Saturday, February 2, 2013

MAGAZETINI LEO 2, FEBRUARY, 2013










Friday, February 1, 2013

AJALI YAUA WATANO YAJERUHI 130 MBARALI MBEYA NI VIBARUA WA KAMPUNGA

 
WATU watano wamepoteza maisha na wengine 130 wamejuruhiwa vibaya  huku hali zao zikiwa mbaya baada ya Lori walilokuwa wakisafiria shambani kuacha njia na kupinduka katika kijiji cha  Mapogolo kata ya Itamboleo  Wilayani Mbarali Mkoani hapa.
Ajali hiyo imetokea leo saa 1:30 asubuhi ambapo lori hilo  ambalo ni mali ya Mwekezaji wa shamba la Kapunga Rice Project, na kwamba watu hao walikuwa wakielekea kwenye shamba la mwekezaji huyo lililkuwa limebeba vibarua hao zaidi ya 200 ambao ni wakazi kitongoji cha  Kapunga.
 Lori hilo lenye namba za uasjili T398 BSE Scania Tipa, ambalo lilikuwa likiendeshwa na dereva aliyejulikana kwa jina  Baraka Moreli, lilionekana likiwa katika mwendo kasi na   dereva huyo akiwa na lengo la kutaka kuipita pikipiki  iliyokuwa mbele yake. huku akishangiliwa na vibarua hao ipite ipite hiyo pikipiki haiwezi kutushinda sisi gari kubwa moja ya majeruhi alisema. ndipo walipofika kwenye kona dereva lilimshinda gari hilo na kupinduka
Akiwa Hospitalini hapo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro ambaye aliweza kufika hospitalini hapo alisema kuwa mara baada ya kupata taarifa ya ajali hiyo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya ,Mbarali Gullam Hussein Kiffuu, huku akiombwa kupatiwa msaada wa kuongezewa madaktari, kuongezewa vifaa vya mataibu sambamba na uwezekano wa kupata damu kwa ajili ya kuwaongezea majeruhi hao alifanikiwa kuwasiliana na uongozi wa hospitali ya Rufaa ya Mbeya, hospitali ya Mkoa ili kuweza kuona namna ya kwenda kuokoa maisha watanzania hao.
Kandoro, alisema kuwa  katika ajali hiyo wanaume wanne wamefariki na mwanamke mmoja. watatu wametambuliwa
Samweli Mapugilo mbena 30 mkazi wa Ilembula
Bon Mfupa 27 mkazi wa mapogolo na Edgar Mwakipesile 35 mkazi wa Nonde Mbeya
   Aidha, Kandoro alisema kuwa idadi ya majeruhi katika  ajali hiyo kuwa ni 130 ambapo wanawake ni 40 na wanaume 89 huku idadi ya watoto waliokuwa wameongozana na wazazi wao haikuweza kufahamika kwa haraka.
Pcha Mbeya yetu na Kamanga
Source: http://francisgodwin.blogspot.com

PICHA ZA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM MH. MANGURA AKIWA MKOANI KIGOMA KATIKA MIKUTANO YAKE PAMOJA NA VIONGOZI WENGINE WA CHAMA HICHO KUANZIA NGAZI YA WILAYA HADI KITAIFA











Monday, January 28, 2013

“MAGAZETI YA UDAKU NI JANGA LA TANZANIA”



JOHN F. KENNEDY (1917-1963)
“There is a traffic disadvantage in not having the abrasive quality of the press applied to you daily. Even though we never like it, and even though we wish they didn’t it, and even though we disapprove, there isn’t any doubt that we could not do the job at all in a free society without a very, very active press”.
                                  John F. Kennedy (1917-1963).
MAKALA YA CHIWAMBO
“MAGAZETI YA UDAKU NI JANGA LA TANZANIA”
                 
Nakubaliana sana na maneno ya President J. F. Kennedy aliposema “kuna hasara kubwa sana kwa kutokuwa na vyombo vya habari vye ubora. Do you know why? Vyombo vingi vya habari nchini vinapotoa zaidi habari za udaku inachangia mawazo ya watu kudumaa na kushindwa kufikiri nini tufanye ili kujiletea maendeleo ya mtu binafsi. Hizi gazeti au tv zenye ubora kwa kawaida hazipedwi. Kwa mfano Nchiya Tanzania kuna gazeti la Raia Mwema, Mwananchi, The citizen, The Gudian, Nipashe na hata lile lililofungiwa na serikali Gazeti la Mwanahalisi, ni         watu wachache ndio wanaosoma gazeti hizi. 
 
              Pia hata Wasomi wetu vyuoni wahasomi. Walio wengi wanasoma magazeti ya udaku na yale ya sport. Pamefikia mwanafunzi unamuuliza hivi leo kuja jambo gani limefunika sana vyombo vya habari mbalimbali. Atakujibu do you know what? Muda sina.
 
      Huyu mwanafunzi wa chuo kikuu anasema muda wa kusoma gazeti ambazoni quality News anasema hana time ila kwenye michezo hata akiliona la juzi au mwakajana anatamani liwe lake asome. Ninyi kama tegemeo letu la taifa mnadhani tutafika kweli.
 
      Mara nyingi utasikia “RAIS AFANYA MAUAJI YA KUFURU”, CHIWAMBO ZE DOCTOR KAFUMANIWA LIVE, WAZIRI AUSI KAKUTWA NA PEMBE ZA TEMBO”. Mmmmmmmmh!!!! Ingia humo ndani usomo uone utumbo uliopo. Hauendani na kitu wanachozungumzia. Eti Rais wanayemzungumzia ni Yule wa wajinga Chikaje street.
 
     Kwanini waandishi kama hawa wasifungiwe tu. Je elimu yake ina faida gani. Kama ana “LAW DEFORMATION” kwanini anashindwa kuandika kitu kinachoendana na hali halisi. Ama kweli “KILIO CHA SAMAKI MACHOZI HUISHIA MAJINI”. Huwezi kuona watanzania wanatesekaje huko chini. Wewe mwandishi wetu taifa linakutegemea sana.
 
      Kulaumu wanafunzi nao sio zuri bali tuangalie zaidi kwa hawa waandishi uchwara wa magazeti yetu. Pamefikia mahali mtu uachoka hata kusoma gazeti husika kwa sababu mwandishi anaonekana anapendelea sana chama Fulani, au sehemu Fulani.
 
       Kwa mfano Tv zilizonyingi Tanzania kama vile Cloud Tv pia wanaangalia zaidi taarifa za majijini na mikoani. Hivi jiulize mara ngapi wanaripoti habari za vijijini. Hikinacho kinachangia kupoteza ubora wa tv zetu. Hata hizi tv media nyingine nazo ni vile vile wanaangalia zaidi Dar es salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya. Hivi kule Kigoma, Rukwa na Mikoa ya kusini mbona hawalipoti matukio kama kule mijini.
 
Ukweli ni kwamba vijijini watu walio wengi wanateseka; hawana huduma za jamii. Umeme kwao ni ndoto. Wanauona wakiwa mjini tu. Kwa msingi huo serikali inataka kufungia matumizi ya analogia bila kuangalia hawa wanakijiji ambao ni asilimia 80% ya Watanzania kweli wataweza kutumia digitari. Kama chakula tu ni shida je mtu alipie king’amuzi ataweza.
 
  Watanzania vijijini wamekata tamaa. Hawana wa kumweleza shida zao,sauti yao imefunikwa na waandishi uchwara ambao wamenunuliwa. Nakumbuka kwamba kipindi nasoma St. Augustine university of Tanzania 2011 katika kozi ya NEWS REPORTING chini ya Mwalimu wangu Madam Mushi,  alinifundisha namna ya kwenda kupata taarifa vijijini. Hapo ndipo aliponikalilisha kuwa maana ya Jonalist “Is the voice of the voiceless”. Hatu Lecture wangu Denis Mpagaze pia alikuwa analizungumzia sana neon hili.
 
Mimi naweza kujiita ni mwanafunzi wa Danis Mpagaze kwa kuwa amenifundisha. Huyu ni Msomi nan i Mwandishi ya jarida la “Physiognomy” pia ni Lecture st. Augistine University-Mwanza. Nilifurahia sana na Documentary zake ambapo alituonyesha mwanga juu ya Uandishi wa habari kwa kutuonyesha documentary ya “Mto tigite” namna watu walivyopalika ngozi na kugeuka kuwa rangi tofauti na walizonazo. 
 
Ukiangalia documentary hiyo utaona namna watanzania vijijini walivyokata tama. Hawana imani na hata viongozi wao kwa kukosa kuwatetea. Haya nimeyathibitisha baada ya kutembelea kijiji kimoja cha wilaya ya Newala kijiji cha Kitangali A, pia hata maeneo mengine ya kusini kama vile kijiji cha Mtama (Masasi), Namakambale B, Azimio,(Tunduru).
 
Hivyo somo langu la bure kwa waandishi wa habari ni kwamba mutembelee vijijini kuliko mijini.
 
   AUSI CHIWAMBO
TEKU UNIVERSITY
MBEYA
ausichiwambor@gmail.com
  

PICHA HALISI ZINAZOONESHA KUANZA KWA MAANDAMANO MTWARA SIKU YA KWANZA MWISHONI MWA MWAKA 2012 HADI SASA


 Mwanzoni mwa maandamano yaliyotokea Mtwara yalipambwa na Mabango ya aina hii. Hii ni siku ya kwanza ya maandamano.
Haya ni mabango mengine
 Hizi ni nyaraka za serikali zikiungua moto mjini Masasi Juzi



 Wauguzi wa Hospitali ya Ndanda wakisubili majeruhi

 Nyumba ya Mbunge wa Jimbo la Masasi,Mariam Masembe ambayo ilichomwa moto juzi na watu wenye hasira. Vitu mbalimbali viliharibiwa.Picha na Mpiga Picha Maalum-Mwananchi


HILI NI GARI LILILOCHOMWA MOTO IKISEMEKANA GARI HILO LILIKWENDA KUMFUATA BIBI (Upande wa kulia) ALIYESEMA KUWA WAKIAMISHA GESI KWENDA DAR ES SALAAM ITAGEUKA KUWA MAJI




 Hili ni gali la kubebea wagonjwa


Huu  ni siku ya kwanza maandamano yalianza kama inavyoonekana wakiwa na mabango yao yaliyoonesha madai yao




 Hii picha imechukuliwa kutoka Masasi








 Nyumba ya Mbunge wa Jimbo la Masasi,Mariam Masembe ambayo ilichomwa moto juzi na watu wenye hasira. Vitu mbalimbali viliharibiwa.Picha na Mpiga Picha Maalum-Mwananchi

 
 MJI WA MASASI KWA MBALI INAONEKANA NAMNA HII