Wednesday, January 23, 2013

VITUKO VYA WAKUBWA HII NDIYO MOJA YA HOTUBA MBAYA ZA P. w. BOTHA



Ø Akiri kuwaua kwa weusi kwa sumu
Ø Mweusi ni malighafi ya mweupe

HABARI KAMILI
Hii ni hotuba ya aliyekuwa rais wa Afrika Kusini, p. w. Botha alipohutubia baraza lake la mawaziri wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi nchini humo. Katika hotuba hiyo iliyochapishwa na gazeti la “SUNDAY TIMES” la nchini humo toleo la Agosti 18, 1985, Botha anapojigamba eti ardhi hiyo ni mali yao na haipaswi kuingiliwa.

Ikumbukwe kuwa katika utawala huo, mtu mweusi aliteswa na kunyimwa haki zake za msingi na alifanywa kuwa kiumbe dhaifu kisichostahili kuishi kwa raha katika nchi hiyo.


“Kaka zangu na dada zangu, Pretoria imetengenezwa na watu weupe kwa ajili ya watu weupe na hatuna haja ya kuuthibitisha umma au mtu mweusi kuwa sisi ni watu bora, tumekuwa tukiwaambia  watu weusi jambo hili kwa njia elfu.

Africa kusini ya leo haikutengenezwa katika mawazo ya kawaida, tumeitengeneza kwa kutumia akili nyingi, jasho na damu. Mnaposema kuwa tunawabagua weusi sielewi.

Hivi ni Afrikaners ndio waliojaribu kusitisha kizazi cha Aborigines wa Australia? Je ni Africaners waliotenga na kuwanyanyasa watu weusi Marekani kasikazini kwa kuwaita niggaz?

Je, ni Africaners waliowatenga na kuwanyanyasa watu weusi huko England kwa kuwatungia sheria ya kuwakandamiza? Canada, Ufarasa , Russia, na Japan nao wana njia zao za kibaguzi. Hivi kwanini hasa kuna kelele nyingi dhidi yetu? Huu ni uendawazimu! Kwanini wanatukaba koo kiasi hiki? Hawatundendei haki hata kidogo.

Nataka kuwaeleza kuwa hakuna kibaya tunachokitenda hapa ambacho hao wanaojihita wako katika dunia ya ustaarabu wameacha kufanya. Sisi ni watu wema tusio na hatia na ambao tumeweka wazi mfumo wa maisha ya tunayotaka tuishi kama watu weupe.

Sisi sio wanafiki kama wazungu wenzetu wafanyavyo kwamba wanapenda watu weusi.

Ukweli kuwa weusi wanaofanana na binadamu na kutenda mambo kama binadamu hayawahalalishi kuwa wao ni watu wenye akili timamu au binadamu aliyetimia. Kanunguyeye si nungunungu na mijusi hawawezi kuwa mamba kwa sababu eti wanafanana.

Kama mungu alitaka tufannane na weusi angetufanya wote tuwe na rangi moja na fikra sawa. Lakini alituumba tofauti, weupe, weusi, wanjano, watawala na watawaliwa. Katika upeo sisi ni bora kuliko weusi na hilo halina ubishi kwani limejidhihilisha kwa miaka mingi iliyopita.

Naamini kuwa Africaner ni mtu safi, mwenye hofu na mungu. Ni mtu mbaye ameonyesha kwa vitendo njia sahihi ya utu. Hata hivyo inafurahisha kuona Ulaya, America, Canada, Australia na wengine wengi wako nyuma yetu achilia mbali maeneo yao.

Kuhusu uhusiano wa kidemokrasia, sote tunafahamu lugha inayotakiwa kutumika. Na kwa ushaidi ulio wazi hivi kuna mtu hapa asiyejua kuwa nchi nyingi za Ulaya zina tamani kuwekeza Afika kusini.

Nani anayenunua dhahabu yetu, nani anayenunua almasi yetu? Nani anafanya bihashara nasi? Nani anatusaidia katika kuendesha siraha za nyukilia? Ukweli ni kwamba sisi ni watu wao na wao ni watu wetu. Hii ni siri kubwa. Nguvu ya uchumi wetu inajengwa kwa kiasi kikubwa na America, Uingereza, na Ujerumani. Ni jambo kubwa sana hili na kwa maana hiyo, mweusi ni malighafi kwa mweupe.

Hivyo basi, kaka na dada zangu hebu tuungane kumpiga vita huyu mweusi. Napiga mbiu kwa Africaners wote kujitokeza kwa hali na mali kupigana vita hii. Kwa hakika mungu hawezi kuwatupa watu wake ambao ni sisi. Hadi sasa imeonekana kwa vitendo kuwa weusi hawawezi kujitawala. Wape bunduki kama hawataanza kuuana.

Hawana lolote jema isipokuwa mashujaa wa kupiga kelele, kucheza ngoma, kuoa wanawake wengi na kupenda sana ngono. Hebu sasa tukubali kuwa mtu mweusi ni alama ya umskini, udumavu wa akili, uvivu na aliyekosa ushindani. Hivi hapo je, si kweli kwamba mtu mweupe aliumbwa ili kumtawala mtu mweusi? Hivi utajisikiaje unaamka asubuhi unakuta Kaff*ir amekaria kiti cha utawala? Hivi unajua kitakachotokea kwa wanawake wetu? Hivi kuna mtu anaweza kwamba mweusi ataitawala nchi hii.
                         
Kwa hiyo tuna sababu nzuri ya kuwapeleka akina Mandela jela waozee huko na katika hili nadhani upo umuhimu wa kupewa pongezi kwani tungekuwa na uwezo wa kuwaangamiza lakini sasa wanaishi.

Napenda kuwatangazia mikakati mipya ya kuwaangamiza hawa weusi. Tutumie sumu kuwamaliza.

Kamwe tusirushusi idadi ya watu weusi iendeleekukua vinginevyo tutakwisha. Tayari nimeshawaleta wanasayansi ambao wamekuja na sehemu kubwa ya mzigo wa sumu na ninawasaka watafiti wengine zaidi waangalie sehemu murua za kuitumia sumu hiyo kwa lengo la kuwaangamiza weusi.

Sehemu nzuri za kuwaangamiza kwa sumu ni hospitali na pia katika usambazaji wa chakula inaweza kutumika. Tumetengeneza sumu inayoua taratibu na kupunguza uwezo wa uzazi. Lakini hofu yetu ni kwamba itakuwaje kama sumu hiyo itaangukia mikono yao.

Hata hivi tunafanya kila yuwezalo kuhakikisha kuwa sumu hiyo inabaki katika himaya yetu. Pili, watu weusi wanapenda sana pesa kwa hiyo tunaweza kuwatenga kwa njia hiyo. Wataalamu wetu wanalifanyia kazi suala hilo ili mtu mweusi amchukie mweusi mwenzake.

Hawana upeo wa kufikiri na huyo ndiye kiumbe dhaifu kisicho na akili ya kuona mbali.

Kuna umuhimu mkubwa wa kupanga mambo hayo yaendelee kwa muda mrefu ili wasibaini kuwaua. Kwa kawaida mtu mweusi hapangi mikakati inayozidi mwaka mmoja. Na hapa napenda niwaombe kina mama wa ki Afrikaner wazae kwa fujo kuongeza idadi.

Litakuwa jambo la maana pia kama kutatengwa vituo maalumu ambako vijana wa kike na kiume watakaa na serikali kuwawezesha ili wazae kwa idadi kubwa iwezekanavyo ili kuongeza idadi yetu. Wakati hilo likiendelea, lazima tuwabane watu weusi waachane na wake zao.

Ninayo kamati inayoratibu na inayoangalia njia nzuri ya kuwafanya watu hawa wachukiane na wauane wenyewe kwa wenyewe. Adhabu kwa mweusi aliyemuua mweusi iwe ndogo ili kuwapa hamasa ya kuendelea na mauaji.

Wanasayansi wangu wameshauri pia kuna ulazima wa kuwawekea sumu kwenye pombe, sumu ambayo itakuwa inawaua taratibu na kumaliza uwezo wa kuzaa pia. Njia kama hii na nyingine zifananazo na hii itawarahisisha kuwapunguza idadi.

Rekodi zinaonyesha pia kuwa mtu mweusi anapenda sana mwanamke mweupe. Hii ni nafasi nzuri kwetu. Wanawake wetu warembo wanaotumika katika mbinu za kuwaangamiza wapinzani wetu watatumika kuwaua hao wanaopinga ubaguzi wa rangi.

Hili jeshi letu la mwituni la mapenzi huku tukiwa na jeshi kama hilo kwa upande wa wanaume ambao watatafuta wanawake weusi. Pia serikali imeagiza Malaya kutoka Marekani na ulaya kwa ajili ya kukidhi haja yao.

Ombi langu la mwisho ni kwamba wajawazito wanapozaa hospitalini, watoto lazima wauwawe pindi tu wanapotoka tumboni. Hatuwalipi wale wauguzi kwa ajili ya kutuletea watoto weusi katika dunia hii bali kuwaangamiza.

Serikali yangu imetenga fungu maalumu la pesa kwa ajili ya kufanikisha mpango huo. Pesa inafanya lolote na kwa vile tunazo tuzitumie ipasavyo.

Kwa muda huu ndugu zangu weupe, msiyaweke moyoni wala msione aibu kuitwa wabaguzi na wala sijali mhandisi wa Mfalme wa ubaguzi.

Siwezi kugeuka nyani eti kwa sababu mtu kaniita nyani. Nitabaki kuwa nyota inayong’aa ….mtukufu Botha.

Leo naondoa mawingu; kesho nitajalibu mlima”.

HABARI HII ILIWAI KUTOLEWA NA GAZETI LA RAI, OKTOBA 19-25, 2006. UK. 17.

IMELETWA KWENU NA CHIWAMBO AUSI R (TEOFILO KISANJI UNIVERSITY-TEKU, BA SOCIOLOGY AND SOCIAL WORK) 18, March, 2012.

MAWASILIANO:-



MCHAKATO WA UCHAGUZI 2015 USIWE MBEBWE KIASI CHA KUSHINDWA KUFANYA KAZI ZENYE MASLAHI KWA UMMA.



 MAKALA YA CHIWAMBO
Katika Makala ya Chiwambo leo inazungumzia zaidi juu ya utendaji kazi wa watumishi wa umma, wanasiasa, na namna vyombo vya habari vinavyotumika visivyo ili kutetea maslahi ya wachache. Hili linajitokeza kila uchaguzi hasa kuanzia Mwaka 2005, 2010, na inavyoonekana 2015 nayo ipo vivyo hivyo. Wananchi hugawanywa vipande vipande katika makundi mbalimbali huku makundi hayo yote husimamia maslahi ya kundi husika.

Katika nchi yetu kwa bahati mzuri hatuna Ukabila kama kule Nchini Kenya ambapo nchi hiyo katika kila chaguzi utawala suala la ukabila. Lakini huku kwetu Tanzania makundi ndiyo tatizo kubwa ambayo lengo kuu ni kushika hatamu ya kuongoza nchi. Wakati huu karibu kila chama kinazunguzia zaidi kuhusu uchaguzi 2015. Nani atakuwa Rais ajaye sio kwa chama tawala tu bali hata chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Viongozi wetu inavyoelekea hasa wale wanaohitaji Urais 2015 wameanza kujisahau. Wamesahau wapiga kura wao na kuzungumzia zaidi suala la uchaguzi mwaka 2015. Swali la kujiuliza ni kwamba je wananchi munawatumikia kweli? Panafikia mahali mtu unapata mashaka juu ya utendaji wao wa kazi. Magazeti wameyatawala kwa kuandika zaidi habari zao za uchaguzi 2015 na nani atakuwa mbabe katika uchaguzi huo.

Ukweli ni kwamba wananchi hatupendi kuona nchi inalumbana juu ya nani atakuwa Rais ajaye Mwaka 2015 badala yake muwatendee haki hawa Wananchi waliowafanya muingie hapo Mjengoni. Katika tafsiri ya mwandishi wa habari inasema kwamba ni “The voice of the voiceless” au Watch dog of the Government”. Hii inamaana kwamba mwandishi wa habari ni mtu anayewasemea wananchi ambao hawana pa kusemea.

Wananchi walio wengi Tanzania hasa wale wa vijijini hawana wasemaji licha ya kuwa na wabunge ambao huwakilisha wilaya hizo na wanaonekana kwao uchaguzi hadi uchaguzi. Sasa huyu mwandishi anatakiwa kuwa msemaji na mfichuaji wa maovu na mazuri yote yanayofanywa na Wananchi, kikundi cha watu, pamoja na kuikosoa serikali iliyopo madarakani kwa kuonesha kwamba hapa bwana mkuu hujafanya vizuri na hapa umefanya vizuri.

Lakini kwa sasa waandishi wa habari wetu wamewageuka wananchi. Na wamebadilisha maana halisi ya Mwandishi wa habari ambapo wameifanya kuwa “Journalist is a person who deal with the viceveser of the voice of the voiceless”. Inamaanisha wanajadili zaidi suala la kwamba mwandishi wa habari na kazi yake ni kuweka kinyume cha tafsili halisi ya kuwasemea wale wasio na sauti na badala yake kusimama upande Fulani wa kundi analoliamini yeye ili kutetea maslahi ya mtu binafsi kunyakua kiti cha uraisi 2015.

Hili ni balaa nan i janga kwa taifa la leo na kesho. Matokeo ya vyombo vya habari kuwa wapiga debe kwa viongozi wa aina Fulani ni bomu ambalo litakuja kuwalipukia wenyewe hapo baadaye. Waandishi wenzangu mulio wengi mumekuwa ndumila kuwili na watawaliwa wa fikra zenu. Inaonesha namna gani elimu muliyonaye haisaidii Taifa letu badala yake unafuata matakwa ya wachahce wenye fedha na wanasiasa.

Wewe mtaaluma wa masuala ya uandishi wa Habari, iweje ufundishwe nini cha kuandika na mtu ambaye hata taaluma yenyewe ya uandishi wa habari hana na hajawai kuisoma. Na wengine hata tafsiri ya neon lenyewe Journalism halijui. Sasa inakuwaje kikundi hiki cha watu kitawale sanaa ya uandishi wa habari. Kwa msingi huu mutaendelea kununuliwa siku hadi siku, maisha hadi kiama. 

Kwa mabo kama haya munakaa vikao na kusema hatuna uhuru wa Habari nchi. Kama unakubali kununuliwa na ukanunulika unadhani uhuru utakuwepo kweli? Tumezichoka habari za kusikia hatuna uhuru wa vyombo vya habari nchini huku ninyi wenyewe mkiwa mstari wa mbele kuwasaliti wananchi. Munategemea nini? Fedha za leo zitawatawala ninyi wenyewe hapo kesho. Mara nyingi ninyi munakuwa mstari wa mbele baadaye kusema kiongozi huyu ni mbaya, hafai na kumwangika vichwa vya habari vya kumkejeli baada ya kupata madaraka.

Kama mimi ningekuwa ndiye Rais wan chi hii ningemshinikiza waziri anayehusika na masuala ya vyombo vya habari andaye mswada mpya zaidi wa kuvinyonga vyombo vya habari ili wakose uhuru zaidi. Kwani kiasi cha uhuru uliopo wameshindwa kukitumia. Mambo ya kuzungumzia yapo mengi ten asana kila kona. Hivi swali lenu ni hili, je umewai kutembelea vijijini kule na kuona nyakati za mvua wanaishije? Wanakula nini? Adha gani wanayokutana nayo?

Hivi ni kweli vitu vya kuzungumzia kwenye vyombo vyenu vya habari (Media) vimekwisha kabaisa? Au munataka wananchi waandamane pamoja na kuwalamba mboko ili muandike habari zao na muwatumikie vyema? Hivi munadhani hiyo elimu yenu bila wananchi mungeza kuipa? Utitili wa magazeti sasa unathibitisha usemi wangu kuwa wanaripoti habari mbalimbali ili kulinda maslahi ya watu wachache badala ya umma.

Mutazame maeneo ya Ngorongoro watu wanavyoteseka na Njaa, Tunduru hadi leo korosho hazinunuliwi na wananchi hawajui lini zitanunuliwa huku watu binafsi wakinunua kangomba za korosho kwa bei ya shilingi 500 kwa kilo. Ninyi waandishi muko wapi? Kwanini musiripoti habari kama hizi zinazooneka ni za ulanguzi. Maisha ya wanatunduru msimu huu wa mvua yanakuwa hali tete? Chakula chao kikuu ni ugali wa muhogo wa wa kuloweka kwenye maji na kukausha ambao hauna virutubisho mwilini. Na mvua zinapochanganya watu hushindwa kula na wengine hushindia miogo ya kupika au uji.

Nakumbuka mwalimu wangu Mama Mushi wa somo la NEWS REPORTING Chuo kikuu MT. Augustine Mwanza alinifundisha kwamba Greater The Name Greater The News, And Greater the Event Greater the New”. Ila hili neon lisitumike visivyo ili kuweza kuwanyima na kuwafunga midomo wananchi. Pamefikia mahari mtu unahamua kuaghahilisha kununua Gazeti Fulani kisa linapendelea sana upande Fulani wa chama au kundi la watu wataka Madaraka badala ya kuwazungumzia wananchi na shida zao zinazozidi kuongezeka siku hadi siku na zitazidi kuongezeka siku hadi siku.

Inawezeka waandishi wetu wanafanya haya kwa sababu vyombo vya habari vilivyo vingi nchini vinamilikiwa na wenye fedha na wanasiasa hivyo wanalazimika kuandika au kuripoti kile basi wao anachohitaji. kwa mfano kama mimi ningekuwa namiliki vyombo vya habari basi nikilala nikiamka natoa amri kesho magazeti au media zangu zote munilipoti kwamba nimetoa msaada huu ili nionekana nafanya mema kwa wananchi kumbe moyoni ni danganya toto.

 HivyoViongozi wetu tunawaomba muwatumikie wananchi vilivyo ili kuweza kuleta ufanisi zaidi na kupunguza lindi la umaskini linaloikabili nchi yetu. Masuala ya uchaguzi 2015 yasiwe ndio kikwazo kwa maendeleo ya nchi yetu Tanzania. CCM na CDM na vyama vingine muwatumikie wananchi kwanza na sio kulumbana juu ya uchaguzi 2015 na badala yake mufanye kama mulivoagizwa na wananchi. Je ukifika mwaka 2015 utawaeleza nini hao wananchi waliokuchagua kuwa kiongozi wao? 

Makala hii Imeandikwa na Chiwambo Ausi
TEOFILO KISANJI UNIVERSITY (TEKU)
E-Mail: Ausichiwambor@hotmail.com

Saturday, December 22, 2012

HOTUBA YA MBUNGE WA BASO MH. TWEVE NEHEMIA J.


HOTUBA NILIYOITOA TAREHE 21 DECEMBER 2012 JIMBONI KWANGU;
Waheshimiwa, viongozi wa darasa Bugoya Ally I, na makamu wako Sara Samwel.
Waheshimiwa, viongozi wa TEKUBA, mabibi na mabwana.
Awali ya yote napenda kumshukuru mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na mwenye kudra juu ya maisha mema.
Pole zangu ziwafikie wenzetu woote waliofikwa na matatizo katika kipindi choote cha nyuma hadi tulipo sasa.
Baada ya yote napenda kutoa shukrani zangu za dhati sana kwenu nyote kwa kutosimamisha mgombea mwingine yeyote katika nafasi ya ubunge wa jimbo letu, Hii ni kuonyesha imani mliyonayo juu yangu na nafasi ya uwajibikaji wangu ndani ya serikali ya wanafunzi ya chou chetu, Ni uhakika wangu kuwa hamkufanya kosa kwani nimehakikisha ninawatumikia wananchi wangu kwa kadri ya uwezo wangu na mamlaka yanguu ndani ya ofisi ya bunge na pia hata katika ofisi ya wizara ya mikopo.
Ndugu zangu nilipoteuliwa kushika nafasi ya kuwa naibu waziri wa pili wa mikopo nilijisikia vizuri kwa sababu ni nafasi adhimu si kwa Tweve bali kwa kitengo chetu cha elimu jamii, kwa maana hiyo basi sisi kama watu wa elimu jamii tunayo adhima kubwa ya kuwatumikia wananchi kwani vyeo tulivyonavyo ni dhamana.
Salamu zangu za pongezi ziwaendee pia BUGOYA ALLY I na SARA kwa kuchaguliwa kuwa viongozi wapya wa darasa letu, kwani hadi sasa uongozi wao umefana na mimi kama mbunge ninatoa kauli yangu kuwa hakuna kiongozi anayeweza kuonekana mzuri kwa watu wote pindi anaposhika hatamu (uongozi)
Napenda kutumia fursa hii kipekee sana kumshukuru Mh. Chiwambo na makamu wake Mote Dorothea ambao ni wastaafu kwa sasa, utumishi wao ni mzuri na tena umetukuka, hongereni sana.
Ndugu zanguni, wanafunzi wenzangu, ilihali hatuwezi kukaa na makaa ya moto yakiwa mifukoni mwetu ni lazima tufikie hatua ya kujadili baadhi ya mambo mahususi ndani ya letu, ni wiki chache tu nilipotoa namba yangu ili watu waweze kutuma mambo mbali mbali yanayohusu jimbo letu.
Ifahamike kwamba ni matarajio yangu makubwa kuwa hotuba yangu haitokuwa kichochezi cha kuwamega wanabaso wala kuwatenga kutoka kwenye umoja uliopo hivi sasa, Bali hotuba hii fupi inalenga kuweka msingi wa umoja endelevu, ushirikano upendo na mshikamano;
Ndugu zangu nilitoa fursa hii ya kunitumia mambo mbali mbali kupitia njia ya simu kwani mtiririko wa maswali ambayo pengine sikuwa na majibu yamezidi na huku mambo niliyonayo ni mengi sana kwa hiyo nilishindwa kuyajibu na kuamua mkutano wa pamoja ambao tunaufanya leo. MAMBO HAYA NI:-
v Mchango wa TEKUBA ni mkubwa kiasi cha kuathiri utayari wa watu kuchangia kwa uhakika, na hata katika michango hiyo inaonekana dhahiri kuwa madhumuni yamejikita katika starehe na sio katika kusaidiana sisi kwa sisi na hata hivyo ni jukumu letu sote kushiriki katika utoaji wa maoni ya katiba ya TEKUBA.
v Michango inayohusu kufiwa ipewe kipaubele hasa kwa pale matatizo ya kufiwa yanapokuwa ni very sensitive kwa muhusika wa tukio la kufiwa, na ikumbukwe kuwa wananchi wanataka ufuatiliaji wa michango ufanyike chini ya uongozi unaotambulika na unafahamika kwa wote na hata hivyo michango ya pongezi kama vile kwa mtu aliyejifungua, na kutuma pongezi za aina yoyote ile ifanyike chini ya uhiari wa mtu na si kufanya ulazima na kutangaziana matangazo kwa kuhimiza ulazima wake.
v Na kwa wale wenye mashine/computer wafanyike msaada kwa wenzao na sio kufanya mashine kuwa chanzo cha mapato ilihali hawafanyi biashara yoyote mfano mzuri ni pale mtu anapoamua kuwatoza wenzake hela kubwa kwa kiasi cha zaidi ya Tshs 5000 na katika hali ya kawaida hakuna kazi inayoweza kuchapwa kwa hela hiyo na hili linaambatana na suala la kukataa kumwandika mtu jina ilihali yupo tayari kuchangia hela ya kuprint kazi na kueleza kile kilichomfanya asiwepo katika mchakato wa kufanya kazi hiyo.
 Mwisho kabisa kwa mapenzi ya dhati kabisa napenda kusisitiza kitu kwenu wenzangu kuhakisha kwamba tunakuwa watu wa mbele kutembelea blog yetu ambayo mmiliki wake yundani yetu, mimi kama mbunge ninachukulia kama ni blog yetu sote na ninajivunia sana kwani ni kitu cha msingi kufanywa na mwenzetu mpendwa na ninaona ni mtu kwanza pengine kufanya kitu kama hiki ndani ya kitenngo cha elimu jamii.
Aidha mimi kama mbunge napenda kuwahimizeni nyoote kujiunga na Asasi ya umoja wa mataifa iliyo na tawi lake hapa chuoni kwani ni muhimu kwetu kama watu wa elimu jamii.
NAWATAKIA SAFARI NJEMA NA SIKUKUU NJEMA ZENYE BARAKA TELE, MUNGU IBARIKI BASO, MUNGU IBARIKI TEKU, MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRICA.
NINAOMBA KUWASILISHA.
 

TWEVE NEHEMIA J (MBUNGE NA NAIBU WAZIRI WA MIKOPO)
P O BOX 20,
NJOMBE, TANZANIA.
ntweve@gmail.com
 +255776047873


Thursday, June 21, 2012

BUSARA ITUMIKE KUZUNGUMZIA MGOGORO WA ZANZIBAR


BUSARA ITUMIKE KUZUNGUMZIA MGOGORO WA ZANZIBAR
Chiwambo Asi R.
Zanzibar mwishoni mwa wiki iliyopita tulishuhudia machafuko makubwa sana. Ikihusisha vitendo vya uchomaji wa makanisa, uhalibifu wa mali za umma, na wengine kuwekwa ndani. Hili si jambo tu la kukurupuka na kuanza kubeza sana upande mmoja kwani kila jambo ni matokeo ya mfumo Fulani.

Taasisi iliyoingia kashfa hiyo ni Taasisi ya UAMSHO ikiwa chini ya baadhi ya waislamu Zanzibar. Zanzibar wanataka nchi yao iwe huru, wakati watanganyika tunataka Zanzibar iendelee kuwa hru. Na cha kusikitisha zaidi lile baraza la usuruhisho masuala ya muungano ni raia wa Zanzibar. Hakuna Mtanganyika pale.

Ofisi inayohusika na masuala ya muungano ni ofisi ya Makamu wa rais. Na hata walio kwenye kamati hiyo wote ni  Wazanzibar. Hivi unadhani kama ikitokea wao hawautaki muungano unadhani kwamba wataleta majibu yaliyo sahihi? Hawa ni viongozi wetu, tuendelee kuwaamini kwani tushike ule usemi usemao kiongozi ni kioo cha jamii.

Makundi yeyote yanavyoanzishwa huanza na  Hatua (stage) zake. Kila hatua inajitegemea kama ifuatavyo:-
  1. Hatua ya kwanza ya kuunda Kikundi. (Preliminary or incipiency stage). Hapa ndipo vichwa vya watu vinapogongana kimawazo juu ya kit Fulani kwenda tofauti. Viongozi hutokea ambao si rasimi na kuanza kuonesha hisia zao.
  2. hatua ya pili ambayo inahsisha kuanza kutengeneza kundi na kuongeza uelewa kwa watu (Coalescence stage). Hapa panahitaji viongozi ambao wataongeza ukaribu na watu wengine. Kipindi kingine wanazungumzia mawazo yao yote hata kupitia vyombo vya habari.
  3. hatua ya nne ambapo kikundi kimekomaa na kufikia kilele cha kundi (Institutionalization or Bureaucratization stage). Hapa viongozi wanakuwa ni wakuchaguliwa na ufata mfumo wa taasisi Fulani (chain of command). Na viongozi hao hulipwa kiasi cha fedha.
  4. Anguko. (Decline stage).hapa ni sehemu ya mwisho kabisa ambapo ni anguko ku la kundi lililoundwa katika hatua ya kwanza. Hapa kundi hili usambaratika kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kufanikiwa kwa lengo lao, au kusambaratishwa.

Hizo ndizo hatua za makundi yanavyotokea. Hivi viongozi wetu hawakuziona hatua kama hizi? Kama kweli tunautaka muungano kwanini serikali iliwaachia uhamsho kuendesha mijadala yake huku wakijua kuwa wanazidi kulikuza zaidi kundi hili? Huu ni uasi au ni nini? Kwa upande wangu naona kwamba ni uzembe wa watu wachache ndio uliopelekea visiwa vya Zanzibar kuingia kwenye machafuko.

Kwa kiongozi yeyote aliyesomea masuala ya uongozi au jamiii lazima amezisoma hatua kama hizi na namna ya kuyasambaratisha haya makundi. Kwanini zisitumike ikiwemo njia za amani. Makundi haya yalipata uchungu zaidi pale viongozi wa taasisi zisizo za kiserikali walipokamatwa na jeshi la polisi katika eneo la bunge kwa madai kuwa ni kinyume na sheria za nchi kwa kifupi nilivyoelewa mimi ni kwamba walikuwa waasi. Ni kweli kabisa.

Lakini ilipaswa itumike busara kutatua mgogoro huu badala ya vitisho. Hawa Wazanzibar walianza kudai Zanzibar ijitenge kwa muda wa miaka mingi sana. Kwa wale wenye kumbukumbu munaweza kumkumbuka yle aliyekuwa rais wa Zanzibar Ndugu Aboud Jumbe Mwinyi alivyotangaza nia ya kutaka kuvunja muungano akiwa Dodoma kwenye vikao Fulani. Kilichompata ni kuondolewa klatika nafasi hiyo.

Nyadhifa zake zote za kichama na serikali alivuliwa kufumba na kufumbua macho. Hii ni kweli kuwa uasi ulianzia muda mrefu sana. Hapo ndipo Mwalimu Nyerere aliposema kuwa tusikubali kuvunja muungano. Hata Nyerere wetu kumbe aliyajua haya mapema hasa pale kundi la G51 lilivyoanza kukua nchini Tanzania.

Kwa hiyo suala la hawa jamaa wa UAMSHO chanzo chake kimetoka mbali. Kwa hiyo kwa wakati huu ambao nchi mbalimbali zinaonyesha namna waasi wanavyoongezeka siku hadi siku, hasa nchi zile za kiarabu na baadhi ya nchi za Kiafrika, napendekeza serikali bora itumie busara zaidi katika kutatua tatizo hili badala ya vitisho na nguvu nyingi. Kweli hawa watu wapo kinyume cha sheria za nchi.

Lakini busara muhimu zaidi kuliko nguvu zaidi. Kwanini serikali isikae nao pamoja na kanza kusikiliza madai yao? Kama yana msingi kwa hatima ya nchi yetu yafanyiwe kazi. Mbona madaktari ilitumika njia kama hii. Kwanini isitumike kule Zanzibar. Inasikitisha kuona kila kukicha vituko Zanzibar mara tunataka nchi yetu.

Haya yamefugwa sana na sisi wenyewe kwani viguvugu lilipoanza hasa katika ule muswada wa maoni ya katiba mpya hawa walichana hadharani na kupinga kujadiliwa. Wakati ule likuwa muhimu kuweza kutafta njia mbadala za kutatua ili kuonyesha namna tunavyoujali muungano wetu.

Nalipenda sana Tanzania hasa hili jina zuri la Tanzania. Kwa hiyo nadhani viongozi wa serikali mutatumia wawazo haya ili kuhakikisha tunabaki na Tanzania moja, Imara na yenye amani na utulivu kama aliotuachia mwalimu Nyerere.

Powered by Chiwambo Ausi R.       

MWANAHARAKATI NA TANZANIA YA LEO


MWANAHARAKATI NA TANZANIA YA LEO

Hapo mwanzo katika kijiji kimoja kulikuwa na vijana wenye nguvu na waliopigania nchi yao kuwa huru. Nchi hiyo ilijulikana kwa jina la Kuabudika, na ilikuwa na miji mikubwa kama sita. hali ya jiji la kwanza ilikuwa sawa na yale mengine. kila kukicha nchi hii maarufu kwa utajili wa kila aina ilibadilika. maisha yalikuwa bora ya jana kuliko leo kikicha. nimesahau kuanza na neno hili "hadithi hadithi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!" hadithi hadithi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!".

yale majoho waliyozoea kuvaa kila siku wale wenye nazo ilifikia mahali bei ilipanda kiasi kwamba kama ni mfanyabiashara ndogondogo ununuapo joo moja fedha za mtajiulikuwa kwaheli. watu walilalamikia juu ya nchi yao. Nchi hii ilikuwa na sifa kubwa yenye viongozi wanaotabili nini hapo baadaye kitatokea na nani aondolewe wapi hapelekwe wapi. kiongozi aliyeamishwa akikataa kufanya hivyo hatima yake ilikuwa ni kifo tu.

Hali ilikuwa vile hadi walipozaliwa watoto mapacha watatu waliofanana kwa kila sifa. walikuwa wakakamavu, wazuri, wenye nia ya kukomboa nchi yao na walitembea wakati wote pamoja. walitumia muda wao wote kusoma kuanzia darasa la kwanza hadi la nane wakiwa na wazazi wao wateule. watoto hawa walipendana sana, walivaa sare vizuri ijapokuwa uwezo wao ulikuwa mmmmmmmmmmm.

Mungu aliwabaliki wale watoto watatu na kufahuru darasa la nane shule ya msingi Majaribu iliyoko wilaya ya Chinyauleje kata ya Kweko. walichaguliwa kuingia kidato cha kwanza na kumaliza kidato cha nne shule ya sekondari Achimwene. mungu aliwabaliki kusomea masomo ya uasikari katika kikosi maalumu. majina ya wale wote yalikuwa "HUZUNI, AMANI NA UTULIVU". baadaye walifanikiwa kwenda kikosi kingine cha masomo ya juu ya uasikari na kuwa makomando wa jeshi.

Hawakulidhika na mishahara waliyopewa kwani walikuwa na ndoto ya kuikomboa nchi yako. Vijana hawa waliamua kuacha kazi na kuendelea na masomo ya chuo kikuu. walisoma chuo kikuu cha Mwanaharakati kilichopo nchi nyingine ya Ahadi. walisoma masomo ya "BA-political science and International Relatioship".

baada ya kutunukiwa Shahada zao walirudi Nyumbani Nchi ya "Kuabudika". siku ile ilikuwa siku ya ajabu kubwa sana. vijana walifuatwa na ndege ya Wanamapinduzi. safari ilianza saa sita mchana. safari ile ilikuwa ni ya siku mbili. waliingia nchini mwao mnamo saa 8.00 mchana. nchi ilianza kutikisika ghafla kabla ndege kutua uwanja maarufu wa St. Ambuje. Mchana kukawa giza nene kama manane ya usiku. nchi ilikuwa nyeusi ikiashiria kuingia kwa wakombozi watatu kutoka Mwanaharakati university.

Ndege ilitua chini, ghafla mchana ulilejea. Kiongozi wa nchi lle maarufu kwa jina la NJETE JA KWEKULA", ALIAGIZA VIJANA WALE WATATU WAUWAWE HARAKA IWEZEKANAVYO KWANI MTABRI WAKE MAARUFU ALITABIRI KUWA VIJANA WALE WA WATATU MMOJA KATI YAO ATAKUWA MTAWALA WA NCHI LE.

ikumbukwe kuwa yule raisi alijiweka madarakani ni kiongozi wa maisha. hakukuwa na uchaguzi wa rais katika nchi ile, yeye aliteua wabunge na viongozi wote wa serikali. yeye ndiye Hakimu na jaji mkuu wa nchi ile. na wazizi wa wae watoto waliuawa na rais wakati watoto hawa wakiwa wachanga sana baada ya rais wa nchi hiyo kuwatuhumu kwa kutaka kufanya mapinduzi.

Wakiwa uwanja wa ndege wale vijana watatu waliwekwa chini ya ulinzi na kikosi maalumu cha makomandoo. ilikuwa patashika vijana wale kukamatwa. vurugu kali ilitokea. na wakati huo huo watu walikuwa wamejaa barabara zote kuzunguka kiwanja maarufu cha ndege. barabara zote zilijaa watu kwa kuwa waliona wanamapinduzi walikuwa wanaingia siku ile. vijana wale walitakiwa kuzungumza na wananchi ili kuzungumzia nini hatima ya nchi yao ambayo uchumi ulishuka kiasi kwamba thamani ya fedha ilishuka hata mkate ulikuwa haushikiki kwa bei mbaya.

wote watatu walikamatwa palepale uwanja wa ndege na kupandishwa ndege maalumu ya jeshi na ndege kupaa tena kuelekea uwanja wa dhambi tayari kwa kunyongwa kama hukumu inavyonesha.

wakati ule vyombo vya habari vilikata matangazo ghafla. wananchi walishangaa sana kuona mgeni wao anapandishwa ndege ya kijheshi na kupaa juu. ghafla mabomu ya machozi yalianza kuvuma huku na kule. watu waliuwa sana. yale yalikuwa mauaji makubwa kuliko yote Tangu nchi ile Iumbwe na Mwenyezi Mungu.

watu waliuwawa makanisani, misikitini, mitaani na maeneo yenye mkusanyiko. hali ilikuwa mbaya tena mbaya sana. watu milioni moja waliuwawa. hapo ndipo sheria mbaya zaidi zilivyoongezeka. katiba ya nchi ilibadilishwa na kunyima uhuru wa vyombo vya habari, maandamano pamoja na mikusanyiko.

siku ile ya mauaji umji ulijaa maiti kiasi kwamba watu walisema leo ndio mwisho wa dunia. Miezi ishirini na nne ilipita, hatima ya nchi haijulikani. wannchi hawajui wale wakombozi wao wamepelekwa wapi. na mtu hana haki ya kuongea juu ya mstakabali wa nchi yao. watu waliamini mungu ndiye aliyesababisha hali hiyo ya nchi. nchi ilikuwa maskini ya mwisho katika dunia ile. watu waliishi bora jana kuliko leo na walikuwa wanasubiri kufa tu maana hakukuwa na namna ya kuwezakuendesha nchi yao.

vijana wale baada ya ya safari ya siku mbili wafikishwa msitu mnene wa "CHIKANJE". msitu ule watu huwa ni chakula cha wanyama. wale askari waliopewa kazi ya kuwanyonga wale vijana watatu, walianza kuwaambia kuwa "nyinyi mlikuwa ni makomandoo wa jeshi, mliacha kazi ya uasikali kwenda masomoni ili kuikomboa nchi yetu. na rais wa nchi hii ametoa amri ya kuuawa kwenu. mnatakiwa muuawe mara moja................................................................................................................. ni amri.

mungu si athumani. mungu amtupi mja wake. wale asikari wanyongaji walikaa kikao cha ghafla. loo!!!!!!!!!!!!. askari mmoja alisema "haiwezekani watu hawa wauawe". mmmmmmmmmm! la hasha!!!!! penye nia pana njia. askari walitafakari na kufikia hatima ya wale vijana watatu. askari wale waliamua kuwaachia huru wale vijana watatu kwa masharti maalumu.

Walikaa kikao cha ghafla na wale watuumiwa watatu. waliwafungua pingu na kuanza kupanga mikakati ya kuipindua nchi. waliweka kila njia na mipangoyote ilikaa vizuri. walipanga wale watakuwa na ulinzi wa jeshi la nchi hiyo. katika mikakati yao ilikuwa ni kumteka kiongozi wa jeshi wa nchi ile na kisha kumalizia kwa rahisi. haraka haraka haina baraka, mmoja wa askari kwa cheo cha Copro Antinion Mwangatu-mbujiko. kazi ilianza mara moja.

kama mungu alipanga hivi. wananchi wa nchi ile waliamka asubuhi bila ya kuamshwa na kuanza kuandamana bila ya kiongozi. kila kijiji, katani, wilaya ,miji na majiji yaliandamana. watu walikuwa wachungu kama pilipili kichaa. Habari ndiyo hiyo kila kona ya jiji. Wananchi walibeba mabango yaliyoandikwa "MAPINDUZI NI LAZIMA, RAIS HATUKUTAKI, LAZIMA UONDOKE, PIGA UA GALAGAZA NCHI HII SI YAKO, RAIS ONDOKA TUPATE AJIRA NA  mengine mengi". kumbe hali ile ilitengenezwa na jeshi la nchi ile na wale vijana watatu wa chuo kikuu.

Askari wote wa nchi waliwatetea wananchi, hakuna aliyeuawa na askari kama ilivyokuwa mwanzo, katiba haikufuatwa kwa askari kuruhusu wananchi waandamane, na kuwapa mabango. kipindi wananchi wakiandamana jeshi la nchi hiyo ilimteka kamanda wa jeshi la nchi hiyo Meja General MWE ULI.

Rais alishangaa ghafla kuona wananchi wanakaribia kasili wakiwa na mabango ya ya maandamano pamoja na silaha kali wakisindikizwa na jeshi la nchi hiyo huku ndege za jeshi za kiita zisizo na rubani na zenye rubani zikiwa na siraha nzito nzito ikiwemo mabomu mazito mazito.

wananchi wa nchi ile walifanikiwa kuiteka ikuru na kumchoma moto Rais wa nchi ile. habari yake iliishia pale. mara ya mwisho yule rais kabla ya kifo chake alisema "KWELI NGUVU YA UMMA..................................................................................................................................................................."

LEO HII NAUKUMIWA BILA KUTAKA KISA UONGOZI WANGU ULIKUWA MBAYA" MUNGU NISAIDIE NIFIKA PAHALA PEMA PEPONI" Wananchi walisema "ameeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee" wengine walisema Amina". 

POWERED BY CHIWAMBO AUSI R, TEKU UNIVERSITY, 2012