Sunday, January 27, 2013
Friday, January 25, 2013
st.johns university walipoandamana Mjini Dodoma
Wanachuo
wakiwa kwenye maandamano kuelekea kwa mkuu wa mkoa hii ni kushinikiza
ulinzi kwa sababu ya matukio ambayo yanaendelea kutokea maana juzi
alifariki mwanachuo na usiku wa kuamkia leo wanachuo walivamiwa
vyumbani baada ya kukata nondo ya dirisha na kuiba Laptop tatu na simu
tano na baada ya kuchukua vitu hivyo waliacha wamewafanyia vitendo
vibaya na pia waliachwa wamefungwa ili wasipige kelele.
Kwa hali hii imesababisha maandamano ili kushinikiza ulinzi katika chuo cha St. John kilichopo Dodoma mjini.
Source:www.mjengwablog.co.tz
FUJO ZILIZOTOKEA MKOANI PWANI, KIBITI, RUFIJI ZITAFUTIWE UFUMBUZI
HAWA NI WANANCHI WA KIBITI JANA MCHANA WAKIVAMIA KITUO CHA POLISI KWA LENGO LA KUKICHOMA MOTO
Source: michuzi.blogsppot.com
Kwa sasa imeonekana ni hali ya kawaida watu kujichukulia uamuzi mikononi. Mwizi akikamatwa kuchomwa moto au kupiga hadi kuua. Maandamano kila kukicha Tanzania hadi inaleta shaka sana kuhusu uwajibikaji wa vionozi wetu. je wananchi wanasikilizwa kweli shida zao?
Source: michuzi.blogsppot.com
Kwa sasa imeonekana ni hali ya kawaida watu kujichukulia uamuzi mikononi. Mwizi akikamatwa kuchomwa moto au kupiga hadi kuua. Maandamano kila kukicha Tanzania hadi inaleta shaka sana kuhusu uwajibikaji wa vionozi wetu. je wananchi wanasikilizwa kweli shida zao?
Thursday, January 24, 2013
Wednesday, January 23, 2013
TANGAZO LA MMILIKI WA BLOG YA TEKU-BASO'BLOG
TANGAZO: KUANZIA LEO BLOG YA sociologist-baso.blogspot.com haitafanya kazi badala yake Munaombwa kuitumia hii blog ya Chiwambo.blogspot.com. bLOG YA MWANZO ITAKUWA KAMA SEHEMU YA HISTORIA. Ila kwa wasomaji wa maswali ya Baso munaruhusiwa ila hakutakuwa na habari mpya kama ilivyozoeleka na unaweza kupata maswali yako kupitia blog hii. kwa sasa tunapatikana kupitia
Chiwambo.blogspot.com
TUNAOMBA RADHI KWA USUMBUFU ULIOJITOKEZA
By Chiwambo
Chiwambo.blogspot.com
TUNAOMBA RADHI KWA USUMBUFU ULIOJITOKEZA
By Chiwambo
VITUKO VYA WAKUBWA HII NDIYO MOJA YA HOTUBA MBAYA ZA P. w. BOTHA
Ć Akiri kuwaua kwa weusi kwa sumu
Ć Mweusi ni malighafi ya mweupe
HABARI KAMILI
Hii ni hotuba ya aliyekuwa rais wa Afrika Kusini, p. w. Botha
alipohutubia baraza lake la mawaziri wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi
nchini humo. Katika hotuba hiyo iliyochapishwa na gazeti la “SUNDAY TIMES” la nchini humo toleo la
Agosti 18, 1985, Botha anapojigamba eti ardhi hiyo ni mali yao
na haipaswi kuingiliwa.
Ikumbukwe kuwa
katika utawala huo, mtu mweusi aliteswa na kunyimwa haki zake za msingi na
alifanywa kuwa kiumbe dhaifu kisichostahili kuishi kwa raha katika nchi hiyo.
“Kaka zangu na
dada zangu, Pretoria
imetengenezwa na watu weupe kwa ajili ya watu weupe na hatuna haja ya
kuuthibitisha umma au mtu mweusi kuwa sisi ni watu bora, tumekuwa
tukiwaambia watu weusi jambo hili kwa
njia elfu.
Africa kusini
ya leo haikutengenezwa katika mawazo ya kawaida, tumeitengeneza kwa kutumia
akili nyingi, jasho na damu. Mnaposema kuwa tunawabagua weusi sielewi.
Hivi ni
Afrikaners ndio waliojaribu kusitisha kizazi cha Aborigines wa Australia?
Je ni Africaners waliotenga na kuwanyanyasa watu weusi Marekani kasikazini kwa
kuwaita niggaz?
Je, ni
Africaners waliowatenga na kuwanyanyasa watu weusi huko England kwa kuwatungia sheria ya
kuwakandamiza? Canada, Ufarasa , Russia, na Japan nao wana njia zao za
kibaguzi. Hivi kwanini hasa kuna kelele nyingi dhidi yetu? Huu ni uendawazimu!
Kwanini wanatukaba koo kiasi hiki? Hawatundendei haki hata kidogo.
Nataka
kuwaeleza kuwa hakuna kibaya tunachokitenda hapa ambacho hao wanaojihita wako
katika dunia ya ustaarabu wameacha kufanya. Sisi ni watu wema tusio na hatia na
ambao tumeweka wazi mfumo wa maisha ya tunayotaka tuishi kama
watu weupe.
Sisi sio
wanafiki kama wazungu wenzetu wafanyavyo
kwamba wanapenda watu weusi.
Ukweli kuwa
weusi wanaofanana na binadamu na kutenda mambo kama
binadamu hayawahalalishi kuwa wao ni watu wenye akili timamu au binadamu
aliyetimia. Kanunguyeye si nungunungu
na mijusi hawawezi kuwa mamba kwa sababu eti wanafanana.
Kama mungu alitaka tufannane na
weusi angetufanya wote tuwe na rangi moja na fikra sawa. Lakini alituumba
tofauti, weupe, weusi, wanjano, watawala na watawaliwa. Katika upeo sisi ni
bora kuliko weusi na hilo
halina ubishi kwani limejidhihilisha kwa miaka mingi iliyopita.
Naamini kuwa Africaner
ni mtu safi, mwenye hofu na mungu. Ni mtu mbaye ameonyesha kwa vitendo njia
sahihi ya utu. Hata hivyo inafurahisha kuona Ulaya, America, Canada, Australia na wengine wengi wako nyuma yetu
achilia mbali maeneo yao.
Kuhusu
uhusiano wa kidemokrasia, sote tunafahamu lugha inayotakiwa kutumika. Na kwa
ushaidi ulio wazi hivi kuna mtu hapa asiyejua kuwa nchi nyingi za Ulaya zina
tamani kuwekeza Afika kusini.
Nani
anayenunua dhahabu yetu, nani anayenunua almasi yetu? Nani anafanya bihashara
nasi? Nani anatusaidia katika kuendesha siraha za nyukilia? Ukweli ni kwamba
sisi ni watu wao na wao ni watu wetu. Hii ni siri kubwa. Nguvu ya uchumi wetu
inajengwa kwa kiasi kikubwa na America, Uingereza, na Ujerumani. Ni jambo kubwa
sana hili na kwa maana hiyo, mweusi ni malighafi kwa mweupe.
Hivyo basi,
kaka na dada zangu hebu tuungane kumpiga vita huyu mweusi. Napiga mbiu kwa
Africaners wote kujitokeza kwa hali na mali kupigana vita hii. Kwa hakika
mungu hawezi kuwatupa watu wake ambao ni sisi. Hadi sasa imeonekana kwa vitendo
kuwa weusi hawawezi kujitawala. Wape bunduki kama
hawataanza kuuana.
Hawana lolote
jema isipokuwa mashujaa wa kupiga kelele, kucheza ngoma, kuoa wanawake
wengi na kupenda sana
ngono. Hebu sasa tukubali kuwa mtu mweusi ni alama ya umskini, udumavu
wa akili, uvivu na aliyekosa ushindani. Hivi hapo je, si kweli
kwamba mtu mweupe aliumbwa ili kumtawala mtu mweusi? Hivi utajisikiaje
unaamka asubuhi unakuta Kaff*ir amekaria kiti cha utawala? Hivi unajua
kitakachotokea kwa wanawake wetu? Hivi kuna mtu anaweza kwamba mweusi
ataitawala nchi hii.
Kwa hiyo tuna
sababu nzuri ya kuwapeleka akina Mandela jela waozee huko na katika hili
nadhani upo umuhimu wa kupewa pongezi kwani tungekuwa na uwezo wa kuwaangamiza
lakini sasa wanaishi.
Napenda
kuwatangazia mikakati mipya ya kuwaangamiza hawa weusi. Tutumie sumu
kuwamaliza.
Kamwe
tusirushusi idadi ya watu weusi iendeleekukua vinginevyo tutakwisha. Tayari
nimeshawaleta wanasayansi ambao wamekuja na sehemu kubwa ya mzigo wa sumu na
ninawasaka watafiti wengine zaidi waangalie sehemu murua za kuitumia sumu hiyo
kwa lengo la kuwaangamiza weusi.
Sehemu nzuri
za kuwaangamiza kwa sumu ni hospitali na pia katika usambazaji wa chakula
inaweza kutumika. Tumetengeneza sumu inayoua taratibu na kupunguza uwezo wa
uzazi. Lakini hofu yetu ni kwamba itakuwaje kama sumu hiyo itaangukia mikono yao.
Hata hivi
tunafanya kila yuwezalo kuhakikisha kuwa sumu hiyo inabaki katika himaya yetu.
Pili, watu weusi wanapenda sana
pesa kwa hiyo tunaweza kuwatenga kwa njia hiyo. Wataalamu wetu wanalifanyia
kazi suala hilo
ili mtu mweusi amchukie mweusi mwenzake.
Hawana upeo wa
kufikiri na huyo ndiye kiumbe dhaifu kisicho na akili ya kuona mbali.
Kuna umuhimu
mkubwa wa kupanga mambo hayo yaendelee kwa muda mrefu ili wasibaini kuwaua. Kwa
kawaida mtu mweusi hapangi mikakati inayozidi mwaka mmoja. Na hapa napenda
niwaombe kina mama wa ki Afrikaner wazae kwa fujo kuongeza idadi.
Litakuwa jambo
la maana pia kama kutatengwa vituo maalumu
ambako vijana wa kike na kiume watakaa na serikali kuwawezesha ili wazae kwa
idadi kubwa iwezekanavyo ili kuongeza idadi yetu. Wakati hilo likiendelea,
lazima tuwabane watu weusi waachane na wake zao.
Ninayo kamati
inayoratibu na inayoangalia njia nzuri ya kuwafanya watu hawa wachukiane na
wauane wenyewe kwa wenyewe. Adhabu kwa mweusi aliyemuua mweusi iwe ndogo ili
kuwapa hamasa ya kuendelea na mauaji.
Wanasayansi
wangu wameshauri pia kuna ulazima wa kuwawekea sumu kwenye pombe, sumu ambayo
itakuwa inawaua taratibu na kumaliza uwezo wa kuzaa pia. Njia kama hii na
nyingine zifananazo na hii itawarahisisha kuwapunguza idadi.
Rekodi
zinaonyesha pia kuwa mtu mweusi anapenda sana
mwanamke mweupe. Hii ni nafasi nzuri kwetu. Wanawake wetu warembo wanaotumika
katika mbinu za kuwaangamiza wapinzani wetu watatumika kuwaua hao wanaopinga
ubaguzi wa rangi.
Hili jeshi
letu la mwituni la mapenzi huku tukiwa na jeshi kama hilo kwa upande wa wanaume ambao watatafuta
wanawake weusi. Pia serikali imeagiza Malaya kutoka Marekani na ulaya kwa ajili
ya kukidhi haja yao.
Ombi langu la
mwisho ni kwamba wajawazito wanapozaa hospitalini, watoto lazima wauwawe pindi
tu wanapotoka tumboni. Hatuwalipi wale wauguzi kwa ajili ya kutuletea watoto
weusi katika dunia hii bali kuwaangamiza.
Serikali yangu
imetenga fungu maalumu la pesa kwa ajili ya kufanikisha mpango huo. Pesa
inafanya lolote na kwa vile tunazo tuzitumie ipasavyo.
Kwa muda huu
ndugu zangu weupe, msiyaweke moyoni wala msione aibu kuitwa wabaguzi na wala
sijali mhandisi wa Mfalme wa ubaguzi.
Siwezi kugeuka
nyani eti kwa sababu mtu kaniita nyani. Nitabaki kuwa nyota inayong’aa ….mtukufu
Botha.
Leo naondoa
mawingu; kesho nitajalibu mlima”.
HABARI HII ILIWAI KUTOLEWA NA GAZETI LA RAI, OKTOBA
19-25, 2006. UK.
17.
IMELETWA KWENU NA CHIWAMBO AUSI R (TEOFILO KISANJI
UNIVERSITY-TEKU, BA SOCIOLOGY AND SOCIAL WORK) 18, March, 2012.
MAWASILIANO:-
MCHAKATO WA UCHAGUZI 2015 USIWE MBEBWE KIASI CHA KUSHINDWA KUFANYA KAZI ZENYE MASLAHI KWA UMMA.
MAKALA
YA CHIWAMBO
Katika
Makala ya Chiwambo leo inazungumzia zaidi juu ya utendaji kazi wa watumishi wa
umma, wanasiasa, na namna vyombo vya habari vinavyotumika visivyo ili kutetea
maslahi ya wachache. Hili linajitokeza kila uchaguzi hasa kuanzia Mwaka 2005,
2010, na inavyoonekana 2015 nayo ipo vivyo hivyo. Wananchi hugawanywa vipande
vipande katika makundi mbalimbali huku makundi hayo yote husimamia maslahi ya
kundi husika.
Katika
nchi yetu kwa bahati mzuri hatuna Ukabila kama kule Nchini Kenya ambapo nchi
hiyo katika kila chaguzi utawala suala la ukabila. Lakini huku kwetu Tanzania
makundi ndiyo tatizo kubwa ambayo lengo kuu ni kushika hatamu ya kuongoza nchi.
Wakati huu karibu kila chama kinazunguzia zaidi kuhusu uchaguzi 2015. Nani
atakuwa Rais ajaye sio kwa chama tawala tu bali hata chama kikuu cha upinzani
nchini Tanzania chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Viongozi
wetu inavyoelekea hasa wale wanaohitaji Urais 2015 wameanza kujisahau.
Wamesahau wapiga kura wao na kuzungumzia zaidi suala la uchaguzi mwaka 2015.
Swali la kujiuliza ni kwamba je wananchi munawatumikia kweli? Panafikia mahali
mtu unapata mashaka juu ya utendaji wao wa kazi. Magazeti wameyatawala kwa
kuandika zaidi habari zao za uchaguzi 2015 na nani atakuwa mbabe katika
uchaguzi huo.
Ukweli
ni kwamba wananchi hatupendi kuona nchi inalumbana juu ya nani atakuwa Rais
ajaye Mwaka 2015 badala yake muwatendee haki hawa Wananchi waliowafanya muingie
hapo Mjengoni. Katika tafsiri ya mwandishi wa habari inasema kwamba ni “The
voice of the voiceless” au Watch dog of the Government”. Hii inamaana kwamba
mwandishi wa habari ni mtu anayewasemea wananchi ambao hawana pa kusemea.
Wananchi
walio wengi Tanzania hasa wale wa vijijini hawana wasemaji licha ya kuwa na
wabunge ambao huwakilisha wilaya hizo na wanaonekana kwao uchaguzi hadi
uchaguzi. Sasa huyu mwandishi anatakiwa kuwa msemaji na mfichuaji wa maovu na
mazuri yote yanayofanywa na Wananchi, kikundi cha watu, pamoja na kuikosoa
serikali iliyopo madarakani kwa kuonesha kwamba hapa bwana mkuu hujafanya
vizuri na hapa umefanya vizuri.
Lakini
kwa sasa waandishi wa habari wetu wamewageuka wananchi. Na wamebadilisha maana
halisi ya Mwandishi wa habari ambapo wameifanya kuwa “Journalist is a person
who deal with the viceveser of the voice of the voiceless”. Inamaanisha
wanajadili zaidi suala la kwamba mwandishi wa habari na kazi yake ni kuweka
kinyume cha tafsili halisi ya kuwasemea wale wasio na sauti na badala yake
kusimama upande Fulani wa kundi analoliamini yeye ili kutetea maslahi ya mtu
binafsi kunyakua kiti cha uraisi 2015.
Hili
ni balaa nan i janga kwa taifa la leo na kesho. Matokeo ya vyombo vya habari
kuwa wapiga debe kwa viongozi wa aina Fulani ni bomu ambalo litakuja
kuwalipukia wenyewe hapo baadaye. Waandishi wenzangu mulio wengi mumekuwa
ndumila kuwili na watawaliwa wa fikra zenu. Inaonesha namna gani elimu
muliyonaye haisaidii Taifa letu badala yake unafuata matakwa ya wachahce wenye
fedha na wanasiasa.
Wewe
mtaaluma wa masuala ya uandishi wa Habari, iweje ufundishwe nini cha kuandika
na mtu ambaye hata taaluma yenyewe ya uandishi wa habari hana na hajawai
kuisoma. Na wengine hata tafsiri ya neon lenyewe Journalism halijui. Sasa
inakuwaje kikundi hiki cha watu kitawale sanaa ya uandishi wa habari. Kwa
msingi huu mutaendelea kununuliwa siku hadi siku, maisha hadi kiama.
Kwa
mabo kama haya munakaa vikao na kusema hatuna uhuru wa Habari nchi. Kama
unakubali kununuliwa na ukanunulika unadhani uhuru utakuwepo kweli? Tumezichoka
habari za kusikia hatuna uhuru wa vyombo vya habari nchini huku ninyi wenyewe
mkiwa mstari wa mbele kuwasaliti wananchi. Munategemea nini? Fedha za leo
zitawatawala ninyi wenyewe hapo kesho. Mara nyingi ninyi munakuwa mstari wa
mbele baadaye kusema kiongozi huyu ni mbaya, hafai na kumwangika vichwa vya
habari vya kumkejeli baada ya kupata madaraka.
Kama
mimi ningekuwa ndiye Rais wan chi hii ningemshinikiza waziri anayehusika na
masuala ya vyombo vya habari andaye mswada mpya zaidi wa kuvinyonga vyombo vya
habari ili wakose uhuru zaidi. Kwani kiasi cha uhuru uliopo wameshindwa
kukitumia. Mambo ya kuzungumzia yapo mengi ten asana kila kona. Hivi swali lenu
ni hili, je umewai kutembelea vijijini kule na kuona nyakati za mvua
wanaishije? Wanakula nini? Adha gani wanayokutana nayo?
Hivi
ni kweli vitu vya kuzungumzia kwenye vyombo vyenu vya habari (Media) vimekwisha
kabaisa? Au munataka wananchi waandamane pamoja na kuwalamba mboko ili muandike
habari zao na muwatumikie vyema? Hivi munadhani hiyo elimu yenu bila wananchi
mungeza kuipa? Utitili wa magazeti sasa unathibitisha usemi wangu kuwa
wanaripoti habari mbalimbali ili kulinda maslahi ya watu wachache badala ya
umma.
Mutazame
maeneo ya Ngorongoro watu wanavyoteseka na Njaa, Tunduru hadi leo korosho
hazinunuliwi na wananchi hawajui lini zitanunuliwa huku watu binafsi wakinunua
kangomba za korosho kwa bei ya shilingi 500 kwa kilo. Ninyi waandishi muko
wapi? Kwanini musiripoti habari kama hizi zinazooneka ni za ulanguzi. Maisha ya
wanatunduru msimu huu wa mvua yanakuwa hali tete? Chakula chao kikuu ni ugali
wa muhogo wa wa kuloweka kwenye maji na kukausha ambao hauna virutubisho
mwilini. Na mvua zinapochanganya watu hushindwa kula na wengine hushindia miogo
ya kupika au uji.
Nakumbuka
mwalimu wangu Mama Mushi wa somo la NEWS REPORTING Chuo kikuu MT. Augustine
Mwanza alinifundisha kwamba Greater The Name Greater The News, And Greater the
Event Greater the New”. Ila hili neon lisitumike visivyo ili kuweza kuwanyima
na kuwafunga midomo wananchi. Pamefikia mahari mtu unahamua kuaghahilisha
kununua Gazeti Fulani kisa linapendelea sana upande Fulani wa chama au kundi la
watu wataka Madaraka badala ya kuwazungumzia wananchi na shida zao zinazozidi
kuongezeka siku hadi siku na zitazidi kuongezeka siku hadi siku.
Inawezeka
waandishi wetu wanafanya haya kwa sababu vyombo vya habari vilivyo vingi nchini
vinamilikiwa na wenye fedha na wanasiasa hivyo wanalazimika kuandika au
kuripoti kile basi wao anachohitaji. kwa mfano kama mimi ningekuwa namiliki
vyombo vya habari basi nikilala nikiamka natoa amri kesho magazeti au media
zangu zote munilipoti kwamba nimetoa msaada huu ili nionekana nafanya mema kwa
wananchi kumbe moyoni ni danganya toto.
HivyoViongozi
wetu tunawaomba muwatumikie wananchi vilivyo ili kuweza kuleta ufanisi zaidi na
kupunguza lindi la umaskini linaloikabili nchi yetu. Masuala ya uchaguzi 2015
yasiwe ndio kikwazo kwa maendeleo ya nchi yetu Tanzania. CCM na CDM na vyama
vingine muwatumikie wananchi kwanza na sio kulumbana juu ya uchaguzi 2015 na
badala yake mufanye kama mulivoagizwa na wananchi. Je ukifika mwaka 2015
utawaeleza nini hao wananchi waliokuchagua kuwa kiongozi wao?
Makala
hii Imeandikwa na Chiwambo Ausi
TEOFILO
KISANJI UNIVERSITY (TEKU)
E-Mail:
Ausichiwambor@hotmail.com
Subscribe to:
Posts (Atom)







































