Monday, January 28, 2013
Sunday, January 27, 2013
GESI YA MTWARA SASA YAONEKANA KAMA YALE YA LUDISM YALIYOTOKEA WIINGEREREZA
MAKALA NA CHIWAMBO
Kwa wale waliosoma kidato cha Tano na
cha sita Katika History 2 wanaweza kuthibitisha hicho kichwa cha habari.
Kipindi kile Nedy Ludy ilifanikiwa kuhalibu viwanda,Majumba na vingine vingi
kwa sababu eti ya ugunduzi wa viwanda ambapo nchi hiyo ilipitia kipindi cha
mageuzi kutoka kutegemea kilimo na kuingia mapinduzi ya viwanda. Wananchi wengi waliona hali hile ni tete
kwani hawakuweza kunufahika badala yake ni mwendo wa mateso tupu. Waliamua
kuchoma moto viwanda kimya kimya.
Kwa wale waliotembelea mikoa ya
kusini na wilaya zake ikiwemo Tunduru unaweza kusema kule sio Tanzania. Ni kama
nchi nyingine hivi. je tUnaweza kusema viongozi waliotokea kusini wana lahana?
Nakumbuka kama dishi langu halijakaa sawa basi hata Rais wa awamu ya Tatu ni wa
Masasi pale Lupaso. ameifanyia nini kusini kwa miaka yote aliyokuwepo kule?
je amechangia kuua bandari ya Mtwara?
waangalie viongozi wa sasa wanavyovutia gesi iende mtwara. sasa unaweza
kujiuliza kwamba hivi hawa viongozi ni wazalendo kweli? wanafanya nini huko
waliko? Kusini sasa hali imekuwa kama vita. vita vinavyojulikana vita vya gesi.
kila kona Tanzania wanazungumzia. sasa wavamia ofisi za umma, mahakama
zinachomwa moto, nyumba za wabunge zinateketezwa. hali ni tete. ni balaa.
wanakusini sasa wamechoka na mfumo uliopo?
Nasikia eti yule kiongozi mkuu wetu bwana
Mkubwa yupo nchi za wenzetu kujadili masula ya nchi za wengine na kusahau vita
baridi na ya moto iliyopo Tanzania. Hadi sasa hatujasikia mataifa makubwa
duniani wakisema chochote. naamini wanasubiri iongezeka nao walete mandege kama
yale ya mali ili kuwauwa wanakusini? Hapo ndipo watapoamini kwamba hali imekuwa
tete? kw nini tusubili waingereza au Ufaransa wakileta yale madege? mungu ibaliki
Tanzania.
Tusifike huko kwani mimi ni ni
Mwanakusini ambao sipo tayari kuona Tanzania ivamiwe na wakoloni wale
waliotutawala kama mali. Tujiulize nani wamesababisha haya. viongozi wetu
wanahusikaje juu ya hili? je kauli zao zinaleta tija kwa wanakusini? kwa upande
wangu naamini kauli za viongozi zinaweza kuleta vita au la kule kusini. hata
Nchini Mali ilianza wa Mvutano kati ya serikali na wananchi hasa waasi.
munakumbuka Misri ilikuwaje? ni jukumu lenu viongozi kuakikisha mapatano ya
maridhiano ni muhimu zaidi kuliko tunakoelekea.
Damu inayomwagika Kusini itadumu vizazi na
vizazi kama mgogoro hautatatuliwa. Kwa wale waliofuatilia uasi wa Nigeria, na
Sudani zote mbili wataona au waliona namna mafuta yalivyosababisha mtafaruku wa
nchi. Vita visivyo na mwisho. Sipendi kuona kusini yangu inagawanywa na kuwa
nchi nyingine? je itaitwaje? hili sio jambo jema. Hili jambo ni hatari.
Serikali jamani kwanini musichukue hatua ya amani kuliko vita iliyoko sasa. Kwa
kawaida umma unanguvu zaidi kuliko majeshi. Kwani ukiua wote kule kusini
wataishi nani? maana pakifikia mahali watu wapo tayari kufa kwa ajili ya
kutetea maslahi yao ona hapo pana jambo. njia pekee ni kukaa meza moja tu.
Hakuna jipya zaidi ya hilo. serikali
ikubali imeshindwa vinginevyo inaweza kutokea yale ya Ludism kule wingereza
miaka ya nyuma sana. Sasa serikali itumie Wanasaikolojia na wanasosholojia
ambao ni wataalamu wa jamii yao ili kutatua mgogoro huu. naamini viongozi wetu
watazuia ili ofisi na majumba yasichomwe moto kama Ludism.
HALI YA USAFIRI KUSINI
Hali ya usafiri kusini ni aibu.
Unaweza kusema haijawai kuwa na Rais kutoka kusini. Pia utajiuliza hawa
viongozi wa kule kusini wanafanya nini? Tuna wabunge wengi kweli kweli. Tunduru
peke yake inawabunge wawili akiwamo Injinia Makani na Mtutura. Je hawa watu wa
kusini Hasa Tunduru, Lindi na Mwata watafaidikaje na gesi iliyopo kusini?
Baraara tangia uhuru haijajengwa. Ni wimbo wa Taifa wakati wa kampeni. Kuna
kupindi walikuwa wanasafiri kwa kutumia meli lakini sasa bandari ilikufa
tunaendelea kupata tabu ya usafiri.
Ukiwauliza viongozi wetu wameifanyia
nini kusini watakujibu Tumejenga lile daraja kubwa nchini Tanzania ya Mkapa na
ile ya Msumbiji. Inawezekana hawa viongozi wanapita kwa anga tu. Uangalie chini
kuna nini unafili wataweza? Hali ni mbaya. Nawaomba mujalibu kutembelea kusini
ukizunguka kuanzia Namtumbo, shuka chini hadi Tunduru, kasha usikae pale
Tunduru teremuka hadi Masasi kasha pandisha hadi Hotel ya Nangurukuru Mkoani
Lindi.
Sasa ukianzia hapo Nangurukuru
kuelekea Daraja la Mkapa utaomba kama lingekuja wingi lizoe tope zote ziwekwe
pembeni ili mupite kwa amani na utulivu. Kulala nchiani ni kawaida kule kwetu.
Unapaswa uwe na Biskuti, ikiwezekana pika kabisa ugali au chukua unga na dagaa
wakati wa kusafiri ili usife njaa maana gari likiingia kwenye tope mbona
mutakesha.
Kwa kifupi hizo barabara nilizozitaja
ni mbaya mno. Tangu uhuru hazijajengwa. Na madai ya hawa wanakusini wanasema
iweje bomba la gesi lijengwe miezi 18 tu wakati barabara tangu uhuru bado?
PICHA ZINAZOONESHA MATUKIO YA MKOANI MTWARA
Kulia ni Rais Kikwete, na Kushoro ni Prof. Ibrahim Lipumba
Hizi ni nyaraka za serikali zikiungua moto mjini Masasi Juzi
Picha hii imewekwa inaonesha hali ya usafiri Mikoa ya Kusini. Walio wengi wanadai kuwa iweje bomba la gesi lijengwe miaka miwili wakati Barabara hii tangia uhuru wa Tanzania hadi leo haijawekwa lami?Nyumba ya Mbunge wa Jimbo la Masasi,Mariam Masembe ambayo ilichomwa moto juzi na watu wenye hasira. Vitu mbalimbali viliharibiwa.Picha na Mpiga Picha Maalum-Mwananchi
Hii ni katuni ya Masudi Kipanya ikionesha kuwa ukitembelea na kuamia mtwara unaweza kuwa tajiri eti kwa kuwa gesi inapatikana hapo.
Rais wa Awamu ya Tatu Mh. Benjamin W. Mkapa aliyetoa kauli kwamba wananchi wasitishe maandamano badala yake wakae meza moja ya mazungumzo ili kufikia muhafaka.
Friday, January 25, 2013
st.johns university walipoandamana Mjini Dodoma
Wanachuo
wakiwa kwenye maandamano kuelekea kwa mkuu wa mkoa hii ni kushinikiza
ulinzi kwa sababu ya matukio ambayo yanaendelea kutokea maana juzi
alifariki mwanachuo na usiku wa kuamkia leo wanachuo walivamiwa
vyumbani baada ya kukata nondo ya dirisha na kuiba Laptop tatu na simu
tano na baada ya kuchukua vitu hivyo waliacha wamewafanyia vitendo
vibaya na pia waliachwa wamefungwa ili wasipige kelele.
Kwa hali hii imesababisha maandamano ili kushinikiza ulinzi katika chuo cha St. John kilichopo Dodoma mjini.
Source:www.mjengwablog.co.tz
FUJO ZILIZOTOKEA MKOANI PWANI, KIBITI, RUFIJI ZITAFUTIWE UFUMBUZI
HAWA NI WANANCHI WA KIBITI JANA MCHANA WAKIVAMIA KITUO CHA POLISI KWA LENGO LA KUKICHOMA MOTO
Source: michuzi.blogsppot.com
Kwa sasa imeonekana ni hali ya kawaida watu kujichukulia uamuzi mikononi. Mwizi akikamatwa kuchomwa moto au kupiga hadi kuua. Maandamano kila kukicha Tanzania hadi inaleta shaka sana kuhusu uwajibikaji wa vionozi wetu. je wananchi wanasikilizwa kweli shida zao?
Source: michuzi.blogsppot.com
Kwa sasa imeonekana ni hali ya kawaida watu kujichukulia uamuzi mikononi. Mwizi akikamatwa kuchomwa moto au kupiga hadi kuua. Maandamano kila kukicha Tanzania hadi inaleta shaka sana kuhusu uwajibikaji wa vionozi wetu. je wananchi wanasikilizwa kweli shida zao?
Thursday, January 24, 2013
Wednesday, January 23, 2013
TANGAZO LA MMILIKI WA BLOG YA TEKU-BASO'BLOG
TANGAZO: KUANZIA LEO BLOG YA sociologist-baso.blogspot.com haitafanya kazi badala yake Munaombwa kuitumia hii blog ya Chiwambo.blogspot.com. bLOG YA MWANZO ITAKUWA KAMA SEHEMU YA HISTORIA. Ila kwa wasomaji wa maswali ya Baso munaruhusiwa ila hakutakuwa na habari mpya kama ilivyozoeleka na unaweza kupata maswali yako kupitia blog hii. kwa sasa tunapatikana kupitia
Chiwambo.blogspot.com
TUNAOMBA RADHI KWA USUMBUFU ULIOJITOKEZA
By Chiwambo
Chiwambo.blogspot.com
TUNAOMBA RADHI KWA USUMBUFU ULIOJITOKEZA
By Chiwambo
Subscribe to:
Posts (Atom)




















































