchaguzi Zimbabwe ajiuzulu



Mabango ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2008


Mkuu wa tume ya uchaguzi nchini Zimbabwe amejiuzulu kwa sababu za kiafya
Hatua ya Bwana Simpson Mutambanengwe, inakuja huku Zimbabwe ikijiandaa kwa kura ya maoni kuhusu katiba mpya pamoja na uchaguzi utakaofanyika baadaye mwaka huu.
Waziri mkuu Morgan Tsvangirai, amekuwa akishinikiza kufanyika mageuzi katika tume ya uchaguzi ili kuhakikisha kuwepo uchaguzi huru na wa haki.
Uchaguzi huo utakuwa ishara ya kumalizika kwa utawala wa serikali ya Muungano iliyoundwa baada ya ushindi wa Rais Robert Mugabe katika uchaguzi uliofanyika 2008 na uliokumbwa na ghasia na vurugu.
Bwana Tsvangirai, kiongozi wa chama cha MDC alisusia duru ya pili ya uchaguzi mwaka huo baada ya kudai kuwa alipokonywa ushindi wake katika duru ya kwanza.
Tsvangirai pamoja na Mugabe wanatarajiwa kugombea urais katika uchaguzi huo.
Chama cha Rais, Mugabe, Zanu-PF, pia kilidaawa kufanya ghasia dhidi ya wafuasi wa upinzani, madai aliyoyakanusha.
Waziri wa sheria, Chinamasa, alisema kuwa Mugabe alikubali kujiuzulu kwa Bwana Mutambanengwe, ambaye ni jaji mstaafu, aliyechukua wadhifa huo baada ya uchaguzi uliokumbwa na utata mwaka 2008.
"sababu za kiafya ndizo zimempelekea kujiuzulu,'' alisema Chinamasa
Mrithi wa Mutambanengwe, atateuliwa baada ya majadiliano kati ya viongozi wa serikali ya Muungano.
Mwezi jana shirika la kutetea haki za binadamu, Human Rights Watch, liliitisha mageuzi katika tume ya uchaguzi , idara ya mahakama na vyombo vya habari likidai kuwa zinaunga mkono chama cha Zanu PF

Papa ahutubia baada ya kujiuzulu

Papa anatarajiwa kujiuzulu rasmi mwishoni mwa mwezi Februari



Kiongozi wa kanisa katoliki duniani, Papa Benedict wa kumi na sita amewashukuru waumini kwa maombi yao kwake katika hotuba yake ya kwanza hadharani tangu kutangaza kuwa anajiuzulu
Papa alishangiliwa na maelfu ya watu alipokuwa anajianda kutoa hotuba yake ya kila wiki mjini Vatican.
Alisema anajiuzulu kwa sababu anaelewa fika kuhusu hali yake ya kiafya inavyoendelea kudhoofika na anavyoishiwa na nguvu kutekeleza majiku yake.
Baadaye leo ataongoza misa yake ya mwisho katika kanisa ya St Peter's Basilica.
Tangazo la kujizulu alilitoa mwishoni mwa Februari,
Papa mwenye umri wa miaka 85, na ambaye jina lake kamili ni Kadinali Joseph Ratzinger ataendelea na majuku yake kama kawaida hadi siku atakapojiuzulu rasmi.
Katika muda wa wiki sita zijazo, Papa mpya anatarajiwa kuteuliwa.
Akiwa na umri wa miaka 78, kadinali Joseph Ratzinger, alikuwa mmoja wa Papa wazee zaidi kuwahi kuteuliwa kuongoza kanisa
Alichukua wadhifa wake wakati ambapo kanisa lilikuwa linakumbwa na kashfa nyingi ikiwemo visa vya kuwaharibu watoto vilivyofanywa na makasisi wa kanisa hilo.

Source: http://www.bbc.co.uk/swahili

KATUNI YA WIKI NA CHIWAMBO'S BLOG


MOTO WA GESI MTWARA WAANZA KUFUKUTA TENA

                                maandamano dhidi ya gesi asilia ya Msimbati mkoani Mtwara.

VURUGU za kupinga ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam uliotulia kwa takriban wiki mbili sasa, umeibuka upya.

Vurugu hizo ziliibuka upya juzi baada ya jengo la Ofisi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kata ya Majengo Mtwara Mjini, kuchomwa moto usiku wa kuamkia juzi na kundi la watu wasiojulikana.


Habari zinasema kuwa hakukuwa na madhara makubwa ya tukio hilo kutokana na umati mkubwa wa watu kujitokeza kuzima moto huo.

Hadi moto huo unazimwa, milango na madirisha ya ofisi hiyo, ilikuwa imeteketea kabisa.

Mbali ya kuchoma jengo hilo, kundi hilo lilichoma matairi ya magari katika mitaa mbalimbali ya eneo hilo na kusababisha hofu kubwa kwa wananchi hao.

Hata hivyo uchunguzi wa gazeti hili, umebaini kuwa chanzo cha chokochoko hizo mpya ni viongozi wa muungano wa vyama vya upinzani kushindwa kuwapa wananchi majibu ya kikao chao cha siri cha hivi karibuni kati yao na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kilichofanyika kwa zaidi ya saa sita nyumbani kwake, jijini Dar es Salaam.

Habari zinasema kuwa viongozi hao waliporudi Mtwara hawakusema yaliyojiri Dar es Salaam kitendo kilichochochea fujo na kusababisha kiongozi wa msafara huo, Hamza Masudi Licheta kupigwa na wananchi wa Mtwara kwa tuhuma kuwa amewasaliti.

Hivi karibuni, viongozi wa muungano wa vyama vya TLP, NCCR Mageuzi, CHADEMA, Sau, APPT Maendeleo, DP, UDP, na ADC, walishiriki mkutano na Waziri Mkuu Pinda usiku kujadili suala la mzozo wa gesi ya Mtwara.

Haikubainika sababu hasa zilizofanya mkutano huo ufanyike usiku nyumbani kwa Waziri Mkuu na ambao haukuripotiwa na chombo chochote cha habari.

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wenzake, mwenyekiti wa umoja huo, Hamza Masudi Licheta, alisema:

“Sisi tulisafiri toka Mtwara kuja Dar es Salaam kuonana na Waziri Mkuu kwa sababu alipokuwa Mtwara aliondoka kabla hatujafikia muafaka, hatukukubali kama Waziri Mkuu alivyosema, aliondoka mapeka kuwahi Dodoma na sababu aliyotoa alipokuwa Mtwara alisema anawahi Dodoma kwa kuwa uwanja wa ndege wa Dodoma hauna taa, jambo lililomlazimu kuondoka Mtwara kwa harakaharaka.”

Alipoulizwa na gazeti hili nani aliratibu safari yao kuja Dar es Salaam alisema, “Utaratibu wetu uliratibiwa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, na tulikuja tukafanya mkutano kuanzia saa mbili hadi saa saba usiku.”

Uchunguzi wa gazeti hili unaonyesha kuwa viongozi hao walisafiri toka Mtwara kuja Dar es Salaam na walilala katika nyumba ya kulala wageni inayoitwa Kisuma, iliyoko jijini Dar es Salaam.

Aliongeza: “Sisi hatukuitwa na Waziri Mkuu, sisi ndio tulitaka kuonana naye kumwambia kuwa wananchi wa Mtwara hawajamwelewa katika taarifa yake aliyotoa bungeni Dodoma, pili tulimtaka yeye aondoe ile marufuku ya mikutano ya hadhara kwani Waziri wa Mambo ya Ndani amepiga marufuku mikutano yote ya hadhara huko na sasa tunashindwa kuwaelimisha wananchi kuhusu suala hilo na kadiri wananchi wanavyokosa taarifa ndio hali inazidi kuwa mbaya sasa wananchi wameanza kutupiga na kututuhumu kuwa tumehongwa kwa kuwa hatuwezi kufanya mikutano kuelezea kilichotokea katika mkutano tuliofanya usiku nyumbani kwa Pinda Dar es Salaam.”

Hamza aliongeza, “Tumeenda kwa Waziri Mkuu ili kumwambia kuwa hatumtaki mkuu wa mkoa, hata kama aliomba radhi, sisi wananchi wa Mtwara hatuko tayari kufanya naye kazi, hatutampa ushirikiano, hivyo tulitegemea kuwa Waziri Mkuu angemwambia Rais, na kesho (leo) tumeambiwa Balozi wa Nigeria nchini anakuja Mtwara, hivyo hatutaki aandamane na mkuu wa mkoa.

Alipoulizwa nani aliwalipia gharama za safari toka Mtwara kuja Dar es Salaam na kurudi pamoja na malazi, alisema: “Huwa tuna utaratibu wa kuomba wananchi, hivyo tuna mfuko wa muungano wa vyama vya upinzani.”

Hata hivyo uchunguzi wa gazeti hili, umebaini kuwa kauli ya Waziri Mkuu kuwa wananchi wa Mtwara wameelewa suala la gesi kupitia viongozi wao imeongeza utata kutokana na mkutano huo wa usiku na viongozi wa vyama vya siasa.

Mwanasiasa mmoja maarufu nchini ambaye hakutaka kutajwa jina amehoji, “Kama Waziri Mkuu alieleweka Mtwara, kikao cha usiku na viongozi wa vyama vya upinzani ulikuwa wa nini? Kulikuwa na kitu gani cha kujadili kwa siri hadi viongozi waliporudi Mtwara hawakutoa taarifa kwa wananchi?”

Taarifa ya Waziri Mkuu aliyoitoa Bungeni, Januari 31, 2013 ilionyesha kuwa amefanikiwa kumaliza mgogoro wa gesi Mtwara, kitendo ambacho kilisifiwa na wananchi wengi akiwemo Rais Jakaya Kikwete.

Wakati akitoa taarifa Bungeni, Pinda alisema kuwa amekutana na makundi mbalimbali Mtwara na baada ya kufanya nao mazungumzo, wamemuelewa na kuacha vurugu.

“Mheshimiwa Spika, kama utakavyoona, kiwango cha vurugu na uharibifu wa mali za serikali na raia kilikuwa kikubwa. Kufuatia hali hiyo, Januari 27, 2013, nililazimika kukatisha safari yangu ya kuja Bungeni Dodoma na kwenda mkoani Mtwara,” alisema.
Kwa mujibu wa Pinda, lengo la ziara yake ilikuwa kujionea hali halisi ya ulinzi na Usalama mkoani Mtwara, kupata taarifa rasmi za matukio mbalimbali yaliyotokea katika siku za hivi karibuni mkoani humo.
Kutoka Juma Mtandablog

PANYA KITOWEO CHA BAADHI YA WATANZANIA

Hii ni picha ya Mama Akishughulikia kitoweo cha Panya ipasavyo. Kwenye panya hakuna mgogoro wa kuchinja kwani kwao ni halali. Hakuna dua, wala mgogoro wa kuchinja